Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 4/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Umati Mkubwa wa Waabudu wa Kweli—Umetoka Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Zizi la Karibuni kwa Ajili ya “Kondoo Wengine”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • “Mchungaji Mwema” na “Kondoo Wengeni” Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 4/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Kusema kwa usahihi kabisa, je, kuna tofauti yoyote kati ya maneno ya Biblia “kondoo wengine” na “umati mkubwa”?

Ndiyo, ingawa hatuhitaji kuwa wenye kutaka usahihi kupita kiasi juu ya utumizi wa maneno au kuudhika mtu atumiapo maneno hayo kwa kubadilikana.

Wakristo wengi hufahamu maandiko tunamopata maneno hayo. Yohana 10:16 ni mojayapo. Hapo Yesu alisema hivi: “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.” Ule usemi mwingine, “umati mkubwa,” uko kwenye Ufunuo 7:9. Twasoma hivi: “Baada ya hayo nikaona, na tazama, [“umati mkubwa,” NW] sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao.”

Ebu tuchunguze kwanza Yohana 10:16. Kondoo ni akina nani? Twapaswa kung’amua kwamba wafuasi wote wa Yesu walio waaminifu-washikamanifu hurejezewa kuwa kondoo. Kwenye Luka 12:32, yeye aliwaita wale wa wanafunzi wake ambao wangeenda mbinguni kuwa “kundi dogo” lake. Kundi la nini? La kondoo. “Kondoo” wa lile “kundi dogo” watakuwa sehemu ya ule Ufalme mbinguni. Hata hivyo, kuna wengine, wale wenye tumaini tofauti, ambao Yesu awaona pia kuwa kondoo.

Twaweza kuona hilo kwenye Yohana sura ya 10. Baada ya kusema juu ya kondoo, kama vile mitume wake, ambao angewaita kwenye uhai mbinguni, Yesu aliongeza hivi katika mstari wa 16: “Kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta.” Kwa muda mrefu Mashahidi wa Yehova wametambua kwamba katika mstari huu Yesu alikuwa akisema juu ya watu wenye mataraja ya uhai duniani. Waaminifu wengi katika nyakati za kabla ya Ukristo, kama vile Abrahamu, Sara, Noa, na Malaki, walikuwa na mataraja kama hayo. Kwa hiyo, kwa kufaa twaweza kuwatia ndani kuwa sehemu ya “kondoo wengine” wa Yohana 10:16. Wakati wa Mileani, mashahidi hao waaminifu wa kabla ya Ukristo watafufuliwa nao watajifunza juu ya Kristo Yesu na kumkubali, nao watakuwa “kondoo wengine” wa yule Mchungaji Mwema.

Twajua pia kwamba tangu ule mwito wa ujumla wa wale watakaoenda mbinguni kwisha, mamilioni wamekuja kuwa Wakristo wa kweli. Hao pia waitwa kwa kufaa “kondoo wengine,” kwa kuwa wao si sehemu ya lile “kundi dogo.” Badala ya hivyo, wale kondoo wengine leo watazamia kuishi kuingia ndani ya paradiso ya kidunia.

Sasa, ni nini linaloweza kusemwa juu ya utambulisho wa ule “umati mkubwa” unaotajwa kwenye Ufunuo 7:9, (NW)? Ebu tazama mstari wa 13 na swali hili, ‘Wao ni akina nani? nao wametoka wapi?’ Twapata jibu kwenye Ufunuo 7:14: “Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu.” Kwa hiyo ule “umati mkubwa” umefanyizwa na wale wanaopita, na kutoka katika, au kuokoka, ile dhiki kubwa. Kama vile mstari wa 17 usemavyo, wao ‘wataongozwa kwenye chemchemi za maji yenye uhai,’ duniani.

Ingawa hivyo, yaeleweka kwamba ili hao waokoke dhiki kubwa, ni lazima tayari wawe wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo, wakija kuwa waabudu wa kweli. Kwa hiyo, ingawa Ufunuo 7:9 lasimulia juu ya umati huo baada ya dhiki, twaweza kutumia maneno “umati mkubwa” kwa wote wale wenye matumaini ya kidunia ambao sasa wanamtolea Yehova Mungu utumishi mtakatifu, kabla tu ya dhiki kubwa kufyatuka kwa mataifa kushambulia dini ya uwongo.

Kwa ufupi, twaweza kukumbuka “kondoo wengine” kuwa usemi mpana, unaotia ndani watumishi wote wa Mungu wenye tumaini la kuishi milele duniani. Watia ndani kikundi kidogo kwa kulinganisha cha watu wenye mfano wa kondoo wanaokusanywa kuwa “umati mkubwa” wenye tumaini la kuishi kupitia dhiki kubwa inayokaribia kutokea. Wengi wa Wakristo hao waaminifu washikamanifu walio hai leo ni wa “kondoo wengine,” nao vilevile ni sehemu ya “umati mkubwa.”

Yafaa kutajwa tena kwamba ingawa ni vema kuwa hususa katika mambo hayo, hakuna haja kwa Mkristo yeyote kuhangaikia maneno kupita kiasi—lile liwezalo kuitwa kuwa mchambuzi sana wa maneno. Paulo alionya juu ya wengine ‘waliojivuna’ na kujihusisha katika “mashindano ya maneno.” (1 Timotheo 6:4) Ikiwa sisi binafsi tumetambua tofauti fulani kati ya maneno, ni vema. Hata hivyo, hatuhitaji kumchambua mwenzetu ama waziwazi ama kindani-ndani, ambaye huenda asitumie maneno ya Biblia kwa usahihi kabisa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki