Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 5/22 uku. 32
  • Pokea Kufundisha Kimungu kwa Nyakati Zetu Zenye Hatari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pokea Kufundisha Kimungu kwa Nyakati Zetu Zenye Hatari
  • Amkeni!—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu kwa Nini Wapaswa Kuhudhuria
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Njoo Usikie Hotuba ya Watu Wote—“Imani na Wakati Ujao Wako”
    Amkeni!—1997
  • “Hofu ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya Umekaribia
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 5/22 uku. 32

Pokea Kufundisha Kimungu kwa Nyakati Zetu Zenye Hatari

Namna Kutakunufaisha

WAWEZA kupokea kufundisha huko kwa kuhudhuria “Kufundisha Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova. Mamilioni watahudhuria mikusanyiko hiyo kiangazi hii katika majiji ya ulimwenguni kote. Katika United States pekee, kutakuwa na mikusanyiko hiyo ya siku nne zaidi ya 150 itakayofanywa wakati wa Juni, Julai, na Agosti.

Uwe mzee-mzee au kijana—mume, mke, baba, mama, tineja, au mtoto—utapokea kufundisha kutakakotolewa kwa njia iliyo wazi, na inayovutia itakayokunufaisha. “Kufanya Ndoa Iwe Muungano wa Kudumu,” “Fanya Bidii Kwa Ajili ya Wokovu wa Nyumba Yako,” na “Wazazi—Watoto Wenu Wanahitaji Uangalifu wa Pekee” ni baadhi tu ya mambo yatakayokuwa katika programu.

Uangalifu wa pekee utakaziwa matatizo ambayo vijana wanapata na jinsi wanavyoweza kukabiliana nayo katika nyakati zetu zenye hatari. Vijana wapaswa watiwe moyo na drama ya kisasa yenye kichwa Vijana Wamkumbukao Muumba Wao Sasa. Drama nyingine iliyotayarishwa vizuri inayoitwa Usidanganyike Wala Kumdhihaki Mungu itazungumzia magumu ambayo vijana Wakristo hukabili kwa sababu ya vidio na muziki unaopendwa na wengi.

Kwa kweli, tunaishi katika nyakati za hatari. Yesu alitabiri kwamba “baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza.” (Mathayo 24:29) Programu ya mkusanyiko itazungumzia uthibitisho kuhusu wakati “dhiki” hiyo inapoanza, pamoja na wakati jua linapotiwa giza.

Katika nyakati hizi za hatari, wengi huuliza, Ni nini kusudi la maisha? Jambo hilo litazungumziwa kikamili, na bila shaka utafurahi kwa yale utakayopokea juu ya habari hiyo. Na bado sehemu nyingine ya programu itapitia rekodi ya Mashahidi wa Yehova katika nyakati za kisasa na kuonyesha mambo ambayo wametimiza.

Katika siku ya mwisho ya mkusanyiko, hotuba ya watu wote itakuwa na kichwa “Kufundisha Kunakosaidia kwa Nyakati Zetu Zenye Hatari.” Programu itamalizia kwa onyo hili la upole “Endeleeni Kushika Sana Kufundisha Kimungu.”

Kwa kweli, utanufaika kwa kuwapo siku zote nne! Unakaribishwa kwa uchangamfu uhudhurie. Ili kupata mahali pa mkusanyiko ulio karibu zaidi na kwako, pata habari zaidi kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova la mahali penu au andikia watangazaji wa gazeti hili au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki