Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 6/1 uku. 32
  • Sababu kwa Nini Wapaswa Kuhudhuria

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu kwa Nini Wapaswa Kuhudhuria
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Pokea Kufundisha Kimungu kwa Nyakati Zetu Zenye Hatari
    Amkeni!—1993
  • “Hofu ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya Umekaribia
    Amkeni!—1994
  • “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Njooni Kwenye “Imani Katika Neno la Mungu” Mkusanyiko wa Wilaya!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 6/1 uku. 32

Sababu kwa Nini Wapaswa Kuhudhuria

UTAPOKEA siku nne zenye kuthawabisha za maagizo ya kiroho kwenye “Kufundisha Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya, utakaofanywa kiangazi hiki katika majiji kotekote ulimwenguni. Katika United States pekee, mikusanyiko hiyo zaidi ya 150 itafanywa wakati wa Juni, Julai, na Agosti. Kwa kawaida, programu hiyo itaanza Alhamisi saa 7:20 za alasiri na kumalizika Jumapili saa 10:15 za alasiri. Jambo kuu kwenye mikusanyiko mingine litakuwa ripoti za wamishonari, ambao wamesaidiwa kurudi nyumbani kwao kwa ajili ya pindi hiyo yenye furaha.

Iwe wewe ni mzee au ni kijana—mume, mke, baba, mama, tineja, au mtoto—utapokea kufundisha kunakotolewa katika njia ya wazi, yenye kuvutia ambayo itakunufaisha. Kwa kielelezo, wengi leo huuliza, Kusudi la maisha ni nini? Ijumaa asubuhi, utafurahia kusikiza swali hilo likizungumziwa na utapendezwa na yale utakayopokea ili kuwasaidia wengine waelewe habari hiyo.

Ijumaa alasiri programu itakazia sehemu “Kufanya Ndoa Iwe Muungano wa Kudumu,” “Fanya Bidii Kwa Ajili ya Wokovu wa Nyumba Yako” na “Wazazi—Watoto Wenu Wanahitaji Uangalifu wa Pekee.” Mara tu baada ya hizo, uangalifu wa pekee utakazwa juu ya matatizo ambayo vijana hukabili na jinsi wanavyoweza kuyashughulikia. Wanapaswa kutiwa moyo na drama ya kisasa yenye kichwa Vijana Wamkumbukao Muumba Wao Sasa.

Jumamosi programu itakazia unabii wa Yesu kuhusu siku za mwisho na hasa maneno yake: “Mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza.” (Mathayo 24:29) Utataka kusikia mazungumzo kuhusu wakati ambapo dhiki hiyo inapotukia. Programu ya Jumamosi itapitia pia rekodi ya Mashahidi wa Yehova katika nyakati za kisasa na kuonyesha yale ambayo wametimiza.

Jumapili drama nyingine yenye kichwa Usidanganyike Wala Kumdhihaki Mungu, itaonyesha ugumu unaokabili uaminifu-maadili wa Kikristo wa mtu kwa sababu ya vidio na muziki wa leo unaopendwa sana. Hotuba ya watu wote wakati wa alasiri itakazia kichwa kikuu “Kufundisha Kunakosaidia kwa Nyakati Zetu Zenye Hatari.” Programu hiyo itamalizia kwa onyo hili la upole “Endeleeni Kushika Sana Kufundisha Kimungu.”

Kwa hakika, utanufaika kwa kuwapo siku zote nne! Umealikwa kwa uchangamfu kuhudhuria. Ili kujua mahali pa mkusanyiko palipo karibu zaidi na nyumbani kwako, wasiliana na Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova la kwenu au andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki