Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 7/15 kur. 24-25
  • Msamaria Mwenye Ujirani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msamaria Mwenye Ujirani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Msamaria Mwenye Fadhili za Kijirani
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Msamaria Athibitika Kuwa Jirani wa Kweli
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Msamaria Athibitika Kuwa Jirani Mwema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Jirani Mwema
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 7/15 kur. 24-25

Maisha na Huduma ya Yesu

Msamaria Mwenye Ujirani

LABDA Yesu amekaribia Bethania, mji ambao uko umbali unaokaribia kilometa 3 kutoka Yerusalemu. Mwanamume mmoja ambaye ni stadi katika Sheria ya Musa amwendea akiwa na swali, anauliza: “Mwalimu, kwa kufanya nini mimi nitarithi uhai wa milele?”

Yesu anaona kwamba mwanamume huyo, mwana-sheria, haulizi tu ili apate habari bali anataka kumjaribu. Huenda kusudi la mwanasheria huyo likawa kwamba anataka Yesu atoe jibu katika njia ambayo itachokoza itikadi na wepesi wa kuona mambo wa Wayahudi. Kwa hiyo Yesu anamfanya mwanasheria huyo ajifunge mwenyewe, kwa kuuliza: “Ni nini ambacho kimeandikwa katika Sheria? Wewe unasoma jinsi gani?”

Kwa kujibu, mwanasheria huyo, akionyesha mtazamo wa ndani usio wa kawaida, ananukuu kutoka kwa sheria za Mungu kwenye Kumbukumbu la Torati 6:5 na Mambo ya Walawi 19:18, NW, akisema: “Lazima upende Yehova Mungu wako kwa moyo wako mzima wote na nafsi yako nzima yote na uthabiti wako mzima wote na akili zako nzima zote,’ na, ‘jirani yako kama wewe mwenyewe.’”

“Umejibu sawasawa,” Yesu anaitikia. “Endelea kufanya hili na wewe utapata uhai.”

Hata hivyo, mwanasheria huyo hakuridhika. Jibu la Yesu si mahususi kwake. Anataka uthibitisho kutoka kwa Yesu kwamba rai zake ni sahihi na kwa sababu hiyo yeye anawatenda wengine kwa uadilifu. Kwa hiyo anauliza: “Jirani yangu ni nani kwa kweli?”

Wayahudi wanaitikadi kwamba neno “jirani” linatumika kwa Wayahudi wenzao tu, kama vile mistari inayozunguka Walawi 19:18 NW, inavyoonekana kuwa inaonyesha. Kwa kweli, baadaye hata mtume Petro alisema: “Ninyi mnajua jinsi lisivyo jambo la kisheria kwa Myahudi kujiunga mwenyewe au kumwendea mwanamume wa kabila lingine.” Kwa hiyo yule mwanasheria, na labda wanafunzi wa Yesu pia, wanaitikadi kwamba wao ni waadilifu ikiwa wanawatendea Wayahudi wenzao tu kwa ufadhili, kwa kuwa, kwa rai yao, watu wasio Wayahudi si majirani wao kweli kweli.

Yesu anaweza kurekebishaje rai yao bila kuwatia uchungu wasikilizaji wake? Yeye anasema hadithi, labda ikitegemea jambo lililotukia kikweli. “[Myahudi] fulani,” Yesu anaeleza, “alikuwa akienda kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko na akaanguka miongoni mwa wanyang’anyi, ambao wote walimvua yeye na kumtia mapigo, na wakaondoka, wakimwacha akiwa nusu mfu.”

“Sasa, kwa kutotazamia,” Yesu anaendelea, “kuhani mmoja alikuwa akienda katika barabara hiyo, lakini, alipomwona yeye, alienda kwenye upande ule mwingine. Vivyo hivyo, Mlawi pia, alipofika kwenye mahali hapo na kumwona yeye, alienda kwenye upande ule mwingine. Lakini Msamaria mmoja akisafiri njia hiyo alikuja kwake na, kwa kumwona yeye, alisukumwa na sikitikio.”

Makuhani wengi na wasaidizi wao Walawi wa hekaluni wanaiishi Yeriko, umbali wa kilometa 23 ambayo inatelemka meta 900 kwenye njia hatari kutoka mahali ambapo wanatumikia kwenye hekalu katika Yerusalemu. Kuhani yule na Mlawi wangetazamiwa kusaidia Myahudi mwenzao akiwa taabani. Lakini wao hawafanyi hivyo. Badala yake, Msamaria anafanya hivyo. Wayahudi wanawachukia Wasamaria sana hivi kwamba karibuni walimtukana Yesu kwa maneno makali sana kwa kumwita “Msamaria.”

Msamaria yule anafanya nini ili asaidie yule Myahudi? “Yeye alimwendea,” Yesu anasema, “na kuvifunga vidonda vyake, akimwaga mafuta na divai juu yavyo. Kisha akapandisha yeye juu ya hayawani wake mwenyewe na kuleta yeye katika mkahawa na kutunza yeye. Na siku ya pili alitoa dinari mbili [karibu mshahara wa siku mbili], na kumpa mtunzaji wa mkahawa, na kusema, “Tunza yeye, na cho chote utakachotumia zaidi ya hiki, mimi nitakulipa wewe nitakaporudi hapa.’”

Baada ya kusimulia hadithi hiyo, Yesu auliza mwanasheria yule: “Ni nani kati ya watatu hawa anayeonekana kwako kuwa alijifanya mwenyewe kuwa jirani kwa mwanamume yule ambaye alianguka miongoni mwa wanyang’anyi?”

Akihisi kuwa jambo lisilofaa kumpa Msamaria sifa yo yote, mwanasheria yule anajibu hivi kwa urahisi: “Yule aliyetenda kwa rehema kuelekea yeye.”

“Enda njia yako na uwe ukifanya vivyo hivyo wewe mwenyewe,” Yesu anamalizia.

Kama Yesu angekuwa amemwambia moja kwa moja mwanasheria yule kwamba watu wasio Wayahudi ni jirani zake pia, mwanamume huyo hangekukubali hilo tu bali yaelekea walio wengi katika hadhirina wangekubaliana naye katika mazungumzc yake pamoja na Yesu. Hata hivyo, hadithi hii ya kweli iliyotokea maishani, ilionyesha waziwazi katika njia isiyoweza kukanushwa kwamba majirani zetu wanatia ndani watu zaidi ya wale wa kabila au taifa letu tu. Lo! njia ya ajabu jinsi gani aliyo nayo Yesu ya kufundisha! Luka 10:25-37; Matendo 10:28; Yohana 4:9; 8:48, NW.

◆ Mwanasheria aliuliza Yesu maswali gani, na kwa wazi ni nini lililokuwa kusudi lake la kuuliza?

◆ Wayahudi waliitikadi ni nani waliokuwa majirani wao, na kuna sababu gani kuitikadi kwamba hata wanafunzi walishiriki rai hii?

◆ Yesu alionyeshaje rai iliyo sahihi hivi kwamba mwanasheria huyo hangeweza kuikanusha?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki