Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 2/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • “Endeleeni Kufanya Hivi Kwa Kunikumbuka Mimi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • “Siku Hii Itakuwa Ukumbusho Kwenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 2/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Mkristo akiwa mgonjwa au anasafiri na hivyo asiweze kuwa kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho, je, anapaswa auadhimishe mwezi mmoja baadaye?

Katika Israeli ya kale Sikukuu ya Kupitwa ilifanywa kila mwaka siku ya 14 ya mwezi wa kwanza, ulioitwa Nisani (au, Abibu). Lakini tunapata uandalizi wa pekee kwenye Hesabu 9:10, 11: “Nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Mtu wa kwenu, au wa vizazi vyenu, ye yote atakayekuwa na unajisi kwa ajili ya maiti, au akiwako mbali katika safari, na haya yote, ataishika Pasaka kwa BWANA [Yehova, NW]; mwezi wa pili [ulioitwa Iyyari, au Zivu], siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, wataishika; watamla pamoja na mikate isiyotiwa chachu na mboga za uchungu.”

Ona kwamba hiyo haikuanzisha tarehe mbili tofauti za Sikukuu ya Kupitwa (Nisani 14 au Zivu 14), kwa Mwisraeli yeyote au watu wa nyumba yoyote kuchagua kwa hiari, kulingana na hali inayofaa zaidi. Uandalizi wa mlo wa Sikukuu ya Kupitwa katika mwezi wa pili ulikuwa na mpaka. Ilikuwa kwa hali ya pekee kwa Mwisraeli aliyekuwa mchafu kisherehe katika Nisani 14 au mbali sana na mahali ambapo mwadhimiso wa kawaida ulifanywa.

Kisa pekee kilichorekodiwa cha uandalizi huo kutumiwa sana kilikuwa wakati Mfalme Hezekia mwaminifu alipoanzisha tena mwadhimisho wa Sikukuu ya Keki Zisizochachishwa. Hakukuwa na wakati wa kutosha wa kujitayarisha kwa ajili ya mwezi wa kwanza (makuhani wakiwa si tayari wala watu wakiwa hawajakusanyika), kwa hiyo ilifanywa katika siku ya 14 ya mwezi wa pili.—2 Mambo ya Nyakati 29:17; 30:1-5.

Isipokuwa kwa sababu ya hali hizo za pekee, Wayahudi waliadhimisha Sikukuu ya Kupitwa katika tarehe ambayo Mungu alikuwa ameweka. (Kutoka 12:17-20, 41, 42; Mambo ya Walawi 23:5) Yesu na wanafunzi wake waliadhimisha jinsi sheria ilivyotaka, bila kuona tarehe hiyo kivivi hivi. Luka aripoti hivi: “Ikafika siku ya mikate isiyotiwa chachu, ambayo ilipasa kuchinja pasaka. [Yesu] akawatuma Petro na Yohana, akisema, Nendeni, mkatuandalie pasaka tupate kuila.”—Luka 22:7, 8.

Katika pindi hiyo Yesu alianzisha mwadhimisho wa kila mwaka ambao Wakristo huujua kuwa Chakula cha Jioni cha Bwana. Thamani ya Wakristo kuhudhuria haiwezi kukaziwa kupita kiasi. Hilo ndilo tukio la maana zaidi katika mwaka wa Mashahidi wa Yehova. Maneno ya Yesu huonyesha sababu ya hilo; alisema hivi: “Fanyeni [fulizeni kufanya, NW] hivi kwa ukumbusho wangu.” (Luka 22:19) Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova wote wapaswa wapange miezi mingi kimbele wasipangie mambo mengine kwenye tarehe hiyo ya mwadhimisho. Chakula cha Jioni cha Bwana kitaadhimishwa Ijumaa Aprili 6, 1993, baada ya jua kushuka kulingana na mahali.

Katika visa vya hali isiyotazamiwa, kama vile ugonjwa au kutatanika kwa safari, yaweza kumzuia Mkristo asihudhurie kama alivyokuwa amepanga. Jambo gani lifanywe katika hali hiyo?

Katika mwadhimisho huo mkate usiotiwa chachu na divai nyekundu hupitishwa, na wale ambao wamepakwa mafuta kwa roho takatifu ya Mungu na ambao wamechaguliwa kwa ajili ya uhai mbinguni hushiriki. (Mathayo 26:26-29; Luka 22:28-30) Ikiwa mwaka huu mmoja ambaye amekuwa akishiriki kila mwaka ni mgonjwa kitandani iwe nyumbani au hospitalini, wazee wa mahali hapo watapanga mmoja wao ampelekee mgonjwa huyo mkate na divai, azungumze maandiko yanayohusu habari hiyo, na kutoa mifano. Ikiwa Mkristo fulani aliye mpakwa-mafuta yu mbali na kundi lake la nyumbani, anapaswa apange kwenda kwenye kundi katika eneo ambamo atakuwamo tarehe hiyo.

Kulingana na hayo, ingekuwa chini ya hali za pekee sana kwamba Mkristo mpakwa-mafuta angelazimika aadhimishe Chakula cha Jioni cha Bwana siku 30 baadaye (mwezi mmoja wa luna), kwa kupatana na amri kwenye Hesabu 9:10, 11 na kile kielelezo kwenye 2 Mambo ya Nyakati 30:1-3, 15

Wale ambao ni “kondoo wengine” wa Yesu, wenye tumaini la uhai wa milele kwenye dunia-paradiso, hawako chini ya ile amri ya kushiriki mkate na divai. (Yohana 10:16) Ni muhimu kuhudhuria mwadhimisho huo wa kila mwaka, lakini hawashiriki mifano. Kwa hiyo ikiwa mmoja wao ni mgonjwa au anasafiri na hivyo hayuko pamoja na kundi lolote jioni hiyo, yeye aweza kusoma kifaragha maandiko yanayohusu (kutia na ule usimulizi wa Yesu akianzisha mwadhimisho huo) na kusali kwa ajili ya baraka ya Yehova juu ya tukio hilo ulimwenguni pote. Lakini katika kisa hiki hakuna uhitaji wa kufanya mpango mwingine zaidi wa kuwa na mkutano au mazungumzo ya Kibiblia ya pekee mwezi ufuatao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki