Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 8/15 kur. 4-7
  • Hofu Itakwisha Lini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hofu Itakwisha Lini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Usalama Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu
  • Ulimwengu Bila Wezi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Kukabiliana Na Uhalifu Katika Ulimwengu Wenye Machafuko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Tunaweza ‘Kuvumilia Mpaka Mwisho’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Wewe Unataka Uhalifu Umalizwe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 8/15 kur. 4-7

Hofu Itakwisha Lini?

JE, UNGESHANGAA kujua kwamba usalama wa kweli unahusianishwa na mtu aliyeishi miaka 2,000 iliyopita? Akionyesha uhitaji wa upendo, Yesu Kristo alieleza mfano huu wenye kutokeza: “Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.” Ijapokuwa wasafiri wawili hawakujishughulisha na mtu huyo, Msamaria mwenye fadhili alionyesha huruma. Lakini, ni nani hujali wanaodhulumiwa na uhalifu leo? Tunaweza kutazamia msaada gani kutokana na hofu?—Luka 10:30-37.

Huku wakidai kumwamini Mungu, wengi hufikiri kwamba sheria na utaratibu zapaswa kutekelezwa na mwanadamu. Lakini je, adhabu kali ya kifungo au polisi wengi na wenye kulipwa mshahara mzuri zaidi watakomesha uhalifu wenye jeuri? Je, kweli unaamini kwamba mashirika ya kutekeleza sheria, yajapofanya jitihada za unyoofu za kuandaa usalama wa kadiri fulani, yataondolea mbali mambo kama vile uzoefu wa dawa za kulevya, uhalifu wa magenge, na umaskini? Hata hivyo, njaa na kiu yetu kwa ajili ya uadilifu haipaswi kuwa ya bure.—Mathayo 5:6.

Zaburi 46:1 husema hivi: “Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.” Tutaona kwamba maneno hayo si shairi nzuri tu.

Kama ujuavyo, vyombo vya habari kila siku huripoti mauaji mengi katika vita vya wenyewe kwa wenyewe na mashambulizi ya maharamia. Katika sehemu fulani za ulimwengu, limekuwa jambo la kawaida kuwaua watoto wasiotakikana au wanaojionea uhalifu. Kwa nini uhai umekuwa wenye thamani ndogo namna hiyo? Ingawa huenda kukawa na visababishi mbalimbali vya jeuri kama hiyo, kuna sababu moja tusiyopaswa kupuuza.

Kulingana na Neno la Mungu, Biblia, ‘dunia yote hukaa katika yule mwovu.’ (1 Yohana 5:19) Kwa kweli, Yesu Kristo alimtambulisha Shetani Ibilisi kuwa mwongo na “muuaji.” (Yohana 8:44) Kikiathiri wanadamu katika njia mbalimbali, kiumbe hiki cha roho chenye nguvu nyingi kinaendeleza ongezeko la jeuri leo. “Ole wa nchi na bahari! kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu,” yasema Ufunuo 12:12. Kwa furaha, nafasi ya mfumo huu mwovu itachukuliwa na “mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.”—2 Petro 3:13.

Ni msaada gani tulio nao sasa hivi, kuongezea tumaini hili tukufu la ulimwengu mpya?

Kabla ya kuchunguza jibu lifaalo la swali hilo, ni vizuri kukumbuka kwamba hata Wakristo wa kweli hawajahakikishiwa kwamba watalindwa kutokana na uhalifu. Mtume Paulo alifafanua hatari fulani alizokabili yeye mwenyewe. Yeye alipata kuwa katika “hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa [lake]; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini.” (2 Wakorintho 11:26) Bado Paulo aliokoka hatari hizo. Ndivyo ilivyo leo; tukiwa wenye busara, bado twaweza kuendelea na kazi zetu kwa ukawaida iwezekanavyo. Acheni tufikirie mambo fulani yatakayosaidia.

Ikiwa unaishi mahali hatari, mwenendo mzuri waweza kuwa ulinzi, kwa kuwa watu huchunguza wengine kwa makini. Ingawa wezi hupanga na kutekeleza uhalifu, wengi hujiona kuwa watu wa kawaida. Epuka kuchambua yale wafanyayo, na usijaribu kujua wanachohusika nacho. Hivyo, unaweza kupunguza uwezekano wa kuwa shabaha ya kulipiziwa kisasi. Ukumbuke kwamba wezi hujaribu kuchunguza ni nani amenunua kitu kipya au ni nani aendaye likizoni na hivyo hawatakuwa nyumbani, hivyo uwe mwenye busara kwa yale unafunulia wengine.

Mashahidi wa Yehova walio wengi wamegundua kwamba sifa yao ya kuwa wahudumu imewaletea kadiri fulani ya ulinzi. Mara nyingi wahalifu wameonyesha kwamba wanaheshimu Wakristo kama hao, ambao hujitoa bila upendeleo kusaidia watu katika jamii. Mashahidi si wauaji au wezi, wala wao ‘hawajishughulishi na mambo ya watu wengine,’ hivyo wao si hatari.—1 Petro 4:15.

Usalama Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu

Tunasikitikia “kuongezeka kwa maasi” yaliyotabiriwa na Yesu Kristo, lakini badala ya kuwa wenye masumbufu kupita kiasi, twaweza kuwa na uhakika kwamba karibuni Mungu ataondolea mbali mfumo huu mwovu. Zaidi ya kutabiri juu ya kuhubiriwa kwa “habari njema ya ufalme,” ulimwenguni pote, Yesu aliwakumbusha wafuasi wake hivi: “Mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.”—Mathayo 24:12-14.

Tunaweza kuwa na hakika kwamba wale hushambulia wenzao, nyakati nyingine kwa ukatili wa unyama, wataharibiwa. Mithali 22:22, 23 lasema hivi: “Usimnyang’anye maskini, kwa kuwa ni maskini; wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni; kwa sababu BWANA atawatetea; naye atawateka uhai wao waliowateka.” Yehova atawaondolea mbali waovu, kama vile wezi, wauaji kimakusudi, na wapotovu wa ngono. Zaidi ya hayo, hatawapuuza waliopatwa na uhalifu kama huo. Atawarudishia waliyopoteza na kuwapa afya kamili.

Kwa kweli, wale ‘wanaojiepua na uovu, na kutenda mema’ watapata uhai udumuo milele ama kwa kuokoka dhiki kuu ijayo ama kwa kufufuliwa kutoka kwa wafu. “Wenye haki watairithi nchi, nao watakaa humo milele.” (Zaburi 37:27-29) Manufaa kama hizo zitapatikana kwa sababu ya fidia ya dhabihu ya Yesu. (Yohana 3:16) Lakini maisha yatakuwaje katika Paradiso iliyorudishwa?

Maisha katika Ufalme wa Mungu yatakuwa yenye raha kwelikweli. Yehova atabiri hivi: “Watu wangu watakaa katika kao la amani; na katika maskani zilizo salama, na katika mahali pa kupumzikia penye utulivu.” (Isaya 32:18) Wote wapatao uhai udumuo milele watakuwa wamerekebisha utu wao. Hakuna atayekuwa mwovu au asiyefuata haki, wala hakuna yeyote atakayeelekea kuumizwa na mtu kama huyo. Nabii Mika asema hivi: “Wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake, na chini ya mtini wake; wala hapana mtu atakayewatia hofu.” (Mika 4:4; Ezekieli 34:28) Ni tofauti iliyoje na ujirani wa leo ulio hatari!

[Sanduku katika ukurasa wa 6]

UWE MWENYE TAHADHARI

Wahalifu wengi hufanya kazi hiyo wakati wote, wakifanya uhalifu uwe kazi yao ya wakati wote. Hata ikiwa mmoja tu ndiye atakayekuonyesha bunduki, huenda wanafanya kazi kwa kikundi cha watu wawili au watatu. Ushuhuda unaoongezeka waonyesha kwamba kadiri mhalifu alivyo mchanga zaidi, ndivyo alivyo hatari zaidi. Waweza kufanyaje ushambuliwapo?

Dumisha utulivu ili usimwogopeshe mwizi—ukosefu wake wa ujuzi waweza kuua. Ikiwa wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova, jijulishe hivyo. Hata hivyo, uwe tayari kumpa mwizi atakacho. Ukikawia, hatari inaongezeka. Baadaye, huenda ukahisi kwamba ni salama kumwomba kitambulisho chako au nauli.

Mara nyingi huwezi kujua ni nani aliye mhalifu. Wezi fulani ni wazoefu wa dawa za kulevya au wahalifu stadi, wengine wanataka tu pesa za kununua chakula. Kwa vyovyote, usibebe pesa kiasi kikubwa. Epuka kuonyesha vito, pete za dhahabu, au saa za thamani. Tembea na usafiri kikawaida, bila kudhihirisha hofu. Usikazie macho watu fulani kana kwamba unataka kuwatambulisha. Bunduki ikifyatuliwa barabarani, jitupe chini; nguo zaweza kufuliwa baadaye.—Aliyekuwa polisi katika Rio de Janeiro.

[Picha katika ukurasa wa5]

Dumisha utulivu na umpe mwizi atakacho. Ukikawia, hatari inaongezeka

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki