Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 11/15 kur. 8-9
  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Poland

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Poland
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ujasiri Katika Kufunua Uongo
  • ‘Kwa Matunda Yao’
  • Dini Katika Poland ya Leo
    Amkeni!—1998
  • Kitabu-mwaka cha Mashahidi wa Yehova 1990
    1990 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Thailand
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 11/15 kur. 8-9

Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—Poland

KATIKA msimu wa vuli wa 1989, serikali za Kikomunisti kutoka Baltiki hadi Bahari Nyeusi zilianza kuporomoka. Wakati Ukuta Usiopitika ulikuwa ukibomolewa, mataifa ya Ulaya Mashariki yakaanza kutafuta miongozo yao wenyewe. Miongoni mwayo kulikuwa Poland, nchi yenye vilima vyenye miteremko, nyanda tambarare, na milima yenye mawe-mawe.a

Wapoland ni wafanyakazi wenye bidii, na Poland imetoa baadhi ya wachoraji na wanasayansi wanaojulikana ulimwenguni. Hata hivyo, zaidi ya hayo, sasa kuna jeshi linaloongezeka la wapiga-mbiu wa habari njema za Ufalme wa Mungu.

Ujasiri Katika Kufunua Uongo

Katika Poland kuna wengi ambao wangependa kujifunza kweli kutoka kwa Biblia. Lakini wengine huzuiwa na watu wao wa ukoo au majirani. Kwa mfano, kwenye ujirani wa Wrocław, mwanamke mmoja mwenye kupendezwa aliacha kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova wakati familia na marafiki walimpinga. Hata hivyo binti yake tineja alisoma mfululizo wa makala za Mnara wa Mlinzi zilizofunua dini ya uongo. Hizo zilichochea kupendezwa kwake na kweli.

Baada ya miezi sita ya kujifunza Biblia, msichana huyu mchanga aliamua kuacha kabisa dini ya uongo. Alimtembelea kasisi wa kanisa lake kumpasha habari juu ya uamuzi wake. Kasisi huyo alimwambia aandike yafuatayo: “Mimi, K—— P——, nakanusha imani ya Katoliki.”

Jumapili iliyofuata, taarifa hii ilisomwa kanisani. Babu ya msichana huyo alizimia, na nyanya yake akalia machozi. Hata hivyo, waumini wengine walivutiwa na kusema: “Hatimaye, kuna mtu hodari vya kutosha kusema kwamba kuna uongo mwingi sana katika kanisa letu.” Tineja huyu mwenye moyo mkuu sasa ni dada wa kiroho aliyebatizwa naye ameanzisha mafunzo ya Biblia saba katika kijiji chake.

‘Kwa Matunda Yao’

Gazeti la kila juma Kujawy i Pomorze lilichapisha ripoti “Mtawatambua kwa Matunda Yao.” Kwa sehemu, makala hiyo ilisema kwamba waabudu katika Jumuiya ya Wakristo “kwa uhalisi hawachukui kwa uzito kanuni za kidini walizozikubali. Wao watofautiana kabisa na Mashahidi wa Yehova wanaotenda wanachosema, nao husema yale Biblia inaamuru.”

Baada ya kutofautisha jinsi Mashahidi wanavyoonekana na jinsi Wakristo wa jina tu walivyo, ripoti hiyo yaendelea kusema: “Huenda [Wakristo wa jina tu] hawajui, na mara nyingi hawatendi kulingana na kweli na kanuni muhimu za imani yao. . . . Kwa mtazamo wao, Mashahidi wa Yehova wanaonyesha upatano wa maneno na matendo yao, hivyo wakithibitisha kwamba wao si ‘manabii wa uongo,’ badala ya hivyo, wanaweza kutambulika kwa matunda yao. ‘Je! watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?’ (Mathayo 7:15-20).”

Mwanamke mmoja aliandika barua kwa Przyjaciółka la kila juma, akiomboleza kwamba mwanaye aliacha Kanisa Katoliki na kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Mhariri alimshaurije? “Ikiwa mwanao alianza kushirikiana na Mashahidi wa Yehova, akajifunza na kukubali imani yao, yote hayo ni uamuzi wake mwenyewe, unaofaa kutambuliwa na kuheshimiwa. . . . Kikundi hiki cha kidini kina sifa nyingi za kijamii zenye kupendeza na zenye kuvutia, kama vile umoja wao usio wa kawaida katika muungano wa kindani sana, unyoofu mkubwa sana na kufuata sana sheria zinazokubalika katika maisha ya kijamii, na mwishowe, uwezo wao wa kuishi kulingana na kweli yao, wakikamilisha kwa matendo kanuni wanazodai kufuata. Hizi ni sifa njema.”

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari zaidi, ona 1994 Calendar of Jehovah’s Witnesses.

[Sanduku katika ukurasa wa 9]

HABARI ZA NCHI

Mwaka wa Utumishi wa 1993

KILELE CHA WANAOTOA USHAHIDI: 113,551

UWIANO: Shahidi 1 kwa Watu 339

HUDHURIO LA UKUMBUSHO: 235,642

WASTANI WA WAHUBIRI WALIO MAPAINIA: 7,961

WASTANI WA MAFUNZO YA BIBLIA: 79,131

IDADI YA WALIOBATIZWA: 8,164

IDADI YA MAKUTANIKO: 1,397

OFISI YA TAWI: Nadarzyn

[Picha katika ukurasa wa 9]

Ofisi ya tawi ya Poland katika Lodz katika 1948

[Picha katika ukurasa wa 9]

Kazi ya kuweka matangazo, Juni 1948, katika ile iliyokuwa Prussia Mashariki

[Picha katika ukurasa wa 9]

Washiriki 72 wa Betheli ya Poland, Januari 1993

[Picha katika ukurasa wa 9]

Ofisi mpya ya tawi katika Nadarzyn

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki