Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 12/1 kur. 21-23
  • Kuhitimu kwa Darasa la 85 la Gileadi Pindi Yenye Shangwe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhitimu kwa Darasa la 85 la Gileadi Pindi Yenye Shangwe
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Shule ya Gileadi—Ina Umri wa Miaka 50 na Yaendelea Kufanikiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Wahitimu Wa Gileadi Waingia Njia ya Maisha Yenye Kuthawabisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Wamisionari Zaidi kwa Ajili ya Mavuno ya Duniani Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Makao Mapya kwa Ajili ya Shule ya Umisionari ya Gileadi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 12/1 kur. 21-23

Kuhitimu kwa Darasa la 85 la Gileadi Pindi Yenye Shangwe

KUFUATA mzinduo wa hekalu yapata miaka 3,000 iliyopita, Sulemani “aliambia watu waende zao kwenye maskani zao, wakiwa na shangwe na wakihisi vyema moyoni.” (2 Nyakati 7:10, NW) Maneno hayo yanaeleza vizuri hisia za watu zaidi ya 4,000 walipokuwa wakiliacha Jumba la Kusanyiko la Mashahidi wa Yehova katika Jiji la Jersey, siku ya Septemba 11, 1988. Ilikuwa pindi gani? Kuhitimu kwa darasa la 85 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi.

Baada ya wimbo mmoja, programu ilifunguka kwa sala yenye kuhisiwa moyoni ikitolewa na W. L. Barry, mshiriki wa Baraza Linaloongoza. T. Jaracz, ambaye pia ni wa Baraza Linaloongoza, alitenda akiwa mwenyekiti kwa siku hiyo. ‘Ili pindi hii iwe yenye kuburudisha kweli kweli na kujenga kiroho,’ akasema Jaracz, ‘roho ya Yehova na baraka zake zinahitajiwa.’ Kweli kweli, zilionekana wazi wakati programu ilipokuwa ikiendelea kusonga mbele.

Kufuata maelezo hayo ya ukaribishaji, wahitimu wakapokea shauri la kuwaaga likiwa katika hotuba fupifupi zenye mafaa. R. L. Rains wa Halmashauri ya Betheli ndiye aliyenena kwanza. Akifanya msingi wa maelezo yake uwe Mwanzo 12:1, 2, Rains aliwaonya kwa upole hivi wanafunzi hao: ‘Thibitikeni kuwa baraka katika mgawo wenu wa kimisionari.’ Nao wanaweza kufanyaje hivyo? ‘Ni kwa mwendo wa maisha yenu mkiisha kufika huko,’ yeye akakazia. Ndipo alipotilia mkazo mambo mawili ambayo yatasaidia sana: (1) Inawapasa wang’amue kwamba watahitaji kufanya mabadiliko fulani ili wapatanike vizuri na migawo yao mipya; na (2) wanapaswa kudumisha mahusiano yenye amani pamoja na wengine.

Aliyefuata katika kuongea kwa njia changamfu yenye kutia moyo alikuwa J. E. Barr wa Baraza Linaloongoza, akihutubia wahitimu juu ya kichwa “Tuongezee Imani,” msingi wacho ukiwa ni Luka 17:5. ‘Kumbukeni kila siku,’ Barr akahimiza, ‘kumwomba Yehova awaongezee imani.’ Lazima sikuzote wazingatie akilini sababu yenyewe hasa ambayo imefanya Yehova awatume kwenye migawo yao. ‘Hisini nguvu ya tengenezo la Mungu lisiloonekana na pia linaloonekana ikiwategemeza sikuzote, mchana na usiku,’ Barr akachagiza. ‘Hakuna wakati itakapokuwa kwamba mmeomba mara nyingi mno katika sala zenu kwa kusema, “Yehova, tafadhali niongezee imani.’”

Hamu iliamshwa wakati mwenyekiti alipotangaza kichwa cha mnenaji aliyefuata, F. D. Songer wa Halmashauri ya Kiwanda: “Itibari Isiyo na Kifani na Ufunguo Maalumu.” Songer alichota maelezo yake kutokana na 1 Nyakati 9:26, 27 na yanayosemwa humo juu ya watunza-malango Walawi. ‘Ofisi yao ilikuwa ya itibari isiyo na kifani, Songer akaeleza. Wao walikuwa na ufunguo​—kifaa ambacho kinaonyesha nguvu halisi ya kudhibiti mwingio wa maeneo matakatifu ya hekalu. Walikuwa watu wa kutegemeka, wakifungua malango kwa njia yenye kutegemeka kila asubuhi. Kwa kumalizia, Songer aliambia wahitimu hivi: ‘Nyinyi mmepewa itibari isiyo na kifani na ufunguo maalumu, kana kwamba ilikuwa, ili kuwafungulia asubuhi baada ya asubuhi wale wanaotafuta mwingio wa kwenda kwenye nyua za ibada ya kweli. Lindeni vizuri itibari hiyo na kutumia ufunguo huo kwa njia ya kutegemeka.’

Halafu, M. G. Henschel wa Baraza Linaloongoza akanena juu ya kichwa “Endelea Kushika Kigezo cha Maneno Yenye Afya.” Akirejeza kwenye 2 Timotheo 1:13, 14, AW, Ndugu Henschel alieleza kwamba shauri ambalo Paulo alimpa Timotheo kwa kumwaga lilikuwa: ‘Tumia kigezo hiki cha maneno yenye afya ambacho umepata kutoka kwangu, na ukilinde kama hazina, itibari.’ Wahitimu, pia, wamepokea hazina. Kwa miezi mitano iliyopita, wao walikuwa wamejifunza Biblia na mambo yenye kuhusu huduma. ‘Maagizo hayo, kigezo hicho cha maneno yenye afya,’ Ndugu Henschel akaeleza, ‘ni kitu ambacho Mungu ametia mikononi mwako ukitumie, si kwa ajili yako mwenyewe tu, hapana, bali kwa ajili ya wengine.’

Wakufunzi wale wawili wa shule hiyo wangekuwa na shauri gani la kuwaaga wanafunzi wao? J. D. Redford ndiye aliyenena kwanza juu ya kichwa “Kubali Makosa Yako.” Redford alisema kwamba ingawa sisi tunajua kwamba “sisi sote hujikwaa mara nyingi,” tukishtakiwa kuwa tumefanya kosa fulani, sisi huwa na elekeo la kujitetea haki. (Yakobo 3:2, AW) ‘Kukataa kukubali makosa yetu ni kama kudai kuwa hatuwezi kamwe kutenda lisilofaa,’ akasema Redford. Kukubali makosa yetu ndio mwendo wa hekima. Jinsi gani hivyo? Mnenaji alieleza hivi: ‘Hakuna mmoja anayeweza kudumisha staha ya wengine ikiwa anasisitiza kwamba ametenda sawa hata wakati anapokuja kuonyeshwa kosa lililo wazi. Mtu yeyote anawezaje kudumisha uhakika katika mtu ambaye kulingana na matukio ya huko nyuma anamjua kwamba yeye hata hugeuza ukweli ili tu aonekane anasema lililo sawa? Kukubali kosa hujenga imara ndani yetu, hali ya kujistahi. Lakini kutofanya hivyo ni jambo la kiwoga, na kunatudhoofisha kiadili.’ Bila shaka kutumia shauri hilo lenye mafaa kutasaidia wahitimu hao wachukuliane vizuri na wengine.

U. V. Glass, mkufunzi yule mwingine aliye pia mwandikishi wa shule hiyo, alifanya msingi wa onyo lake la upole la mwisho uwe usimulizi wa Biblia wa Gideoni, aliyetumiwa na Yehova kukomboa Israeli mkononi mwa Wamidiani. (Waamuzi, sura 6-8) Gideoni alionyesha kwamba uhakika ambao Yehova alikuwa nao katika yeye haukuwa usiofaa, kwa maana wakati watu walipotaka kumfanya awe mfalme, yeye alikataa, akisema: “Bwana [Yehova, AW] atatawala juu yenu.” (Waamuzi 8:23) ‘Nyinyi pia,’ akasema Glass, ‘hamtaki mwinuliwe juu. Nyinyi mmejithibitisha wenyewe. Lakini hiyo haimaanishi kwamba nyinyi ndio wenye kufanya pigano. Yehova ndiye anayewategemeza. ‘

Mnenaji wa mwisho asubuhi hiyo alikuwa A. D. Schroeder wa Baraza Linaloongoza, na alipokuwa akinena ilikuwa wazi kwamba Shule ya Gileadi ina upenzi mwingi moyoni mwake. Na kuna sababu njema​—yeye alikuwa ndiye mwandikishi wakati shule hiyo ilipoanzishwa katika 1943. Ndugu Schroeder alikuza kichwa “Upatikane Ukiwa Mwaminifu,” msingi wacho ukiwa ni 1 Wakorintho 4:2, AW. Kuwa mwaminifu kunahusisha nini ndani? ‘Kunaeleza hali ya mmoja ya kujawa na imani katika matangazo rasmi na ahadi zenye thamani kubwa za Yehova Mungu,’ Schroeder akaeleza. ‘Pia kunamaanisha kwamba mmoja ni wa kweli, mwenye kudumu bila ugeugeu, mshikamanifu kwa Yehova.’ Je! kuna vielelezo vyovyote vya wale ambao wamekwisha tayari kupatikana wakiwa waaminifu? Walikuwako wale wanaume na wanawake wa kabla ya Ukristo wanaotajwa kwenye Waebrania sura ya 11; Yesu Kristo; na mitume na wanafunzi wengine wapakwa-mafuta wa karne ya kwanza W.K. Baada ya kuvuta fikira kwenye vielelezo fulani vya ki-siku-hizi, Ndugu Schroeder aliuliza: ‘Namna gani sisi?’ Aliongezea hivi: ‘Ama wewe ni mwaminifu ama wewe si mwaminifu. Kama sisi ni sehemu ya wapakwa-mafuta au sehemu ya umati mkubwa, sisi sote, jamii zote mbili, lazima tuwe waaminifu kwa wito wetu kwa kadiri ile ile moja.’

Kufuata maelezo ya Ndugu Schroeder, mwenyekiti alitoa salamu kutoka nchi mbalimbali. Sasa wakati ukafika ili wanafunzi wapokee shahada zao. Wanafunzi hao 22 walitoka nchi sita​—Kanada, Finland, Ujeremani, Uingereza, Sweden, na United States. Ingawa hivyo, migawo yao itawapeleka kwenye mabara 11 tofauti​—Belize, Dominika, Ekwedori, El Salvador, Hong Kong, Lesotho, Pakistan, Paraguay, Puerto Rico, Senegal, na Taiwan. Na ni jambo gani walilosema wahitimu hao siku ya kuhitimu kwao? Mmoja wa wanafunzi hao alisoma barua iliyoelekezwa kwa Baraza Linaloongoza na jamaa ya Betheli, iliyosema hivi kwa sehemu: “Sisi tunawaambia nyinyi asante tena kwa kufanya miezi hii mitano iwe ya kukumbukika kuliko mingine yote ya maisha zetu zote.”

Baada ya pumziko, W. L. Van De Wall wa Halmashauri ya Idara ya Utumishi alianza programu ya alasiri kwa kuongoza Funzo la Mnara wa Mlinzi lililofupishwa. Kufuata hilo, wanafunzi wakaonyesha programu fupi, ikiigiza matukio machache ya kupendeza​—na nyakati fulani ya kuchekesha​—yaliyokuwa yamewapata wakitoa ushuhuda katika Jiji la New York. Halafu, wote waliohudhuria, kutia na darasa hilo la 85, wakaona shangwe juu ya programu maalumu yenye kichwa “Kufahamiana Vizuri Zaidi na Wamisionari Wetu Wenye Bidii.” Kupitia slaidi na mirekodio, hadhirina iliweza kuwaona​—na kuwasikia​—wamisionari wa muda mrefu.

Ukiwa umalizio unaofaa, wanafunzi wakaonyesha drama ya Biblia yenye mavazi ya mwigizo, ikikazia uhitaji wa kufanya mapenzi ya Mungu kwa bidii. Baada ya wimbo mmoja wa mwisho, mmoja kwa wote wakaguswa kwa kina kirefu wakati F. W. Franz, msimamizi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi mwenye umri wa miaka 95 alipokuwa akitoa sala ya kufunga yenye hisia nyingi. Kufuata hilo, wote wakaenda “zao kwenye maskani zao, wakiwa na shangwe na wakihisi vyema moyoni.”

Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi, iliyoanzishwa katika 1943, huzoeza na kutuma wamisionari sehemu zote za dunia. Kwa ajili ya madarasa 35 ya kwanza, shule hiyo ilikuwa kwenye Shamba la Ufalme la Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, karibu na South Lansing, New York. Kuanza na darasa la 36, lililoanza Februari 6, 1961, shule hiyo ilihamishwa ikapelekwa kwenye makao makuu ya Sosaiti katika Brooklyn, New York, ambako imeendeshwa mpaka sasa. Hata hivyo, kuanzia darasa la 86 siku ya Oktoba 17, 1988, shule hiyo imehamishwa ikapelekwa Mashamba ya Mnara wa Mlinzi, karibu na Pine Bush, New York.

[Sanduku katika ukurasa wa 21]

Takwimu za Darasa:

Umri wa wastani: 29.1

Miaka ya wastani katika ukweli: 13.4

Miaka ya wastani katika huduma ya wakati wote: 9.1

Hesabu ya ndugu waseja: 2

Hesabu ya waliooana, mume na mkeye: 10

Darasa la 85 Lenye Kuhitimu la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi

[Picha katika ukurasa wa 23]

Katika orodha iliyopo chini, mistari imepewa namba kuanzia mbele hadi nyuma, na majina yameorodheshwa kutoka kushoto hadi kulia katika kila mstari.

(1) Johnston, Y.; Kuismin, S,; Ugarte, Z.; Williams, Z.; Grischkewitz, G. (2) Powers, E.; D’Angelo, L.; Honsberger, J.; Williams, J.; James, J. (3) Kuismin, V.; Grischkewitz, U.; Ugarte, R.; Rogerson, A.; Lantunen, K.; James, D. (4) Rogerson, M.; Johnston, R.; D’Angelo, T.; Honsberger, T.; Powers, T.; Danielson, M.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki