Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 8/1 uku. 3
  • Mifano ya Kidini Wewe Una Maoni Gani Juu Yayo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mifano ya Kidini Wewe Una Maoni Gani Juu Yayo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Sanamu Zaweza Kukuleta Karibu Zaidi na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Kuzipa Sanamu Heshima Kibishanio
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Maoni ya Kikristo Juu ya Mifano
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Sanamu
    Amkeni!—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 8/1 uku. 3

Mifano ya Kidini Wewe Una Maoni Gani Juu Yayo?

KATIKA 1888 kulikuwa na mfuriko mkubwa katika Canton, China. Mvua yenye kuendelea iliangamiza mazao. Kwa kutojua la kufanya wenye vishamba walisali kwa mungu wao Lung-wong ili akomeshe miminiko lile la mvua, lakini wapi. Kwa kutiwa kasirani na kutojali kwa mungu wao, wao walitia mfano wake katika jela kwa siku tano! Miaka fulani kabla ya hapo, mungu huyo huyo alikuwa amepuuza sala zao za kumaliza ukavu fulani. Wao waliweka mfano wake kule nje katika joto kali sana ukiwa umefungwa mnyororo.

Katika 1893 ukavu ulikumba Sisili. Maandamano ya kidini, mishumaa yenye kuwashwa katika makanisa, na sala zenye kutolewa kwa mifano, yote hayo yalishindwa kutokeza mvua. Wakiwa wamekosa saburi, wale watu wenye vishamba waliivua mifano fulani kanzu zayo, wakageuza nyuso za nyinginezo zielekee ukutani, na hata wakachovya mingine katika vidimbwi vya kunyweshea farasi! Katika Licata, “Mtakatifu” Angelo alivuliwa mavazi, akafungwa minyororo, akatukanwa, na kutishwa kunyongwa. Katika Palermo Italia, “Mtakatifu” Joseph alitupwa katika bustani iliyokaushwa na joto kali ili angojee mvua.

Vituko hivi, vilivyosimuliwa katika kitabu The Golden Bough, kilichotungwa na Bwana James George Frazer, vinaashiria mambo ya kufadhaisha. Vinaonyesha kwamba wote wawili, wenye kudai kuwa ni Wakristo na wale wasio Wakristo, wanaelekea kuwa na rai (maoni) zinazolingana juu ya mifano ya kidini. Katika visa vyote viwili, waabudu walitumia mifano yao kama njia ya kupashana habari na “mtakatifu” au mungu fulani. Na kwa kupendeza, wote wawili walijaribu kuchochea “watakatifu” au miungu yao yenye uchelewevu ifanye kitendo kwa kuiadhibisha hali zile zisizo za starehe zilizokuwa zikipata waabudu wayo.

Ingawa hivyo, leo watu wengi wanaotumia mifano ya kidini wangekuwa na rai ya kwamba vitendo hivyo vinapita kiasi, labda hata vinastahili kuchekwa. Wao wangetoa hoja ya kwamba kwa maoni yao mifano ni vitu vya kupewa staha tu​—si ibada. Huenda hata wakadai kwamba sanamu-umbo, misalaba, na michoro ya kidini ni misaada halali katika kuabudu Mungu. Labda wewe unahisi hivyo hivyo. Lakini swali ni: Mungu anahisi jinsi gani juu ya jambo hili? Je! ingeweza kuwa kwamba, kwa kweli kustahi mno mfano ni sawa na kuuabudu? Je! inawezekana kwamba kwa kweli mazoea hayo yana hatari zilizofichika?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki