Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 2/1 kur. 20-25
  • Kufichua “Mtu wa Kuasi [Sheria]”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufichua “Mtu wa Kuasi [Sheria]”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Wenye Wajibu wa Kupenda Wengine
  • Kufichua Yule Mtu wa Kuasi Sheria
  • Kwa Nini Ni Wenye Uthabiti Sana?
  • Hukumu ya Mungu Dhidi ya “Mtu wa Kuasi [Sheria]”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kifo cha Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kutambulisha “Mtu wa Kuasi [Sheria]”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kristo Aliuchukia Ukosefu wa Kufuata Sheria —Je! Wewe Wauchukia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 2/1 kur. 20-25

Kufichua “Mtu wa Kuasi [Sheria]”

“Ondokeni katika yeye, watu wangu, ikiwa nyinyi hamtaki kushiriki pamoja na yeye katika madhambi yake, na . . . kupokea sehemu ya tauni zake.”​—UFUNUO 18:4, NW.

1, 2. (a) Mtu wa kuasi sheria aweza kutambulishwaje? (b) Maoni ya Mungu ni nini kuhusu wale ambao wadai kumtumikia lakini ambao ni wenye hatia ya damu? (Mathayo 7:21-23)

NENO la Mungu lilitabiri kuja kwa “mtu wa kuasi [sheria].” Pia lilitabiri kwamba kiasili hiki cha uasi sheria ‘kingeondolewa mbali na kufanywa si kitu’ na Mfishaji wa kimbingu wa Mungu, Kristo Yesu. (2 Wathesalonike 2:3-8, NW) Kama vile makala zilizotangulia zimeonyesha, mtu huyo wa kuasi sheria ni makasisi wa Jumuiya ya Wakristo. Zamani za kale wao waliacha kweli za Neno la Mungu wakachagua kufuata mafundisho ya kipagani, kama vile Utatu, moto wa helo, na kutokufa kwa nafsi. Kwa kuongezea, walitokeza kazi zilizo kinyume cha sheria za Mungu. Kama wale ambao Paulo alionya Tito dhidi yao, “wanakiri [peupe, NW] ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala kwa kila tendo jema hawafai.”​—Tito 1:16.

2 Yesu alisema: “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. Mtawatambua kwa matunda yao.” Manabii bandia wangetokeza “matunda mabaya.” (Mathayo 7:15-17) Ushuhuda kuhusu uzaaji wa matunda mabaya wa makasisi ni hatia yao kubwa sana ya damu. Kwa karne kadhaa wameunga mkono krusedi, mabaraza ya kutesa wazushi, na vita ambavyo vimemwaga damu ya mamilioni. Wametoa sala kuombea na kubariki pande zote mbili katika vita ambamo washiriki wa dini zao wenyewe wameuana. Tofauti na hivyo, mtume Paulo aliweza kutaarifu hivi: “Mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote.” (Matendo 20:26) Makasisi hawakosi hatia. Mungu awajulisha wazi hivi watu wa jinsi hiyo: “Mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.”​—Isaya 1:15.

3. Ni matukio gani yenye kuhusu dunia yote yanayokaribia kasi?

3 Wakati wa Mungu kufikiliza hukumu yake dhidi ya yule mtu wa kuasi sheria unakaribia kasi. Karibuni, kama Yesu alivyotabiri, “kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.” (Mathayo 24:21) Wakati huo wa matata yasiyopata kuwa na kifani utaanza na kuuawa kwa Babuloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini bandia, ambayo yahusisha ndani dini za Jumuiya ya Wakristo. Viasili vya kisiasa ‘vitamfanya kuwa mkiwa na uchi, vitamla nyama yake, vitamteketeza kabisa kwa moto.’ (Ufunuo 17:16) Dhiki kubwa itaisha na uharibifu wa sehemu iliyobaki ya ulimwengu wa Shetani kwenye Har–​Magedoni, “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.”​—Ufunuo 16:14, 16; 19:11-21.

Ni Wenye Wajibu wa Kupenda Wengine

4. Ni lazima wale wenye kuabudu Mungu “katika roho na kweli” wakumbuke nini?

4 Kwa kuwa matukio haya yenye kutikisa ulimwengu yatakuja karibuni juu ya dunia hii yenye kukaliwa, ni wajibu gani mbalimbali ulio juu ya wale ambao ‘huabudu Baba katika roho na kweli’? (Yohana 4:23) Mmoja ni kwamba, ni lazima wakumbuke kwamba Yesu alisema: “Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. . . . Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.”​—Yohana 15:10-14; 1 Yohana 5:3.

5, 6. (a) Yesu aliamuru wanafunzi wake wafanye jambo gani ambalo lingewatambulisha wao? (b) Hii ilikuwa amri mpya katika maana gani?

5 Hivyo Wakristo wa kweli wapewa wajibu wa kupenda watu wale wengine, hasa ndugu na dada zao Wakristo katika mabara yote. (Matendo 10:34; Wagalatia 6:10; 1 Yohana 4:20, 21) Kwa kweli, ni lazima Wakristo wenzi wawe na “juhudi nyingi katika kupendana.” (1 Petro 4:8) Upendo wa aina hiyo kwa kadiri ya duniani pote huwatambulisha kuwa waabudu wa kweli, kwa maana Yesu alisema hivi: “Nawapeni amri mpya: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi. Mkipendana, watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu.”​—Yohana 13:34, 35, HNWW.

6 Ni nini kilichokuwa kipya kuhusu amri hiyo? Je! kwani Wayahudi chini ya Sheria ya Musa hawakupewa amri ya kwamba, “Umpende jirani yako kama nafsi yako”? (Walawi 19:18) Ndiyo, lakini Yesu alionyesha jambo fulani la ziada aliposema, “Kama nilivyowapenda ninyi.” Upendo wake ulihusisha ndani kutoa uhai wake kwa ajili ya wengine, na ni lazima wanafunzi wake wawe na nia ya kufanya ivyo hivyo. (Yohana 15:13) Hicho kilikuwa kiwango cha juu zaidi cha upendo, kwa kuwa Sheria ya Musa haikutaka kujidhabihu kwa kadiri hiyo.

7. Ni dini ipi imetii ile sheria ya upendo katika karne hii?

7 Katika karne yetu, ni dini ipi imetii sheria hii ya upendo? Hakika si dini za Jumuiya ya Wakristo, kwa maana zimechinjana mtu na mwenzake kwa makumi ya mamilioni katika vita viwili vya ulimwengu na mahitilafiano mengine. Mashahidi wa Yehova ndio wametii ile sheria ya upendo duniani pote. Wao wamefuatilia kabisa kudumisha hali ya kutokuwamo katika vile vita vya mataifa, kwa maana Yesu alisema kwamba ni lazima wafuasi wake wawe “si sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:16, NW) Hivyo, wao waweza kusema, kama alivyosema Paulo, kwamba ‘hawana hatia kwa damu ya mtu awaye yote.’ Kwa kielelezo, angalia sehemu ya ufunguzi wa azimio moja lililopitishwa na watumishi wa Yehova kwenye mkusanyiko wa Washington, D.C., siku ya Novemba 27, 1921:

“Sisi Wakristo wanaojitahidi sana kufuata mafundisho ya Kristo Yesu Bwana wetu na Mitume wake, twashikilia hivi: kwamba vita ni salio la tabia ya kishenzi, yenye kuharibu maadili mema na ni suto kwa jamii za watu walio Wakristo; kwamba kanuni zilizofundishwa na Bwana Yesu Kristo zafanya isiwezekane Wakristo waliotengwa kwa makusudi matakatifu wajitie kwa namna yoyote katika vita, umwagaji damu au jeuri.”

8. Kumbukumbu la kihistoria lasema nini kuhusu Mashahidi wa Yehova wakati wa Vita ya Ulimwengu 2?

8 Maoni hayo yalitumiwaje wakati wa Vita ya Ulimwengu 2? Katika vita hiyo iliyo mbaya zaidi katika historia yote ya kibinadamu, watu kama 50 milioni waliuawa. Lakini hakuna hata mmoja aliyeuawa na mmoja wa Mashahidi wa Yehova! Kwa kielelezo, karibu makasisi wote wa Ujeremani waliunga mkono Unazi kwa utendaji wenye bidii au kwa kuachilia mambo tu. Tofauti na hivyo, Mashahidi wa Yehova chini ya utawala wa Kinazi walifuatilia kabisa hali ya kutokuwamo na wakakataa kusema mwokozi ni Hitler au kuwa sehemu ya harakati yake ya kijeshi. Kwa sababu hiyo, wao hawakuua yeyote wa ndugu zao za kiroho wa nchi nyinginezo, wala mtu awaye yote. Na Mashahidi wa Yehova katika mabara mengine yote walibaki pia katika hali ya kutokuwamo.

9. Ni jambo gani lililopata Mashahidi wa Yehova katika Ujeremani na Austria chini ya utawala wa Kinazi?

9 Wengi wa Mashahidi wa Yehova wamekubali kutoa nafsi yao kwa ajili ya rafiki zao kwa kutii ile sheria ya upendo. Pitio la kitabu Kirchenkampf in Deutschland (Pigano la Makanisa Katika Ujeremani), kilichotungwa na Friedrich Zipfel, lasema hivi kuhusu Mashahidi: “Asilimia tisini na saba [97] ya washiriki wa kikundi kidogo hiki cha kidini walikuwa majeruhi wa mnyanyaso wa [Nazi] ya Usoshalisti wa Kitaifa. Theluthi moja kati yao walikufa, ama kwa kuuawa, kwa vitendo vingine vyenye jeuri, njaa, ugonjwa au kazi-jasho ya kiutumwa. Ukali wa utiisho huu haukuwa na kifani na ulitokana na imani isiyoridhiana msimamo ambayo haikuweza kupatanishwa na mawazo ya Usoshalisti wa Kitaifa.” Katika Austria, asilimia 25 ya Mashahidi wa Yehova waliuawa, wakapigwa mpaka kufa, au wakafa kwa maradhi au kunyong’onyea katika kambi za Nazi.

10. Wale waliokufa kwa kutii ile sheria ya upendo walikuwa na uhakika gani?

10 Wale waliouliwa imani kwa kutii ile sheria ya upendo walikuwa na uhakika kwamba “Mungu si dhalimu hata aisahau kazi [yao], na pendo lile [wa]lilodhihirisha kwa jina lake.” (Waebrania 6:10) Walijua kwamba “ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, bali yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anabaki milele.” (1 Yohana 2:17, AW) Walikuwa na tumaini hakika la kufufuliwa kwa tazamio la uhai wa milele.​—Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15.

11. Ni kwa njia gani watumishi wa Yehova hawana kifani, na ni unabii gani unaotimizwa katika wao?

11 Watumishi wa Yehova hawana kifani katika kutii ile kanuni iliyonenwa na Petro na mitume wengine kwa mahakama moja kuu: “Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.” (Matendo 5:29, NW) Kwa sababu Mashahidi wa Yehova hufanya hivyo, wao hutegemezwa na “roho takatifu, ambayo Mungu amewapa wale wanaotii yeye kuwa mtawala.” (Matendo 5:32, NW) Hiyo ndiyo nguvu ambayo huwawezesha watimize unabii ulio kwenye Isaya 2:2-4, NW. Huo ulitabiri kwamba katika wakati wetu ibada ya kweli ingeanzishwa upya ikiwa imara na kwamba watu kutoka mataifa na dini zote wangetiririka kuiendea. Tokeo moja lingekuwa hili: “Watalazimika kufua panga zao ziwe plau za kulimia na mikuki yao iwe makasi ya kupogolea. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.” Kwa sababu watumishi wa Yehova wanajitayarisha kwa ajili ya uhai katika ulimwengu mpya wenye amani, wao hawataki kujifunza vita tena. Wao hujifunza ile sheria ya upendo.​—Yohana 13:34, 35.

12. Ni lazima wale wanaotii ile sheria ya upendo wafanyie wengine nini?

12 Kwa kuwa upendo wa Kikristo watia ndani ‘kupenda jirani yako kama nafsi yako,’ watumishi wa Mungu hawawezi kuwa wabinafsi kuhusu mambo wajuayo. (Mathayo 22:39) Kungali kuna wengine wengi ambao wangetaka kutumikia Mungu na kuishi katika ulimwengu wake mpya. Maadamu kuna wakati, hawa pia wahitaji kujifunza juu ya ile sheria ya upendo na kweli nyingine nyingi ambazo zahusiana na Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote Mzima, Yehova Mungu. Ni lazima wafundishwe kwamba Yehova peke yake ndiye astahiki ibada yetu na ni jinsi gani ibada hiyo yapasa kutolewa. (Mathayo 4:10; Ufunuo 4:11) Wale ambao tayari wamejifunza mambo haya wako chini ya wajibu wa kuambia wengine kuyahusu ili wao pia wapate kuingia katika upendeleo wa Yehova,​—Ezekieli 33:7-9, 14-16.

Kufichua Yule Mtu wa Kuasi Sheria

13. Ni lazima sisi tujulishe nini likiwa sehemu ya ushahidi wetu wa ulimwenguni pote, na kwa nini?

13 Yesu alisema kwamba “habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia nzima yote inayokaliwa kwa ajili ya ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 24:14, NW) Wakiwa sehemu ya ushahidi huu wa ulimwenguni pote, watumishi wa Mungu wako chini ya wajibu wa kujulisha hukumu yake dhidi ya dini bandia, hasa makasisi wa Jumuiya ya Wakristo. Hawa ndio wenye kulaumika zaidi machoni pa Mungu kwa sababu wao wadai ni Wakristo. Ni lazima wafichuliwe ili wale watakao kutumikia Mungu waweze kuwa huru bila uvutano wao na waweze kuchukua hatua zifaazo ili waokoke. Kama alivyosema Yesu: “Hiyo kweli itawaweka huru.”​—Yohana 8:32.

14. Ni ujumbe gani wa wazi ambao ni lazima upigiwe mbiu kuhusu dini bandia?

14 Hivyo, ni lazima Mashahidi wa Yehova wajulishe ujumbe huu uliovuviwa kuhusu dini bandia: “Ondokeni katika yeye, watu wangu, ikiwa nyinyi hamtaki kushiriki pamoja na yeye katika madhambi yake, na ikiwa nyinyi hamtaki kupokea sehemu ya tauni zake. Kwa maana madhambi yake yametungamana pamoja moja kwa moja hadi kwenye mbingu, na Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki. . . . Katika siku moja tauni zake zitakuja, kifo na ombolezo na njaa kuu, na yeye atachomwa kabisa kwa moto, kwa sababu Yehova Mungu, ambaye alihukumu yeye, ni imara.”​—Ufunuo 18:4-8, NW.

15. Mwaka 1914 ulihusikaje katika jedwali-wakati ya Yehova, na ni nini kilichotokea baada ya Vita ya Ulimwengu 1?

15 Unabii wa Biblia waonyesha kwamba “siku za mwisho” kwa mfumo huu wa mambo zilianza katika ule mwaka 1914 wenye badiliko kubwa. (2 Timotheo 3:1-5, 13; Mathayo 24:3-13) Tangu mwaka huo tumekuwa katika “wakati wa mwisho.” (Danieli 12:4) Mara tu baada ya Vita ya Ulimwengu 1, kwa kupatana na orodha-wakati ya Yehova, watumishi wake walianza kupanua tangazo la Ufalme wa Mungu kwa jitihada nyingi kama ilivyotabiriwa kwenye Mathayo 24:14. Pia walianza kufichua dini bandia kwa imara zaidi, hususa jamii ya makasisi waasi sheria wa Jumuiya ya Wakristo yenye uasi-imani.

16. Kufichua mtu wa kuasi sheria kumeongezekaje kani kwa miaka zaidi ya 70?

16 Kwa miaka zaidi ya 70 sasa, watumishi wa Mungu wakiwa na kani nyingi zaidi wamewafanya watu chonjo waone utendaji mdanganyifu wa yule mtu wa kuasi sheria. Kulikuwako Mashahidi elfu chache tu wenye kufanya hivyo baada ya Vita ya Ulimwengu 1. Lakini sasa wamekuwa “taifa hodari” la wahudumu watendaji zaidi ya milioni tatu na nusu waliopangwa kitengenezo wakawa makundi zaidi ya 60,000 duniani kote. (Isaya 60:22) Kwa kadiri yenye kupanuka, kwa bidii watumishi wa Mungu wanapiga mbiu ya Ufalme wa Mungu kuwa ndilo tumaini pekee kwa aina ya binadamu na, wakati ule ule, wanawafichua makasisi kama walivyo hasa​—mtu mdanganyifu wa kuasi sheria.

Kwa Nini Ni Wenye Uthabiti Sana?

17. Kwa nini watumishi wa Yehova wamemfichua kwa uthabiti mtu wa kuasi sheria?

17 Kwa nini muda wa miaka yote hii watumishi wa Yehova wamemfichua kwa uthabiti mtu wa kuasi sheria? Kwa sababu mamilioni ya umati mkubwa wa kondoo za Yehova ambao tayari wako njiani kwenda kwenye wokovu ni lazima walindwe kutokana na ulimwengu wa Shetani na dini yao bandia. (Yohana 10:16; Ufunuo 7:9-14, NW) Zaidi ya hilo, makasisi wasipofichuliwa, watu wenye mioyo ya kufuata haki ambao hawajawa bado sehemu ya kundi la kondoo za Mungu hawangejua jinsi ya kuepuka mwendo usiofaa. Kwa hiyo ni lazima wapashwe habari, sawa na vile Yesu alivyowapasha watu habari aliposema hivi kuhusu viongozi wa kidini walio wanafiki katika siku yake: “Hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.”​—Mathayo 15:14; ona pia 2 Wakorintho 4:4; 11:13-15.

18. Watafutaji wa ukweli wahitaji kujua nini?

18 Makasisi ni sehemu ya ulimwengu wa Shetani. (Yohana 8:44) Lakini huo ni ulimwengu ambao karibuni Mungu ataubomoa upotelee mbali. (2 Petro 3:11-13; 1 Yohana 2:15-17) Kwa hiyo Neno la Mungu laonya hivi: “Yeyote anayetaka kuwa rafiki wa ulimwengu anajifanya adui wa Mungu.” (Yakobo 4:4, HNWW) Makasisi wapuuza onyo hilo na kuendelea kujiingiza-ingiza katika mambo ya kisiasa. Wao huambia wafuasi wao kwamba ulimwengu bora utakuja kupitia jitihada za wanasiasa. Lakini hilo ni tumaini bandia, kwa kuwa ulimwengu huu ulio chini ya Shetani waenda kutokomea. Kwa hiyo watu ambao hutegemea ulimwengu huu kwa tumaini wanadanganywa. Wao wahitaji kuambiwa ukweli kuhusu mahali ambako ulimwengu unaelekea na ni kitu gani kitachukua mahali pao.​—Mithali 14:12; 19:21; Mathayo 6:9, 10; Ufunuo 21:4, 5.

19. Uulimwengu wa makasisi fulani umefichuliwaje katika vyombo vya habari hivi majuzi?

19 Uulimwengu wa makasisi fulani hata umefichuliwa katika vyombo vya habari hivi majuzi, kwa kielelezo ile mitindo ya maisha ya uasherati na anasa ya makasisi fulani wa televisheni. Mwandikaji mmoja wa ki-siku-hizi alitunga wimbo wenye kichwa: “Je! Yesu Angevaa Rolex [saa] ya [dola 10,000] Katika Maonyesho Yake ya Televisheni?” Wimbo huo waendelea kusema: “Je! Yesu angekuwa mtu wa kisiasa kama Yeye angerudi duniani, awe na nyumba Yake ya pili katika [eneo la anasa la] Palm Springs na kujaribu kuficha ustahiki Wake?” Zaidi ya hilo, makasisi wengi zaidi na zaidi huachilia au huzoea ugoni-jinsia-moja. Hata sasa Kanisa Katoliki katika United States linalipa dola milioni nyingi kwa hasara zilizofanywa na mapadri wenye hatia ya kutumia watoto vibaya katika ngono.​—Warumi 1:24-27; 1 Wakorintho 6:9, 10.

20. Kwa nini ni lazima watumishi wa Mungu waendelee kufichua yule mtu wa kuasi sheria?

20 Utendaji makosa huo hauwezi kupuuzwa na watumishi wa Mungu bali ni lazima ufichuliwe kwa manufaa ya wengine. Umati mkubwa wa kondoo wengine ni lazima ulindwe kutokana na wale ambao wangejaribu kuwaongoza wavunje sheria za Mungu. Na wale “wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika” wahitaji kutafutwa-tafutwa na kukusanywa kwenye mwongozo wa ulinzi wa yule Mchungaji Mkubwa, Yehova Mungu, na “mchungaji mwema,” Kristo Yesu.​—Ezekieli 9:4; Yohana 10:11; Mithali 18:10.

21. Mashahidi wa Yehova wataendelea kujulisha nini wazi?

21 Kwa hiyo, watu wa Mungu hawatasitasita kujulisha wazi kisasi chake dhidi ya ulimwengu wote wa Shetani, kutia ndani humo na yule mtu wao wa kuasi sheria, wale makasisi wa Jumuiya ya Wakristo. Kwa jitihada nyingi wao watapiga mbiu ya ujumbe wa kimalaika ulio katika Ufunuo 14:7, NW: “Hofuni Mungu na kumpa yeye utukufu, kwa sababu saa ya hukumu kwa yeye imewasili.” Na katika mbiu hii watahusisha lile onyo la kufanya hima lililo katika Ufunuo 18:4, NW, kuhusu dini bandia: “Ondokeni katika yeye, watu wangu, ikiwa nyinyi hamtaki kushiriki pamoja na yeye katika madhambi yake, na . . . kupokea sehemu ya tauni zake.”

Maswali kwa Kupitia:

◻ Msiba wa mtu wa kuasi sheria utakuwa nini, na kwa nini?

◻ Watumishi wa Yehova wana wajibu gani kuhusu wengine?

◻ Watu wa Yehova wameendeleaje kuwa uhuru bila damu ya wanadamu wote?

◻ Ni lazima tufanye nini kuhusu Babuloni Mkubwa?

◻ Kwa nini sisi tutaendelea na ujumbe wetu thabiti kuhusu yule mtu wa kuasi sheria?

[Picha katika ukurasa wa 23]

Mitume waliambia mahakama moja kuu: “Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu”

[Picha katika ukurasa wa 24]

Watu wenye mioyo myeupe wahitaji kujua ulimwengu na dini zao unaelekea wapi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki