Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 1/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • “Mkate wa Uzima” Upo kwa Watu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Yesu​—“Mkate wa Uzima”
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • “Mkate wa Kweli Kutoka Mbinguni”
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Yesu “Mkate wa Kweli Kutoka Mbinguni”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 1/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ Kwa nini Yesu aliahidi kwamba wale wenye kutia imani katika yeye hawangekufa kabisa,’ hali kwa uhakika wasikilizaji wake wote walikufa?​—Yohana 11:25, 26.

Yesu aliponena juu ya kutokufa, au juu ya kuishi milele, ni wazi kwamba hakumaanisha ya kuwa wasikilizaji wake wa huko nyuma hawangepatwa kamwe na kifo cha kibinadamu. Wazo la msingi ambalo Yesu alikuwa akitokeza lilikuwa kwamba kuwa na imani katika yeye kungeweza kuongoza kwenye uhai wa milele.

Wakati mmoja, Yesu alijiita mwenyewe “mkate wa uhai.” Halafu akaongeza hivi: “Huu ndio mkate ambao huja chini kutoka mbinguni, hivi kwamba yeyote apate kula baadhi ya huo na asife. Mimi ndimi mkate ulio hai uliokuja chini kutoka mbinguni; ikiwa yeyote anakula baadhi ya mkate huu ataishi milele.”​—Yohana 6:48-51, NW.

Kwa kutazama maneno hayo tu, mtu angeweza kukata shauri kwamba Yesu alikuwa akiambia hadhirina yake kwamba wangeweza kuepuka kupatwa na kifo. Hata hivyo, habari zinazozunguka haziungi mkono njia hiyo ya kukata shauri. Yesu alikuwa ndiyo sasa tu ametoka kusema hivi: “Mapenzi yake aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika wote alionipa nisimpoteze hata mmoja, bali nimfufue siku ya mwisho. . . . Kila mtu amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. . . . Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho.” (Yohana 6:39-44) Na baadaye aliongezea hivi: “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.” (Yohana 6:54) Kwa sababu hiyo, ahadi ya Yesu ya ‘kuishi milele’ haingeweza kwa haki kueleweka kuwa inamaanisha kwamba wasikilizaji wake hawangepatwa na kifo kamwe.

Ndivyo ilivyo pia kuhusu ahadi inayojulikana sana ambayo Yesu alimtolea Martha: “Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa.” (Yohana 11:25, 26) Ni wazi kwamba Yesu hakumaanisha kwamba mitume waaminifu, mathalani, hawangekufa kamwe kama ilivyokuwa kwa wanadamu wengine. Katika muda wa mwaka mmoja, wao wangepakwa mafuta kwa roho takatifu na wangepewa tumaini la kutawala wakiwa wafaIme mbinguni. Ili wapokee thawabu hiyo, wao wangelazimika kufa wakiwa wanadamu. (Warumi 8:14-23; 1 Wakorintho 15:36-50) Na angalia kwamba Yesu alikuwa amesema hivi: “Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi.”

Ahadi ya Yesu itatimizwa kuelekea watumishi wa Mungu wenye bidii ya kujitolea yeye ambao wameishi na kufa kabla ya wakati ambapo uhai wa milele unaanza kuandaliwa. Waaminifu hao wamo katika mstari wa kupata ufufuo wa wakati ujao. Kwa kubaki wakiwa waaminifu baada ya wao kuinuliwa, wao hawatapatwa kamwe na “kifo cha pili,” kifo cha milele.​—Ufunuo 20:15; 21:8, NW; Yohana 8:51.

Lakini unabii wa Biblia unaonyesha kwamba sisi leo tuna fursa ya pekee. Tukiwa sasa tunaishi katika umalizio wa mfumo wa mambo, huenda sisi tukaokoka “dhiki kubwa” inayokuja na kupita moja kwa moja tuingie ndani ya ulimwengu mpya. Hao walio na tumaini la kupata uhai wa milele katika dunia-paradiso na wanaodumisha ushikamanifu wao kwa Mungu hawatalazimika kupatwa hata kidogo na kifo cha kibinadamu. Wakiokoka “dhiki kubwa,” wao wataongozwa “kwenye chemchemi za maji yenye uhai.”​—Ufunuo 7:9-17.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Maneno ya Yesu kwa Martha mwenye kihoro yanaweza kutupa sisi tumaini la uhai wa milele

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki