Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 12/15 uku. 30
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Hirizi za Bahati Njema Zaweza Kukulinda?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Kwa Nini Ukubali Kosa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Je! Ulinzi wa Kweli Wawezekana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • ‘Jivikeni Wenyewe Ustahimilivu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 12/15 uku. 30

Je! Wakumbuka?

Je! umethamini kuyasoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Basi, ona ikiwa waweza kuyajibu maswali yafuatayo:

▫ Ni msaada upi wenye kufaa uwezao kutolewa kwa wagonjwa na wazee-wazee ndani ya kutaniko leo?

Katika kutaniko la Kikristo la mapema, orodha iliwekwa ya wajane waliohitaji utegemezo wa kimwili. (1 Timotheo 5:9, 10) Leo vilevile, wazee wa kutaniko waweza kutayarisha orodha ya wagonjwa na wazee-wazee wanaohitaji ufikirio wa pekee. Hata hivyo, si wazee pekee yao wapaswao kuchukua hatua ya kwanza katika jambo hilo. Ni lazima wote katika kutaniko watambue mahitaji hayo. (1 Timotheo 5:4-8)—8/15, kurasa 28-9.

▫ Je! simulizi la Biblia juu ya Yona kumezwa na mnyama wa baharini ni lisiloaminika?

La, ama nyangumi-shahawa, papa-mweupe mkubwa sana, ama papa-nyangumi aweza kummeza mwanadamu. Zaidi ya hayo, Yesu mwenyewe alithibitisha simulizi hilo juu ya Yona kuwa la kweli. (Mathayo 12:39, 40)—8/15, ukurasa 32.

▫ Ni madhara gani yanayotokana na utumizi wa kishirikina wa talasimu na hirizi?

Utumizi wazo kwa kweli huwazuia watu wasikabili matatizo yao kwa kutumia akili na kuwatia moyo watazamie bahati kuwa ndilo suluhisho la mambo yote. Pia hizo humpa mwenye kuzitumia hisi bandia ya usalama. La maana zaidi, mtu atiaye imani katika nguvu za kichawi za talasimu na hirizi za bahati njema huenda akasalimisha udhibiti wa uhai wake kwa kani za kishetani zisizoonekana.—9/1, ukurasa 4.

▫ Ni mambo gani manne yawezayo kufanya ndoa idumu?

Hayo ni nia ya kusikiliza, uwezo wa kuomba msamaha, kuweza kuandaa utegemezo wa daima wa kihisiamoyo, na tamaa ya kugusana kwa shauku. (1 Wakorintho 13:4-8; Waefeso 5:33; Yakobo 1:19)—9/1, ukurasa 20.

▫ Ni nini njia moja ambayo Yehova huandaa uvumilivu kwa wale wanaokabili majaribu?

Yehova hufanya hivyo kupitia vielelezo vya uvumilivu vilivyorekodiwa katika Neno lake, Biblia. (Warumi 15:4) Tunapotafakari juu ya hivyo, tunatiwa moyo kuvumilia, na pia tunajifunza mengi juu ya jinsi ya kuvumilia.—9/15, kurasa 11-12.

▫ Ujitoaji kimungu ni nini?

Ujitoaji kimungu hurejezea ujitoaji kwa Yehova ambao hutusukuma kufanya yale yanayompendeza, hata tunapokabili majaribu magumu, kwa sababu twampenda Mungu kutoka moyoni.—9/15, ukurasa 15.

▫ Twapaswa kuionaje rehema ya Mungu?

Hatupaswi kamwe kuipuuza rehema kuu ya Mungu. Twapaswa kuwa kama Paulo na kuonyesha uthamini wetu kwa kung’ang’ana dhidi ya kutokamilika kwetu wenyewe. (1 Wakorintho 9:27) Kwa njia hiyo tutaonyesha kwamba tuna tamaa ya kweli ya kufanya yaliyo mema, hata tunapokabili magumu.—10/1, ukurasa 23.

▫ Kwa nini yafaa kwamba Paulo aliorodhesha ustahimilivu ukiwa sehemu ya kwanza ya upendo?

Imesemwa kwamba ushirika wa Kikristo hauwezekani hata kidogo bila ustahimilivu, au bila kuchukuliana kwa subira. Ni hivyo kwa sababu sisi sote ni watu wasiokamilika, na kutokamilika kwetu na udhaifu wetu mbalimbali huwajaribu wengine. Kwa hiyo, ustahimilivu ni jambo la msingi ikiwa upendo utakuweko kati ya ndugu.—10/15, ukurasa 21.

▫ Je! Wakristo wa kwanza walitumia jina la Mungu?

Ithibati yasema ndiyo. Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali kwa Mungu hivi: “Jina lako litukuzwe.” (Mathayo 6:9) Na mwishoni mwa huduma yake, yeye alisali hivi: “Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu.” (Yohana 17:6) Zaidi ya hayo, nakala za mapema za Septuagint zilikuwa na jina la Mungu kwa namna ya Tetragramatoni ya Kiebrania.—11/1, ukurasa 30.

▫ Ni vielelezo vipi vya Biblia vionyeshavyo kwamba njia tunayoshughulikia makosa yetu yaweza kuathiri maisha zetu?

Mfalme Sauli alikinza shauri kwa ukaidi, na makosa yake yaliongezeka, hatimaye yakifikia upeo katika kifo chake bila upendeleo wa Mungu. (1 Samweli 15:17-29) Kwenye upande ule mwingine, yajapokuwa makosa na dhambi zake, Mfalme Daudi alikubali usahihisho kwa kutubu akabaki akiwa mwaminifu kwa Yehova. Vielelezo hivyo vya Biblia vyaonyesha kwamba kukubali makosa yetu hutusaidia tudumishe uhusiano mzuri na Mungu na hivyo kuwa na taraja la uhai wa milele. (Zaburi 32:1-5)—11/15, kurasa 29-30.

▫ Yehova husaidiaje watu wake wanapokuwa katika msononeko kwa sababu ya misiba ya asili au mambo mengine?

Yehova husaidia, si kwa kutangua kani za asili kimuujiza au kwa tendo jingine linalozidi nguvu za kibinadamu, bali kwa kani nyingine ambayo watu walio wengi hawaelewi kikweli—upendo. Ndiyo, Yehova huwapenda watu wake kikweli, na amekuza kati yao upendo kwa ajili ya mmoja na mwenzake ulio wenye nguvu sana hivi kwamba aweza kuwatimizia jambo ambalo laonekana kuwa la kimuujiza. (1 Yohana 4:10-12, 21)—12/1, ukurasa 10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki