Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 10/1 kur. 5-7
  • Ulimwengu Usio na Vita—Lini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ulimwengu Usio na Vita—Lini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Dini—Kizuizi Kikubwa
  • Wakati Ujao wa Dini
  • Hali ya Binadamu ya Kutokamilika
  • Yesu Kristo—Mwana-Mfalme wa Amani
  • Mfalme Apigana Penye Har-Magedoni
    “Ufalme Wako Uje”
  • Je! Sanamu Inaweza Kuleta Amani na Usalama?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Amani na Usalama Kutoka Chanzo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Umoja wa Mataifa—Rafiki au Adui ya Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 10/1 kur. 5-7

Ulimwengu Usio na Vita—Lini?

KATIBA ya Umoja wa Mataifa ilianzishwa katika Oktoba 24, 1945. Ndio mpango bora zaidi wa amani ya ulimwengu uliowahi kufanywa na wanadamu. Likiwa na Mataifa 51 yaliyo washirika, Umoja wa Mataifa ndilo shirika kubwa zaidi la kimataifa katika historia ya ulimwengu. Pia, kwa mara ya kwanza kabisa, shirika la kimataifa lingeweza kuwa na jeshi la kuhifadhi amani na usalama na kuleta ulimwengu usio na vita.

Leo, Umoja wa Mataifa ukiwa na Mataifa 185 yaliyo washirika, ni wenye nguvu kuliko wakati mwingine wowote. Kwa nini basi, shirika la kimataifa lenye nguvu zaidi katika historia lishindwe kutimiza makusudio yalo mazuri kwa ukamili?

Dini—Kizuizi Kikubwa

Tatizo moja kubwa ni fungu la dini katika mambo ya ulimwengu. Kweli, tangu Umoja wa Mataifa ulipoanzishwa, dini zilizo kubwa katika ulimwengu zimeapa kutegemeza tengenezo hilo. Akirejezea mwaka wao wa 50, Papa John Paul 2 alizungumza juu ya Umoja wa Mataifa kuwa “kifaa bora kabisa cha kuleta na kuhifadhi amani.” Maneno yake yanashirikiwa na jumuiya ya viongozi wa kidini ya ulimwengu wote. Lakini uhusiano huu wa kisiri kati ya dini na serikali hauwezi kufunika uhakika wa kwamba dini imekuwa kizuizi na kipingamizi kwa Umoja wa Mataifa.

Kwa karne nyingi dini imekuwa na fungu kubwa katika kuendeleza au kuunga mkono chuki, vita, na mauaji ya kimataifa. Katika miaka ya majuzi, wakijisitiri kwa dini, majirani wameuana. Usemi “utakaso wa kikabila” umetumiwa sana kuhusiana na vita katika Balkani. Hata hivyo, chuki yenye jeuri ambayo wengi wanayo huko kuelekeana inahusu uhusiano katika dini wala si jamii, kwa kuwa wengi wao wametokana na jamii moja. Ndiyo, ni lazima dini ikubali sehemu kubwa iliyoshiriki katika umwagaji wa damu katika ile iliyokuwa Yugoslavia, na Umoja wa Mataifa haujaweza kuukomesha.

Kwa kufaa, profesa mmoja wa chuo wa mambo ya dini hivi majuzi alisema “katika ulimwengu wa baada ya vita baridi wenye uharamia wa kidini unaoongezeka, uchunguzi wa dini na machinjo ya jamii nzima-nzima huenda ukawa mojapo mambo ya kutangulizwa zaidi, bila kujali uchunguzi huo unafunua nini.” Utambuzi mpya wa jinsi dini inavyozuia jitihada za amani ya ulimwengu ni dhahiri leo.

Tangazo la UM la 1981 lilisema: “Hangaiko la ukosefu wa uvumilivu na kuwapo kwa ubaguzi katika mambo ya dini au itikadi zilizo dhahiri katika sehemu fulani za ulimwengu, Azimio la kuchukua hatua zozote zinazotakikana ili kumaliza ukosefu wa uvumilivu katika kila hali na kupigana na ubaguzi wa kidini na itikadi.”

Kwa kupatana na tangazo lao, Umoja wa Mataifa umetangaza 1995 kuwa Mwaka wa Kuachilia. Lakini je, kweli itawezekana wakati wowote kupata amani na usalama katika ulimwengu uliogawanywa na dini?

Wakati Ujao wa Dini

Unabii katika kitabu cha Biblia cha Ufunuo unatoa jibu. Unaeleza juu ya “kahaba mkuu” wa ufananisho anayeketi kama “malkia” na ana “ufalme juu ya wafalme wa nchi.” Kahaba huyo anaishi kwa “anasa” naye amezini na serikali za ulimwengu. Serikali hizi zinafananishwa na “mnyama mwekundu sana,” ambaye kahaba huyo amemkalia kwa starehe. (Ufunuo 17:1-5, 18; 18:7) Akiitwa “Babiloni Mkubwa,” (New World Translation) mwanamke huyo asiye na adili na mwenye nguvu nyingi anaitwa kwa jina la Babiloni ya kale, kile chanzo cha dini ya ibada ya sanamu. Kwa kufaa, kahaba huyo leo anafananisha dini zote za ulimwengu, ambazo zimejiingiza katika mambo ya serikali.

Simulizi hilo laendelea kusema kwamba, baada ya muda, Mungu atatia ndani ya mioyo ya sehemu za kijeshi za hayawani-mwitu huyo ili zichukue hatua. Hizo ‘zitamchukia yule kahaba, nazo zitamfanya awe mkiwa na uchi, zitamla nyama yake, zitamteketeza kabisa kwa moto.’ (Ufunuo 17:16)a Hivyo Yehova Mungu mwenyewe atakuwa amechukua hatua kwa kuchochea mataifa yenye nguvu yafanye kampeni ya kuondoa dini bandia. Mfumo wa ulimwengu wote wa kidini, kutia ndani mahekalu na sehemu zao za ibada zenye anasa, zitaharibiwa kabisa. Sasa dini haitazuia amani na usalama. Lakini hata hivyo je, kutakuwa na amani na usalama wa kweli duniani?

Hali ya Binadamu ya Kutokamilika

Je, kuna uhakikisho wowote kwamba kuondolea mbali kwa dini kutaongoza kwenye ulimwengu usio na vita? La. Umoja wa Mataifa utaendelea kukabili hali ya kutatanisha. Kwa upande mmoja, watu wanataka amani na usalama. Hata hivyo, kwa upande mwingine, ni watu wanaotatiza kabisa amani na usalama. Chuki, kiburi, majisifu, ubinafsi, na upumbavu ndizo hali za binadamu zinazosababisha magombano yote na vita vyote.—Yakobo 4:1-4.

Biblia ilitabiri kwamba katika siku yetu watu wangekuwa “wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna.”—2 Timotheo 3:1-4.

Katibu-Mkuu Boutros Boutros-Ghali alikiri kwamba “ulimwengu unaugua kutokana na mzoroto wa kijamii na kiadili ambao katika jamii nyingi, ni mbaya sana.” Hakuna njia zozote ziwezazo kumaliza vitabia vyenye kudhuru vya hali ya binadamu ya kutokamilika.—Linganisha Mwanzo 8:21; Yeremia 17:9.

Yesu Kristo—Mwana-Mfalme wa Amani

Kwa wazi, Umoja wa Mataifa hauna uwezo wa kuleta amani ulimwenguni. Washiriki na wategemezaji wao wote ni binadamu wasiokamilika, wajapokuwa na miradi ya juu. Biblia husema kwamba “njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” (Yeremia 10:23) Zaidi ya hayo, Mungu aonya hivi: “Msiwatumainie wakuu, wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.”—Zaburi 146:3.

Biblia hutabiri yale Yehova atakayotimiza kupitia Mwanaye, “Mwana-Mfalme wa Amani.” Isaya 9:6, 7, lasema: “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, [“Mwana-Mfalme wa amani,” NW]. Maongeo ya enzi yake na amani hayatakuwa na mwisho.”

Mataifa ya ulimwengu yamechoshwa na miaka 50 ya jitihada zilizovurugika. Hivi karibuni yataharibu mashirika ya kidini yanayofananishwa na kahaba. Kisha Yesu Kristo, yule “Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana,” na jeshi lake la kimbingu ataangamiza serikali zote za binadamu na kuwaua wote wanaokataa enzi kuu ya Mungu. (Ufunuo 19:11-21; linganisha Danieli 2:44.) Kwa njia hiyo Yehova Mungu ataleta ulimwengu usio na vita.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa somo lenye kina la unabii wa Ufunuo kuhusu Babiloni Mkubwa, ona sura 33 hadi 37 za kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, kilichotangazwa katika 1988 na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

MAONI YA MKRISTO KUELEKEA UMOJA WA MATAIFA

Katika unabii wa Biblia, serikali za binadamu hufananishwa na hayawani-mwitu. (Danieli 7:6, 12, 23; 8:20-22) Hivyo, kwa miongo mingi gazeti la Mnara wa Mlinzi limeshirikisha hayawani-mwitu wa Ufunuo sura za 13 na 17 na serikali za ulimwengu za leo. Hilo latia ndani Umoja wa Mataifa, ambao katika Ufunuo sura ya 17 unafananishwa na hayawani mwekundu sana mwenye vichwa saba na pembe kumi.

Hata hivyo, utambulisho huo wa Kimaandiko haupendekezi kutoheshimu kwa njia yoyote serikali au wakuu wazo. Biblia yaeleza waziwazi hivi: “Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo imeamriwa na Mungu. Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.”—Warumi 13:1, 2.

Kupatana na hilo, Mashahidi wa Yehova, wanaodumisha kutokuwamo kabisa katika siasa hawaingilii mambo ya serikali za binadamu. Kamwe hawachochei mapinduzi au kushiriki katika matendo ya raia ya kutotii. Badala ya hivyo, wanatambua kwamba serikali ya aina fulani ni ya lazima ili kudumisha sheria na utaratibu katika jamii ya kibinadamu.—Warumi 13:1-7; Tito 3:1.

Mashahidi wa Yehova huona tengenezo la Umoja wa Mataifa kama waonavyo mashirika yale mengine ya serikali za ulimwengu. Wao hutambua kwamba Umoja wa Mataifa unaendelea kuwapo kwa ruhusa ya Mungu. Kulingana na Biblia, Mashahidi wa Yehova huonyesha serikali zote heshima istahiliyo na kuzitii ikiwa utii huo hauwalazimishi kufanya dhambi dhidi ya Mungu.—Matendo 5:29.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki