Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 12/15 uku. 30
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Sehemu ya 1—Je! Yesu na Wanafunzi Wake Walifundisha Fundisho la Utatu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je! Kwa Wazi Hilo Ni Fundisho la Biblia?
    Je, Uamini Utatu?
  • Utatu Hufafanuliwaje?
    Je, Uamini Utatu?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 12/15 uku. 30

Je! Wakumbuka?

Je! wewe umetafakari kwa uangalifu juu ya matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, yaelekea utaliona kuwa jambo la kupendeza kukumbuka yafuatayo:

◻ Rekodi ya Biblia ya mapigano ya Yehova inatupaje uhakika katika kukabili “dhiki kubwa”? (Mathayo 24:21)

Akiwa mwenye kudhibiti mambo sikuzote, Yehova ameonyesha kwamba aweza kushinda adui zake katika kuwaza na aweza kugeuza hali kwa ajili ya wokovu wa watu wake.—8/15, ukurasa 27.

◻ Ni lazima wazazi wawe na nia ya kufanya nini ili kudumisha uwasiliano kati yao wenyewe na watoto wao?

Ni lazima wazazi watumie wakati pamoja na watoto wao. Pia, ni lazima wawe na nia ya kuwafanyia watoto wao dhabihu kwa ajili ya ukuzi wao wa kiakili, kimwili, na kiroho.—9/1, ukurasa 22.

◻ Kugeuka umbo kwa Yesu kwamaanisha nini kwetu leo? (Marko 9:2-4)

Kugeuka umbo kwaweza kujenga imani katika neno la kiunabii la Yehova na kuimarisha imani yetu katika Yesu Kristo akiwa Mwana wa Mungu na Mesiya aliyeahidiwa. Kwaweza pia kuimarisha imani yetu katika ufufuo wa Yesu kwenye uhai wa roho na kuongezea imani yetu katika serikali ya Mungu.—9/15, ukurasa 23.

◻ Ni nini maana ya “kwa kitambo fulani” katika Isaya 11:6, NW?

Ufasiri wa uangalifu wa mstari huo waonyesha kwamba jibwa-mwitu na mwana-kondoo mume hawatakuwa pamoja wakati wote katika ulimwengu mpya. Yawezekana kwamba wanyama kama hao bado watakuwa na makao mbalimbali na kupata kuwa chini ya jamii za ‘wanyama wa kufugwa na wanyama wa mwitu’ kama zilivyokuwako katika Paradiso ya asilia. (Mwanzo 1:24) Hata hivyo, wanyama watakuwa na amani kati ya mmoja na mwingine, kuweza kuwa pamoja bila hatari yoyote.—9/15, ukurasa 31.

◻ Ni nini ufunguo wa Ukristo wa kweli?

Upendo ndio ufunguo wa Ukristo wa kweli. Imani, matendo, na ushirika unaofaa ni vya lazima, lakini bila upendo thamani yavyo haitimizwi. Hivyo ndivyo ilivyo kwa sababu Yehova ni Mungu wa upendo hasa, zaidi ya mambo mengine yote. (1 Wakorintho 13:1-3; 1 Yohana 4:8)—10/1, ukurasa 20.

◻ Je! maneno “wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa” kwenye Mhubiri 3:2 yanaunga mkono wazo kwamba Mungu ameamua kimbele wakati wetu wa kufa?

La. Sulemani alikuwa akizungumzia tu hali yenye kuendelea ya maisha na kifo inayoipata ainabinadamu isiyokamilika. Mhubiri 7:17 hutaarifu hivi: “Usiwe mwovu kupita kiasi; wala usiwe mpumbavu; kwani ufe kabla ya wakati wako?” Shauri hilo lingekuwa na umaana gani ikiwa wakati wa kifo cha mtu ungekuwa umeamuliwa kimbele?—10/15, ukurasa 5-6.

◻ Ni nini kinachotoa hoja dhidi ya kuwa kwa mtume Petro askofu wa kwanza wa Roma?

Hakuna uthibitisho wowote kwamba Petro alipata kutembelea jiji la Roma kwa wakati wowote; wala Petro hakujirejezea mwenyewe kamwe kuwa mwenye hali iliyo bora zaidi ya mmoja wa mitume wa Kristo. (2 Petro 1:1)—10/15, ukurasa 8.

◻ Je! inafaa kwa Wakristo kupeleka maua kwenye maziko?

Ikiwa inajulikana sana kwamba desturi fulani (au pambo, kama vile msalaba) ina maana ya kidini wakati huo katika eneo la mtu, yapasa iepukwe. Kwa hiyo Wakristo wasingepeleka maua kwa namna ya msalaba au kuyatumia kwa njia fulani rasmi ambayo kwa wazi ina maana bandia ya kidini. Hata hivyo, katika nchi nyingi wakati huu, desturi ya kuandaa maua bila uhusiano wowote wa kidini imeenea. Wakristo wengine wamepeleka maua kuongeza hali ya uchangamfu kwenye pindi yenye huzuni na kuonyesha huruma na ufikirio.—10/15, ukurasa 31.

◻ Maelezo rasmi huelewesha wazi nini kuhusu Utatu?

Yanaelewesha wazi kwamba fundisho la Utatu si wazo rahisi. Badala ya hivyo, hilo hufanyizwa na mawazo mbalimbali yaliyo magumu kueleweka ambayo yamekusanywa pamoja kupitia muda wa karne kadhaa na kufungamanishwa pamoja. Wanachuo wengi, kutia na Wanautatu, hukiri kwamba Biblia kwa kweli haina fundisho la Utatu.—11/1, Kurasa 21-2.

◻ Ni kwa nini 29 W.K. ni tarehe ya mhimili katika historia ya Biblia?

Kwa sababu kwa kulinganisha habari sahihi ya Kibiblia pamoja na tarehe ya kilimwengu ya utawala wa Tiberio, wanafunzi wa Biblia waweza kuhesabu kwamba huduma ya Yohana ilianza katika masika ya 29 W.K. na kwamba miezi sita baadaye, katika vuli ya 29 W.K., Yohana alimbatiza Yesu.—11/15, ukurasa 31.

◻ “Ibada” ilimaanisha nini kwa watu wenye kusema Kiebrania, na hilo linatumikaje kwa Mashahidi wa Yehova leo?

Neno la Kiebrania lililo sawa na neno “ibada” laweza kutafsiriwa “utumishi.” Kwa hiyo, katika akili ya Mwebrania ibada ilimaanisha utumishi. Hivyo ndivyo inavyomaanisha kwa watu wa Yehova leo, kwa hiyo alama ya maana sana ya ibada ya kweli ni ule utumishi wa kimungu wa kuhubiri.—12/1, ukurasa 19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki