Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 9/15 kur. 24-25
  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—India

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—India
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Imara kwa Ajili ya Ibada Safi Shuleni
  • Utii kwa Sheria ya Mungu Juu ya Damu Wathawabishwa
  • “Nimeshika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • “Kutoka Kinywani mwa Watoto Wachanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Kitabu-mwaka cha Mashahidi wa Yehova 1990
    1990 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 9/15 kur. 24-25

Mashahidi wa Yehova Ulimwenguni Pote—India

INDIA! Hiyo kontinenti ndogo yenye kuenea sana ni makao ya mtu 1 kati ya watu 6 duniani. Kwa ujumla, zaidi ya lugha na lahaja 1,000 zinazungumzwa katika nchi hiyo yenye watu wa aina mbalimbali. Wengi wa watu ni Wahindu, asilimia 83 kati yao, Waislamu wakiwa asilimia 11, huku Wasikh, Wabuddha, Wajaini, na wanaojiita Wakristo wakifanyiza sehemu iliyobaki.

Katika miaka ya majuzi Mashahidi wa Yehova wamefurahia fanaka yenye kutokeza katika India. Wamepata watu wenye mfano wa kondoo wanaotaka kuchukua msimamo imara upande wa Ufalme wa Yehova, ijapokuwa namna zote za mikazo na upinzani.

Kwa kielelezo, msichana mmoja kutoka kwa familia yenye kufuata Uhindu wa kawaida alikuwa amelemaa kwa ugonjwa wa kupooza tangu utotoni. Maumivu aliyopata yalimfanya afikiri juu ya Mungu na kusudi la maisha. Alitafuta jibu katika dini nyingi lakini hakupata kitulizo. Tokeo likawa kwamba alipoteza imani yake katika dini, ingawa si katika Mungu.

Karibu na pindi hiyo Mashahidi wawili wakiwa katika huduma yao ya nyumba kwa nyumba walimkuta msichana huyo. “Nilisukumwa moyoni hadi kutokwa machozi niliposikia wakisoma Ufunuo 21:4,” yeye akumbuka. Alichukua vichapo vingi vya Watch Tower Society na kukubali funzo la Biblia nyumbani ujapokuwa upinzani wa mama yake. Msichana huyo alifanya mabadiliko mengi maishani mwake, kwa ujasiri akakabili upinzani kutoka kwa watu wa ukoo, akawa Shahidi aliyebatizwa. Yeye asema: “Nimetoka mbali sana, na mwendo umekuwa mgumu sana. Lakini Yehova Mungu amekuwa nami sikuzote na kunipa shangwe na amani nyingi sana.”

Imara kwa Ajili ya Ibada Safi Shuleni

Dada mchanga aliambiwa na mwalimu wake aende kwenye kanisa Katoliki pamoja na wanadarasa wenzake. Dada huyo kwa upole akakataa, akisema kwamba yeye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova naye hawezi kuabudu yeyote au chochote isipokuwa Yehova. Mwalimu akasema kwamba wengine wote waendapo kanisani, ni lazima dada huyu aende pia. Lakini dada huyo alisimama imara na kusema kwamba kwa kuwa wale wanaoenda kwenye kanisa hilo hawamwombi Yehova, hakuona jinsi angekuwa mhudhuriaji huko.

Kwa sababu ya uimara wa msichana huyo, mwalimu wake alitaka kujua mengi juu ya itikadi yake. Hivyo siku iliyofuata dada huyo akampa nakala ya Mnara wa Mlinzi iliyozungumza juu ya ibada ya Yehova. Kwa kuvutiwa na yale aliyokuwa amesoma, mwalimu huyo akamwondoa msichana huyo kutoka kwenye utendaji wote wa kidini shuleni. Dada huyo aliweza kumwangushia magazeti kumi pamoja na walimu wengineo.

Utii kwa Sheria ya Mungu Juu ya Damu Wathawabishwa

Majuzi homa iletwayo na virusi ilizuka na kuenea sana katika sehemu fulani za jimbo la Kerala. Ugonjwa huo huharibu figo vibaya sana na hutokeza uhitaji wa utibabu aina ya dialisisi. Mara nyingi utiaji-damu mishipani hutumiwa. Katika jiji moja watu 14 walilazwa hospitalini wakiugua maradhi hayo. Mmoja wa wagonjwa hao alikuwa Shahidi, mzee katika kutaniko la hapo. Aliambiwa kwamba utiaji-damu mishipani ndio tiba pekee iliyopatikana. Mzee huyo akaeleza itikadi zake za Kimaandiko na kukataa damu kabisa. (Matendo 15:28, 29) Baada ya bishano kubwa madaktari walisema kwamba angekufa kwa sababu ya kukataa kwake utiaji-damu mishipani.

Wagonjwa wale wengine 13 wakatiwa damu. Kwa kusikitisha, wote wakafa baada ya siku chache. Ndugu huyo ndiye aliyekuwa mwokokaji pekee! Wakuu wa hospitali walishangaa sana. Wafanyakazi wa tiba walivutiwa sana na ziara za kawaida zilizofanywa na washiriki wa kutaniko. Baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali, ndugu huyo akaenda kuwashukuru madaktari, lakini walisema hivi: “Kwa nini utushukuru? Shukuru Mungu wako, Yehova. Ndiye aliyekuokoa. Tafadhali utuombee pia kwa Mungu wako, Yehova.”

[Sanduku katika ukurasa wa 24]

HABARI ZA NCHI

Mwaka wa Utumishi wa 1994

KILELE CHA WANAOTOA USHAHIDI: 14,271

UWIANO: Shahidi 1 kwa watu 65,266

HUDHURIO LA UKUMBUSHO: 38,192

WASTANI WA WAHUBIRI WALIO MAPAINIA: 1,780

WASTANI WA MAFUNZO YA BIBLIA: 12,453

IDADI YA WALIOBATIZWA: 1,312

IDADI YA MAKUTANIKO: 410

OFISI YA TAWI: LONAVLA

[Picha katika ukurasa wa25]

Ofisi ya Tawi, Lonavla

[Picha katika ukurasa wa25]

Kutoa ushahidi kuhusiana na mkusanyiko wa “Habari Njema za Milele” katika 1963

[Picha katika ukurasa wa25]

Kumhubiria mchuuzi nje ya Red Fort katika Delhi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki