Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 3/1 kur. 29-31
  • Tatizo la Kitheolojia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tatizo la Kitheolojia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Chanzo na Ukuzi wa Tatizo Hilo
  • Je, Paulo Aliamini Ile “Hali ya Katikati”?
  • Ufufuo—Kweli ya Biblia Iliyo Nzuri Ajabu
  • Jizoeze Imani Ili Upate Uhai wa Milele
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Imani Yako Katika Ufufuo Ni Yenye Nguvu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Ufufuo, Siku ya Hukumu na Uasi-imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kuzaliwa Pamoja na Nafsi Isiyokufa au Ufufuo—Ni Jambo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 3/1 kur. 29-31

Tatizo la Kitheolojia

“WAZO la kutokufa kwa nafsi na imani katika ufufuo wa wafu . . . ni dhana mbili zilizo tofauti kabisa, ambazo ni lazima uchaguzi mmoja ufanywe kati yazo.” Maneno haya ya Philippe Menoud yaonyesha kwa ufupi tatizo likabiliwalo na wanatheolojia wa Kiprotestanti na Kikatoliki juu ya hali ya wafu. Biblia yasema juu ya tumaini la ufufuo katika “siku ya mwisho.” (Yohana 6:39, 40, 44, 54) Lakini tumaini la waamini wengi, asema mwanatheolojia Gisbert Greshake, “lategemea kutokufa kwa nafsi, inayojitenga na mwili wakati wa kufa na kurudi kwa Mungu, huku tumaini katika ufufuo likiwa limetoweka sana, ama kabisa.”

Katika hali hiyo, tatizo kubwa lazuka, aeleza Bernard Sesboüé: “Hali ya wafu ni nini wakati wa kile ‘kipindi’ cha kati ya kifo chao cha kimwili na ufufuo wa mwisho?” Swali hilo laonekana limekuwa mada ya mjadala wa kitheolojia katika miaka michache ambayo imepita. Ni nini kilifanya lizushwe? Na jambo la maana zaidi, tumaini halisi la wafu ni nini?

Chanzo na Ukuzi wa Tatizo Hilo

Wakristo wa kwanza walielewa wazi suala hilo. Wao walijua kutoka kwa Maandiko kwamba wafu hawajui lolote, kwa kuwa Maandiko ya Kiebrania yasema: “Walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote . . . Hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.” (Mhubiri 9:5, 10) Wakristo hao walitumaini ufufuo kutukia katika wakati wa “kuwapo kwa Bwana” kwa wakati ujao. (1 Wathesalonike 4:13-17, NW) Wao hawakutazamia kuwa na fahamu mahali fulani wakingojea wakati huo. Joseph Ratzinger, ambaye ni ofisa mkuu wa wakati huu wa Kundi la Vatikani la Fundisho la Imani, asema hivi: “Hakuna uthibitisho uliokuwa katika Kanisa la kale juu ya kutokufa kwa nafsi.”

Hata hivyo, Nuovo dizionario di teologia, yaeleza kwamba tuliposoma maandishi ya Mababa wa Kanisa, kama vile Augustine au Ambrose, “tulikuja kung’amua jambo jipya kwa habari ya mapokeo ya Kibiblia—kuibuka kwa mafundisho ya Kigiriki ya hali zinazopata binadamu, kwa msingi yakitofautiana sana na yale ya Wakristo-Wayudea.” Fundisho hili jipya lilitegemezwa kwa “kutokufa kwa nafsi, kuhukumiwa kwa mtu mmoja-mmoja kwa kuthawabishwa au kuadhibiwa mara baada ya kifo.” Basi, swali lilizushwa juu ya ile “hali ya katikati”: Ikiwa nafsi huokoka kifo cha mwili, ni nini huipata inapongojea ufufuo katika “siku ya mwisho”? Hili ndilo tatizo ambalo wanatheolojia wameng’ang’ana kusuluhisha.

Katika karne ya sita W.K., Papa Gregory 1 alibisha kwamba wakati wa kifo, mara hiyo nafsi huenda mahali zilipopangiwa kimbele. Papa John 22 wa karne ya 14 alisadiki kabisa kwamba wafu wangepokea thawabu yao katika Siku ya Hukumu. Hata hivyo, Papa Benedict 12, alikanusha mtangulizi wake. Katika barua ya kipapa Benedictus Deus (1336), yeye aliamuru kwamba “nafsi za wafu huingia katika raha mstarehe [mbinguni], hutakaswa [purgatori], au huadhibiwa [helo] mara tu baada ya kifo, ili ziunganishwe tena na miili yazo iliyofufuliwa katika mwisho wa ulimwengu.”

Kujapo ubishi na mjadala, huo umekuwa msimamo wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo kwa karne nyingi, ingawa makanisa ya Kiprotestanti na Kiorthodoksi kwa ujumla hayaamini purgatori. Hata hivyo, tangu mwisho wa karne ya mwisho, wasomi wanaozidi kuongezeka wameonyesha watu chanzo kisicho cha Kibiblia cha fundisho la kutokufa kwa nafsi, na matokeo ni kwamba, “theolojia ya kisasa hujaribu kumwona mtu kuwa kitu kimoja kinachokwisha kabisa katika kifo.” (The Encyclopedia of Religion) Kwa hiyo, wafafanuzi wa Biblia, hupata ugumu kuthibitisha kuwapo kwa ile “hali ya katikati.” Je, Biblia yakitaja, au yatoa tumaini jingine tofauti?

Je, Paulo Aliamini Ile “Hali ya Katikati”?

Catechism of the Catholic Church chasema hivi: “Ili tuinuke na Kristo, ni lazima tufe na Kristo: ni lazima ‘tusiwe katika mwili na kukaa pamoja na Bwana’. [2 Wakorintho 5:8] Katika ‘kuondoka’ huko ambako ni kifo, nafsi hutenganishwa na mwili. [Wafilipi 1:23] Itaunganishwa na mwili katika siku ya ufufuo wa wafu.” Lakini katika maandiko yaliyonukuliwa hapa, je, mtume Paulo asema kwamba nafsi huokoka kifo cha mwili na kisha kungojea “Hukumu ya Mwisho” ili iunganishwe tena na mwili?

Katika 2 Wakorintho 5:1, Paulo arejezea kifo chake naye asema juu ya ‘nyumba ya dunia’ ambayo ‘ingeharibiwa.’ Je, alikuwa akifikiri juu ya mwili ulioachwa na nafsi yao isiyoweza kufa? La. Paulo aliamini kwamba mtu ni nafsi, si kwamba anayo nafsi. (Mwanzo 2:7; 1 Wakorintho 15:45) Paulo alikuwa Mkristo mtiwa-mafuta ambaye tumaini lake, kama lile la ndugu zake wa karne ya kwanza, ‘aliwekewa akiba mbinguni.’ (Wakolosai 1:5; Warumi 8:14-18) Hivyo basi, ‘tamaa’ yake ilikuwa ni kufufuliwa mbinguni katika wakati uliowekwa na Mungu akiwa kiumbe cha roho kisichoweza kufa. (2 Wakorintho 5:2-4) Akisema juu ya tumaini hili, yeye aliandika hivi: “Sote tutabadilika . . . wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.”—1 Wakorintho 15:51, 52, italiki ni zetu.

Katika 2 Wakorintho 5:8, Paulo asema: “Tuna moyo mkuu; nasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana.” Wengine huamini kwamba maneno hayo hurejezea ile hali ya katikati ya kungojea. Watu kama hao pia hurejezea ahadi ya Yesu kwa wafuasi wake waaminifu kwamba alienda kuwaandalia mahali ‘awakaribishe kwake.’ Lakini mataraja hayo yangetimizwa lini? Kristo alisema kwamba ungekuwa wakati ‘angekuja tena’ katika kuwapo kwake kwa wakati ujao. (Yohana 14:1-3) Kwa njia iyo hiyo, katika 2 Wakorintho 5:1-10, Paulo alisema kwamba tumaini la ujumla la Wakristo watiwa-mafuta lilikuwa kurithi makao ya kimbingu. Hilo lingetimizwa, si kupitia kule kutokufa kwa nafsi kunakodhaniwa, bali kupitia ufufuo wa wakati wa kuwapo kwa Kristo. (1 Wakorintho 15:23, 42-44) Mfafanuzi wa mambo Charles Masson akata kauli kwamba 2 Wakorintho 5:1-10 “laweza kueleweka wazi bila kujaribu kutumia nadharia ya ile ‘hali ya katikati.’”

Katika Wafilipi 1:21, 23, Paulo asema hivi: “Kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida. Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo; maana ni vizuri zaidi sana.” Je, hapo Paulo arejezea ile “hali ya katikati”? Wengine hufikiri hivyo. Hata hivyo, Paulo asema kwamba alikuwa amesongwa na mawezekano mawili—uhai au kifo. Lakini “ninatamani,” yeye akaongezea, akitaja uwezekano wa tatu, “kwenda zangu nikae na Kristo.” Je, ni “kwenda” kuwa na Kristo mara tu baada ya kifo? Kama tulivyoona tayari, Paulo aliamini kwamba Wakristo watiwa-mafuta walio waaminifu wangefufuliwa wakati wa kuwapo kwa Kristo. Kwa hiyo, ni lazima alikuwa akisema juu ya matukio ya wakati huo.

Hilo laweza kuonekana kwa maneno yake katika Wafilipi 3:20, 21 na 1 Wathesalonike 4:16. “Kwenda” huko wakati wa kuwapo kwa Kristo Yesu kungewezesha Paulo kupokea thawabu ambayo Mungu alikuwa amemwekea. Uhakika wa kwamba hili lilikuwa tumaini lake laonekana katika maneno yake kwa kijana Timotheo: “Baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.”—2 Timotheo 4:8.

Ufufuo—Kweli ya Biblia Iliyo Nzuri Ajabu

Wakristo wa kwanza waliona ufufuo kuwa tukio ambalo lingeanza wakati wa kuwapo kwa Kristo, nao walipokea nguvu na faraja kutoka kwa kweli hii ya Biblia iliyo nzuri ajabu. (Mathayo 24:3; Yohana 5:28, 29; 11:24, 25; 1 Wakorintho 15:19, 20; 1 Wathesalonike 4:13) Kwa uaminifu wao walingojea shangwe hiyo ya wakati ujao, wakikataa mafundisho ya uasi-imani ya nafsi isiyoweza kufa.—Matendo 20:28-30; 2 Timotheo 4:3, 4; 2 Petro 2:1-3.

Bila shaka, si Wakristo wenye tumaini la kimbingu pekee wanaopata ufufuo. (1 Petro 1:3-5) Wazee wa ukoo na watumishi wengine wa kale wa Mungu walidhihirisha imani katika uwezo wa Yehova wa kuwarudisha wafu kwenye uhai duniani. (Ayubu 14:14, 15; Danieli 12:2; Luka 20:37, 38; Waebrania 11:19, 35) Hata yale mabilioni ya watu ambao hawakumjua Mungu katika karne zilizopita wana fursa ya kurudishwa kwenye uhai katika paradiso ya kidunia, kwa kuwa “kutakuwa na ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia.” (Matendo 24:15; Luka 23:42, 43) Je, hilo si tazamio zuri ajabu?

Badala ya kutufanya tuamini kwamba kuteseka na kifo kitakuwako sikuzote, Yehova atuonyesha wakati ‘adui wa mwisho, mauti,’ atakapoondolewa milele na jamii ya wanadamu yenye uaminifu itaishi milele katika dunia itakayorudishwa kuwa Paradiso. (1 Wakorintho 15:26; Yohana 3:16; 2 Petro 3:13) Itakuwa vizuri kama nini kuwaona wapendwa wetu wakirudia uhai! Tumaini hili hakika ni zuri kama nini kuliko ile dhana ya kutokufa kwa nafsi ya kibinadamu—fundisho ambalo halitegemezwi kwa Neno la Mungu, bali falsafa za Kigiriki! Ukitegemeza tumaini lako katika ahadi ya Mungu iliyo hakika, wewe pia waweza kuwa na hakika kwamba karibuni “mauti haitakuwapo tena”!—Ufunuo 21:3-5.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Ufufuo ni kweli ya Biblia iliyo nzuri ajabu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki