Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 8/15 uku. 31
  • Je, Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Mchapishaji Aliyepata Sifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kwa Nini Utafute Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Wakristo Huabudu kwa Roho na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Je, Kweli ya Kidini Yaweza Kupatikana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 8/15 uku. 31

Je, Wakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, utapendezwa kukumbuka yafuatayo:

▫ Je, kweli ya kidini yaweza kupatikana?

Yesu Kristo alisema: “Mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” (Yohana 8:32) Yesu hakuonyesha tu kwamba kweli yaweza kupatikana bali alionyesha pia kwamba kuitafuta kunatakiwa katika ibada yetu ya Mungu. Alimwambia mwanamke Msamaria hivi: “Waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli.” (Yohana 4:23)—4/15, ukurasa 5.

▫ Robert Estienne alikuwa nani, naye alipataje sifa?

Robert Estienne alikuwa mchapishaji aliyeishi katika karne ya 16. Alitoa maisha yake kwa uchapishaji wa Maandiko Matakatifu akajaribu kufunua maneno ya Biblia kama yalivyoandikwa awali. Mfumo wake wa kugawanya andiko la Biblia katika mistari yenye nambari ungali unatumiwa ulimwenguni pote leo.—4/15, kurasa 10, 14.

▫ Tunanufaikaje na kusoma Biblia kila siku?

Maandiko hupata maana mpya kwetu kila wakati, na unabii mbalimbali unaohusu siku za mwisho huja kuvutia hata zaidi kwa sababu ya yale tumeona, tumesikia, na kujionea binafsi. Maono yetu maishani yaongezekapo na tunapokabili matatizo, twatambua kikamili shauri la Biblia. (Mithali 4:18)—5/1, ukurasa 14.

▫ Maandiko ya Biblia yaweza kukumbukwaje?

Usomapo Biblia, weka alama maandiko yaliyochaguliwa ambayo unataka kukumbuka, au uyanakili katika kadi na kuziweka mahali utakapokuwa unaziona kila siku. Unapojaribu kuikariri mistari, uitafakari na kuitumia. Usijaribu kukariri mistari mingi pamoja, labda moja au miwili kila juma.—5/1, kurasa 16, 17.

▫ Gospeli ya Luka ina habari gani ambayo ni nyongeza ya yale yanayoandaliwa na waandikaji wengine wa Gospeli?

Ingawa mambo mengi yaliyorekodiwa na Luka yanafanana na yale yaliyo katika simulizi la Mathayo, asilimia 59 ni tofauti. Luka alirekodi miujiza sita ipatikanayo katika kitabu chake pekee naye aliripoti zaidi ya maradufu ya hesabu hiyo ya vielezi vya Yesu ambavyo havikutajwa na waandikaji wengine wa Gospeli.—5/15, ukurasa 12.

▫ Ni mmweko gani wenye kutokeza wa nuru ya kweli uliofunuliwa katika 1935?

Mwaka huo watu wa Yehova walikuja kuelewa kwamba umati mkubwa uliotajwa kwenye Ufunuo 7:9, 14 haukurejezea jamii ya pili ya kimbingu bali ulirejezea wale ambao tumaini lao lilikuwa la kidunia. (Yohana 10:16)—5/15, ukurasa 20.

▫ Tunaweza kufariji waliofiwa katika njia zipi zenye kutumika?

Sikiliza. Andaa kitia-moyo. Uwe mwenye kupatikana. Uwe mwenye kuchukua hatua ya kwanza ifaapo. Andika barua au kadi ya kufariji. Sali pamoja nao. (Yakobo 5:16) Endelea kuwasaidia.—6/1, kurasa 13, 14.

▫ Ndugu na dada wa kiroho wanaweza kufanya nini ili kusaidia wale wanaoishi katika nyumba zilizogawanyika kidini wavumilie?

Kwa ukawaida sema nao maneno yenye kutia moyo, yaliyo chanya, na yenye kufariji. (1 Wathesalonike 5:14) Hilo huburudisha akili yao na mwili wao. Inapowezekana na ifaapo, wahusishe katika utendaji wako wa kitheokrasi na kijamii. Uwatie katika sala zako. (Warumi 1:9; Waefeso 1:16)—6/1, ukurasa 29.

▫ Kudhihirisha saburi tunaposhiriki katika huduma ya shambani kutaleta thawabu zipi?

Saburi husaidia wahubiri wa Ufalme kuvumilia ubaridi na upinzani wowote. Badala ya kubishana na wenye nyumba wenye hasira, wahudumu wenye saburi wataweza kutoa jibu la upole au kuondoka kwa utulivu, hivyo wakidumisha amani na shangwe. (Mathayo 10:12, 13) Zaidi ya hayo, wenye mfano wa kondoo watavutwa na ujumbe wa Ufalme.—6/15, ukurasa 9.

▫ Kwa nini kujua kweli ya Biblia ni jambo lenye thamani sana?

Kujua kweli hutuweka huru kwa uwongo, madanganyo, na ushirikina. Tukiishi kupatana nayo, kweli hutuimarisha kuvumilia magumu na hutujaza sana tumaini liwezalo kutusaidia kusimama imara chini ya jaribu.—7/1, ukurasa 8.

▫ Ni daraka gani la msingi ambalo kutaniko la Kikristo lililotiwa mafuta lilitwaa kutoka kwa Israeli la asili?

Pendeleo la kutoa ushahidi juu ya ukuu wa Yehova miongoni mwa mataifa. (Isaya 43:21; 1 Petro 2:9)—7/1, ukurasa 19.

▫ Maneno ya mtume Petro kwamba mume anapaswa ‘kumpa heshima’ mke wake yanamaanisha nini? (1 Petro 3:7)

Mume anayemheshimu mke wake hamfedheheshi au kumshusha. Badala ya hivyo, yeye huonyesha kwa maneno yake na matendo yake—faraghani na hadharani—kwamba amstahi. (Mithali 31:10-31)—7/15, ukurasa 19.

▫ Kwa nini inaweza kusemwa kwamba ni jambo lenye upendo kumwondosha mkosaji asiyetubu kutoka kutaniko la Kikristo?

Kutenga na ushirika ni wonyesho wa upendo kwa Yehova na njia zake. (Zaburi 97:10) Kunaonyesha upendo kwa wale wanaofuatia mwendo mwadilifu kwa sababu kunaondosha kutoka kati yao mtu ambaye angeweza kutumia uvutano mbaya kwao; kufanya hivyo kwalinda pia usafi wa kutaniko. (1 Wakorintho 5:1-13)—7/15, ukurasa 25.

▫ “Mtumwa mwaminifu mwenye akili,” aliyetajwa na Yesu kwenye Mathayo 24:45-47, aweza kutambuliwaje leo?

Wanatambuliwa hasa kwa kazi wafanyayo ya kuandaa vichapo vyenye msingi wa Biblia, katika kufundisha na kuhubiri “habari njema ya ufalme,” na kwa ushikamano wao wa karibu na Neno la Mungu, Biblia. (Mathayo 24:14; 28:19, 20)—8/1, ukurasa 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki