Wazia Ulimwengu Usio na Pupa
JE! WEWE waweza kuona njozi ya ulimwengu ambamo watu washirikiana badala ya kushindana? Ambamo wanadamu watendea wengine vile wao wenyewe wangependa watendewe? Hizi ndizo tabia za ulimwengu usio na pupa. Utakuwa ulimwengu wee! Je! utapata kuja? Ndiyo. Lakini pupa—ambayo imeimarika sana katika ainabinadamu—yaweza kukomeshwaje?
Kupata jibu, ni lazima kwanza tuelewe asili ya pupa. Biblia yaonyesha kwamba hiyo haikuwa tabia ya jamii ya kibinadamu sikuzote. Nabii Musa atukumbusha kwamba hapo kwanza kasoro kama ya pupa haikuwa katika mwanadamu wa kwanza, ule uumbaji mkamilifu wa Muumba asiye na pupa: “Mwamba, ni mkamilifu utendaji wake, kwa maana njia zake zote ni za haki.” Basi, pupa ilitoka wapi? Wanadamu wa kwanza wawili waliiruhusu isitawi ndani yao wenyewe—Hawa akawa nayo kwa kutazamia kupata kitu fulani kwa kula tunda ambalo Mungu alikuwa amekataza na Adamu akawa nayo kwa kuwa na pupa «a kutotaka kupoteza mke wake mzuri. Kwa kutumia maneno ambayo yalikuwa ya kweli Dja kuhusu Adamu na Hawa, Musa aliongeza hivi: “Wametenda kwa uangamivu upande wao; wao si watoto wake, kasoro ni yao wenyewe.”—Kumbukumbu 32:4, 5; 1 Timotheo 2:14, NW.
Kufikia wakati wa Gharika ya tufe lote ya siku ya Noa, pupa na uchu vilikuwa vimesitawi kwa hali ya kwamba “ubaya wa mwanadamu ulikuwa mwingi sana katika dunia na kila mbetuko wa mawazo ya moyo wake yalikuwa mabaya tu wakati wote.”—Mwanzo 6:5, NW.
Mtazamo huu wa pupa wenye kutawala katika mwanadamu umeendelea mpaka sasa, yaonekana ukafikia kileleta katika jamii ya leo isiyo na shukrani na yenye pupa.
Kuiondolea Mbali Pupa Kupitia Elimu
Kama vile pupa imeongezeka miongoni mwa wanadamu, ndivyo kinyume chawezekana. Pupa yaweza kushindwa. Hata hivyo, ili iwe hivyo, yahitajiwa kuwe na elimu na mazoezi yafaayo, pamoja na miongozo au kawaida za mwenendo zenye kufuatiliwa sana. Huenda hilo likasikika kuwa lafaa, lakini nani angeweza kutoa elimu ya aina hiyo na kuhakikisha kwamba masomo hayo yazoewa kimatendo—hata yatekelezwe ikihitajiwa hivyo?
Ni lazima elimu hiyo itokane na chanzo kisicho na pupa yenyewe. Ni lazima kusiwe na makusudio yoyote ya kichinichini wala tarajio la kupata kitu kutokana na mazoezi hayo. Kwa kuongezea, ni lazima thamani na mafaa ya kutokuwa na ubinafsi yafunzwe na kujulishwa kwa vionyeshi. Mwenye kujifunza ahitaji kusadikishwa si kwamba tu njia hiyo ya maisha yawezekana bali kwamba ndiyo njia yenye kupendelewa zaidi, yenye manufaa kwake mwenyewe na kwa wale walio karibu yake.
Mungu wa mbinguni ndiye pekee awezaye kutoa elimu ya aina hii, kwa maana ni mwanadamu au tengenezo gani duniani lingekuwa na sifa na mandhari-nyuma hiyo? Wanadamu wote hawana sifa za ustahili kwa msingi wa ukweli huu wa Kibiblia: “Wote wamefanya dhambi na hupungukiwa na utukufu wa Mungu.”—Warumi 3:23, NW.
Kwa kufurahisha, Yehova, Mungu wa mbinguni, huandaa elimu hiyo katika kitabu chake cha mafunzo, au cha masomo, Biblia Takatifu. Mwana Wake, Yesu Kristo, alitetea fundisho la aina hii alipokuwa mwanadamu duniani. Katikati ya Mahubiri ya Mlimani yaliyo maarufu, Yesu alinena juu ya njia ya maisha iliyosikika kuwa ngeni kwa wasikilizaji, kwa maana ilihusisha ndani kutokuwa na ubinafsi hata kuelekea adui au wapinzani wa mtu. Yesu alisema: “Endeleeni kupenda adui zenu na kusali kwa ajili ya wale wanaonyanyasa nyinyi; kwamba nyinyi mpate kujithibitisha wenyewe kuwa wana wa Baba yenu aliye katika mbingu, kwa kuwa yeye hufanya jua lake liwainukie waovu na wema na hufanya inye juu ya waadilifu na wasio waadilifu. Kwa maana ikiwa nyinyi mwapenda wale wanaopenda nyinyi, mna thawabu gani? Je! wakusanya-kodi hawafanyi jambo ilo hilo?”—Mathayo 5:44-46, NW.
Sehemu ya utume wa Yesu duniani ilikuwa kuzoeza wafunzi wasio na ubinafsi ili wao nao waweze kuelimisha wengine njia hii ya maisha isiyo na pupa. Wakati fulani baada ya kufa na kufufuliwa kwa Yesu, mtume Paulo akawa mmoja wa wafunzi hao. Katika hesabu fulani ya barua zake zilizovuviwa, Paulo alihimiza ukomeshaji wa pupa. Mathalani, aliandikia Waefeso hivi: “Acheni uasherati na ukosefu wa usafi wa kila namna au upupa hata usitajwe miongoni mwa nyinyi, sawa na vile hujuzu watu watakatifu.”—Waefeso 5:3, NW.
Vivyo hivyo leo, Mashahidi wa Yehova wanafundisha wanaume na wanawake kukandamiza mielekeo yenye pupa. Watu hawa pia huja kustahili kwenda wakafundisha wengine njia hizo za kumcha Mungu.
Kweli za Biblia Katika Tendo
Lakini huenda ukauliza hivi: ‘Je! watu wasiokamilika, waliokwamwa sana na pupa, waweza kweli kuing’oa katika nyutu zao?’ Ndiyo. Bila shaka hawawezi kufanya hivyo kikamilifu, bali kwa kadiri kubwa ajabu. Acheni tufikirie kielelezo cha jambo hili.
Mwizi mmoja wa kupindukia aliishi katika Hispania. Nyumba yake ilijaa vitu vya kuiba. Ndipo akaanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Tokeo ni kwamba dhamiri yake ilianza kumsumbua, kwa hiyo akaamua kurudishia wenyewe vitu alivyokuwa ameiba. Alimfikia aliyekuwa mwajiri wake wa hapo kwanza akaungama kwamba alikuwa ameiba kutoka kwake mashine ya kufua nguo. Mwajiri huyo, kwa kuvutwa sana na mtazamo wake uliobadilika, aliamua kutowapasha polisi habari na kuruhusu huyo aliyekuwa mwizi hapo zamani alipe tu bei ya mashine ile ya kufua nguo.
Halafu, mwizi huyo aliyeongolewa akawania kuzuru kila mtu mwingine ambaye alikumbuka alikuwa ameiba kutoka kwake arudishe vitu vilivyoibwa. Kila mtu ambaye yeye alizuru alionyesha mshangao kwamba ye alikuwa amefanya badiliko kubwa hili la ipt zamo kwa sababu ya kutumia kanuni za Biblia.
Sasa alikabiliwa na ugumu mkubwa kwe kweli. Hakuwajua wenye vitu vingi ambavy alikuwa angali navyo. Kwa hiyo, baada y kusali kwa Yehova, alienda kwenye mak makuu ya polisi akapeleka redio sita za alizokuwa ameiba katika magari. Polisi walj. shangaa, kwa maana alikuwa na rekodi safi kwao. Wakaamua alipe faini na kufungwa jela muda mfupi tu.
Mwizi huyu wa hapo zamani ana dhamiri safi sasa, akiisha kuacha maisha yake ya uhalifu na pupa ili awe sehemu ya kundi la ulimwenguni pote la Mashahidi wa Yehova.
Maelfu ya vielelezo kama hicho yangeweza kutolewa kwa utayari. Ingawa wale ambao wamefanya mabadiliko hayo katika maisha zao ni wachache tu kati ya wakaaji wa dunia, uhakika wa kwamba wengi wamefanya hivyo waonyesha kwamba kujua na kutumia kanuni za Biblia kuna nguvu za kutokeza mema.
Kila mwaka upitapo, watu zaidi na zaidi hupokea kwa moyo njia hii ya maisha. Mafunzo ya Biblia yanatolewa katika makundi zaidi ya 60,000 ya Mashahidi wa Yehova katika sehemu zote za dunia. Mashahidi hawatazamii kubadili ulimwengu kwa ujumla wakati huu, huku wakikomesha pupa miongoni mwa maelfu ya mamilioni walio hai kwa sasa. Hata hivyo, unabii wa Biblia waonyesha kwamba karibuni sasa njia ya maisha isiyo na pupa itaenea duniani pote!
Ulimwengu Mpya Usio na Pupa
Pupa na ubinafsi havitakuwa na nafasi yoyote katika ulimwengu mpya unaokuja. Mtume Petro atuhakikishia kwamba uadilifu utakuwa si chapa ya “mbingu mpya” tu bali pia ya “dunia mpya.” (2 Petro 3:13, NW) Pupa itakuwa miongoni mwa “mambo ya kwanza” ambayo yatakuwa yamepitilia mbali, pamoja na magonjwa, majonzi, na hata kifo,—Ufunuo 21:4.
Kwa sababu hiyo, ikiwa wewe wasononeshwa na pupa yenye kuongezeka sana na njia ya maisha yenye kuonwa mahali pote kutuzunguka leo, jipe moyo! Anza sasa kuishi kwa ajili ya ulimwengu mpya unaokuja ambao karibuni utakuwa uhalisi. Kwa msaada wa Mungu, jitahidi kukomesha pupa katika maisha yako mwenyewe. Jiunge katika kusaidia wengine waone manufaa ambazo zaweza kuonewa shangwe sasa hivi kwa kuishi Kikristo. Weka imani na tegemeo lako katika ahadi ya Yehova Mungu kwamba muda si muda pupa itakuwa miongoni mwa mambo mengi yasiyofurahisha ambayo ‘hayatakumbukwa, wala hayataingia mioyoni mwetu.’—Isaya 65:17.
[Picha katika ukurasa wa 5]
Yesu alinena juu ya njia ya maisha ambayo huendeleza utovu-binafsi, si pupa
[Picha katika ukurasa wa 7]
Karibuni—ulimwengu usio na pupa