Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 5/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Tito Anashughulika na Mgawo Mgumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kitabu cha Biblia Namba 56—Tito
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kwa Sababu Gani Uwe Mnyofu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Tito—“Mfanyakazi Mwenzi kwa Ajili ya Masilahi Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 5/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Je! mtume Paulo alikuwa akionyesha maoni ya kuhukumu mapema kwa ukabila alipokubaliana na uchambuzi wa lawama la ujumla kuhusu Wakrete?

Sivyo, Paulo hakujiacha ashindwe na zoea la misemo ya kuwashutumu kwa ujumla watu wenye malezi ya kabila au taifa jingine.

Swali hili linatokana na maelezo yaliyo katika barua ya Paulo kwa mwanafunzi Tito. Paulo alikuwa amemwacha katika kisiwa kile kikubwa cha Krete katika Mediterania ili ‘ayatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji.’ Paulo alipangilia sifa fulani kwa wazee wa kundi lakini akampa Tito ushauri huu: “Kwa maana kuna wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, wadanganyaji, na hasa wale wa tohara, ambao yapasa wazibwe vinywa vyao. Hao wanapindua watu wa nyumba nzima.”​—Tito 1:5,10, 11.

Paulo aliendelea hivi katika Tito 1 mstari wa 12: “Mtu wa kwao, nabii wao wenyewe, amesema, Wakrete ni waongo sikuzote, hayawani wabaya, walafi wavivu.” Katika Tito 1 mstari wa 13, aliongezea hivi: “Ushuhuda huo ni kweli. Kwa sababu hiyo uwakemee [uwakaripie, NW] kwa ukali, ili wapate kuwa wazima katika imani.”

Watafsiri wengi wa Biblia wanaacha elezo la Paulo la kwamba “ushuhuda huo ni kweli” liendelee mara baada ya maneno aliyotaja kutokana na mnabii mmoja Mkrete. Wengine wanaanza fungu jipya kwa mstari wa 13.a Vyovyote vile, Paulo alikuwa akikubaliana kiasi fulani na jambo gani?

Kwa uhakika hakuwa akikubaliana na msemo wowote wenye ubaguzi wa rangi au wenye ukabila kwa kuwahusisha ndani Wakrete wote kwa ujumla. Tunaweza kuwa na uhakika wa jambo hilo, kwa maana Paulo alijua kwamba katika Krete walikuwako Wakristo wazuri sana ambao Mungu alikuwa amewakubali na kuwapaka mafuta kwa roho takatifu Yake. (Matendo 2:5, 11, 33) Walikuwako Wakristo wenye ujitoaji ambao walitosha kufanyiza makundi katika “kila mji” [jiji baada ya jiji, NW]. Ingawa Wakristo hao hawakuwa wanadamu wakamilifu, tunaweza kuwa na uhakika kwamba hawakuwa waongo na walafi wavivu; au sivyo wasingaliendelea kuwa na kibali cha Yehova. (Wafilipi 3:18,19; Ufunuo 21:8) Na kama vile sisi leo tunavyopata katika mataifa yote, inaelekea kwamba katika Krete walikuwako watu wenye mioyo ya ufuataji haki waliohuzunishwa na viwango vya chini vya kiadili ambavyo viliwazunguka na wakawa tayari kuuitikia ujumbe wa Kikristo.​— Ezekieli 9:4; linganisha Matendo 13:48.

Kwa upande ule mwingine, katika Krete walikuwako pia watu ambao hawakuwa na viwango vya juu vya kiadili. Paulo aliona ilifaa kutaja maneno ambayo inaonekana yalitokana na Epimenide, mshairi Mkrete (mnabii au mnenaji) katika karne ya sita K.W.K. Lakini Paulo alikuwa akikubaliana na uelezaji huo kama ulivyotumiwa kuhusu kisehemu fulani hasa cha Wakrete.

Hawa ndio waliokuwa ‘wenye maneno yasiyo na maana na wadanganyaji’ ambao walionana na Wakristo waaminifu na wakawa wakijaribu ‘kupindua watu wa nyumba nzima. Wadanganyaji hao wenye upinduzi walifaa kikweli kuhusishwa kwenye uelezaji wa kuwa ‘waongo, hayawani wabaya, jambo ambalo lilikuwa kweli jinsi ile ile kuhusu watu wa jinsi hiyo mahali penginepo. (2 Timotheo 3:6, 13) Zaidi ya hilo, mtu yeyote katika makundi ambaye tayari alidanganywa kufuata njia hizo alihitaji ‘kukaripiwa kwa ukali.’ Wale wenye kunufaika na karipio wangeweza kusaidiwa hivyo wawe kielelezo kuhusu kazi zilizo nzuri sana na “maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa.”​—Tito 2:6-8.

Katika jambo hili inatupasa tuone tahadhari kwa sisi sote. Huenda maoni ya ukabila au utaifa ya kuhukumu watu mapema yakawa tele kutuzunguka. (Linganisha Yohana 7:47-52.) Inaelekea kwamba sisi huwasikia majirani, wanashule wenzetu, au wafanya kazi wenzetu wakisema maneno ya lawama la ujumla kuhusu watu wengine, kama vile, ‘Wapi, jamaa hao wote wa kutoka kule juu ni baridi-baridi na wasiojali hisia za wengine’; ‘Wewe wajua tu jinsi jamaa hao wa kutoka kule chini walivyo na kiburi’; au, ‘Ni hatari kuamini watu wa ng’ambo hiyo.’

Ni lazima tujitahidi kuepuka kujiacha tushindwe na uelezaji wa vitabia vya watu ambao labda hauna msingi au umetiwa chumvi sana. Huenda watu fulani wakawa wenye urafiki zaidi na wenye kueleza sana maoni yao, wengine wakawa wasiojihusisha sana katika mambo au wenye upolepole wa kuchangamsha watu wasiowajua. Hata hivyo, inatupasa tukumbuke kwamba bila shaka baadhi ya ndugu zetu Wakristo wanapatikana miongoni mwa watu wa kabila au taifa hilo, na pia wengine wengi ambao hawajawa Wakristo wa kweli lakini walio na vitabia vya kuvutia na ambao wana njaa ya kutaka uadilifu.

Mtume Petro alikazia uhakika wa kwamba “Mungu hana upendeleo; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki [uadilifu, NW] hukubaliwa na yeye.” (Matendo 10:34,35) Tunaweza kuwa na uhakika kabisa kabisa kwamba Paulo alikubaliana na jambo hilo, akionyesha maoni ayo hayo katika miandiko na uneni wake. Sisi pia tunapaswa kufanya hivyo.

[Maelezo ya Chini]

a Ona The New Berkeley Version na pia tafsiri zilizofanywa na R. F. Weymouth, F. A. Spencer, K. S. Wuest, na Abner Kneeland.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki