Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 12/1 kur. 24-27
  • Kitovu cha Kielimu cha Watchtower Chatuma Wamishonari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitovu cha Kielimu cha Watchtower Chatuma Wamishonari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Shauri kwa Darasa Lenye Kuhitimu
  • Kupata Kujua Hilo Darasa Vizuri Zaidi
  • Makao Mapya kwa Ajili ya Shule ya Umisionari ya Gileadi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Shule ya Gileadi—Ina Umri wa Miaka 50 na Yaendelea Kufanikiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Shule ya Gileadi Yatuma Darasa Layo la 100
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Wanafunzi Wenye Kuhitimu wa Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 12/1 kur. 24-27

Kitovu cha Kielimu cha Watchtower Chatuma Wamishonari

SHULE ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower imekuwa na madarasa katika sehemu mbalimbali. Kati ya 1943 na 1960, katika majengo ya South Lansing, New York, Marekani, madarasa 35, yenye wanafunzi kutoka nchi 95, yalipokea mazoezi ya kipekee. Kisha shule hiyo ikahamia makao makuu ya ulimwengu katika Brooklyn, New York, ambapo iliendeshwa kwa karibu miaka 28. Tangu 1988 hadi karibu 1995, Shule ya Gileadi ilifanywa katika Wallkill, New York.

Katika miaka hiyo shule hiyo ilipanua nyanja zayo za utendaji. Chini ya mwongozo wayo, mtaala wa mafundisho wa majuma kumi ulitolewa kwa madarasa matatu katika Mexico; madarasa matano kama hayo yalifanyiwa katika Ujerumani; mawili katika India. Tangu 1987 shule nyingine ya ziada iitwayo Shule ya Mazoezi ya Kihuduma imekuwa na madarasa katika nchi 34, ikiandaa majuma nane ya kipekee ya mtaala wa kuzoeza wanaume vijana wanaostahili. Hata hivyo, mafundisho yaliyopewa darasa la 99 la Gileadi, kwenye Kitovu cha Kielimu cha Watchtower katika Patterson, New York, yalikuwa mtaala wa majuma 20, uliotia ndani somo la kina kirefu la Biblia nzima, mazungumzo ya historia ya kisasa na tengenezo la Mashahidi wa Yehova, na vilevile mashauri mengi juu ya kazi ya mishonari katika nchi za kigeni.

Katika Septemba 2, darasa hilo la 99 lilihitimu. Programu ya kuhitimu iliyochukua muda wa saa tatu ilifanywa katika jumba jipya kwenye Kitovu cha Kielimu cha Watchtower. Lilijaa kabisa. Wasikilizaji wengine zaidi waliokuwa kwenye majengo ya Betheli katika Patterson, Wallkill, na katika Brooklyn waliunganishwa kwa waya za elektroni. Hiyo ilikuwa siku ya kusisimua si kwa darasa lenye kuhitimu pamoja na watu wao wa ukoo na marafiki wa karibu tu bali pia kwa mamia ya wajitoleaji waliokuwa wameshiriki wakiwa wajitoleaji katika kujenga majengo mazuri mapya ya shule.

Katika maelezo yake ya kufungua, Carey Barber wa Baraza Linaloongoza alikazia fikira kwenye umaana wa mambo yaliyokuwa yakitendeka. Yeye alisema: “Hiki ndicho kitakuwa kitovu cha utendaji mkubwa kabisa wa elimu ya kimungu ambayo imepata kuendelezwa katika dunia hii.” Alieleza kwamba tunakaribia upeo wa vita kati ya mbegu ya mwanamke na mbegu ya nyoka. (Mwanzo 3:15) Alionyesha kwamba wale tu watakaookoka huo mkabiliano wenye kutisha sana wakati wa dhiki kuu inayokuja, watakuwa wale wenye ujuzi sahihi wa Neno la Mungu na wanaoutii.

“Programu yetu ya kielimu ya wakati huu,” yeye akatangaza, “imekusudiwa kuleta watu wote wa Yehova kila mahali kwenye ile hali bora ya ukomavu inayofafanuliwa kwenye Mithali 1:1-4—ile ya kupata kujua hekima na nidhamu, kuweza kutambua uelewevu, kupokea nidhamu itoayo ufahamu wenye kina, uadilifu, hukumu, unyoofu, na uwezo wa kufikiri.” Ni ulinzi salama ulioje kuwa na mali kama hizo za kiroho!

Shauri kwa Darasa Lenye Kuhitimu

Maelezo hayo ya utangulizi yalifuatwa na mfululizo wa hotuba tano fupi zilizoelekezewa darasa lenye kuhitimu. Harold Jackson, aliyekuwa zamani mfunzi wa Gileadi na ambaye sasa ni mshiriki wa wafanyakazi wa makao makuu katika Brooklyn, alilisihi darasa akisema, “Shikeni Sana Uradhi Wenu wa Kimungu.” Lloyd Barry, mishonari wa muda mrefu na sasa akiwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza, alizungumza juu ya “Kumtumikia Yehova kwa Unyenyekevu.” Alieleza kwamba sifa hii ingekuwa ya muhimu kwa wahitimu wanapojipatanisha na hali mpya na vilevile katika uhusiano wao na wamishonari wenzao, katika makutaniko ambayo wangetumikia, na pamoja na watu wa mahali waendapo.

Karl Adams, anayetumikia sasa katika ufundishaji wa Gileadi, alisababu pamoja na hilo darasa juu ya swali “Imani Itakuongoza Kufanya Nini?” Aliwatia moyo wasiwe kama wale Waisraeli waliolalamika kuhusu hali zilizokuwa jangwani wakitamani kurudi Misri lakini, badala ya hilo, wawe kama Abrahamu, aliyeutazamia Ufalme wa Mungu kuwa suluhisho la matatizo badala ya kurudi Uru wa Wakaldayo. (Kutoka 16:2, 3; Waebrania 11:10, 15, 16) Ulysses Glass, msajili wa shule, alielekeza fikira kwenye ono la Asafu kama lilivyorekodiwa katika Zaburi 73 ili kuonya kwa upole darasa lenye kuhitimu, “Fikirieni Baraka Zenu.” Naye Albert Schroeder, mshiriki wa Halmashauri ya Ufundishaji ya Baraza Linaloongoza, alizungumza juu ya kichwa hiki “Yehova Huandaa.” Alitaja Shule ya Gileadi yenyewe na fungu layo katika kutimiza kazi kubwa ya kuhubiri na kufanya wanafunzi kuwa uthibitisho wa uandalizi kama huo.

Baadaye wasikilizaji walisikiliza kwa makini sana wakati Milton Henschel, msimamizi wa Watch Tower Society, alipozungumza juu ya “Viungo Ambavyo Kila Kimoja Ni Mali ya Kile Kingine.” Alisoma na akatoa maelezo kwa urefu sana juu ya Warumi sura ya 12. Miongoni mwa mambo mengine, alisema: “Ni lazima tukumbuke kwamba tuna uhusiano wa karibu sana pamoja na watumishi wenzetu kutanikoni.” Aliongezea hivi: “Ni vizuri sikuzote tufikiriane kuwa mali ya Yehova, na badala ya kuwa wenye uchambuzi, badala ya kutafuta kosa, acheni tuwe wenye kusaidia sikuzote. Tunajifaidi tudumishapo muungano wa kiroho wa kutaniko la Kikristo.” Alionyesha jinsi roho ya kusaidiana kama hiyo ingeweza kudhihirishwa katika kuandaa chakula katika makao ya mishonari, kwa kufikiria hali ya kwamba huenda si kila mtu anaweza kula chakula kilekile. Pia aliwatia moyo wawe wenye kusaidia badala ya kuchambua washirikipo katika utumishi wa shambani pamoja na Wakristo wenzi ambao wana vichache sana kimwili. Ikiwa sisi ni wenye kusaidia, wenye kujengana, na wenye kutiana moyo kwelikweli, Ndugu Henschel akaeleza, “Yehova atatupenda kwa ajili ya hilo.” Hilo ni onyo la upole lililo zuri kama nini kwa wamishonari ambao karibuni watakuwa wakitumikia katika nchi zilizo tofauti katika hali nyingi na walizokuwa wakiacha!

Kupata Kujua Hilo Darasa Vizuri Zaidi

Hao wanafunzi 48 wa darasa la 99, walikuwa na umri wa miaka 32 kwa wastani nao tayari walikuwa wametumia zaidi ya miaka 11 kwenye utumishi wa wakati wote.

Mahojiano yaliyokuwa sehemu ya programu ya kuhitimu yaliwapa wasikilizaji fursa ya kupata kuwajua wachache wao. Nikki Liebl, kutoka Marekani, na Simon Bolton, kutoka Uingereza, walisimulia matukio yaliyokuwa yamejaribu imani yao kwamba Yehova angeandaa mahitaji yao ya kimwili. Kwa kweli waliona utunzaji wa Yehova walipoweka utumishi wa wakati wote mahali pa kwanza.

Isabelle Kazan, ambaye lugha yake ni Kifaransa, alisema kwamba alikuwa amejifunza Kiarabu ili awatolee ushahidi Waarabu waliokuwa wakiishi Ufaransa. Alipoanza katika 1987, kile kikundi kidogo katika Paris kilikuwa na ndugu wanne tu wenye kusema Kiarabu, kutia ndani yeye na dada mwingine waliokuwa wakijifunza lugha hiyo. (Haikuwa rahisi. Walikuwa wakitumia muda wa saa nane katika kutayarisha somo lao la Mnara wa Mlinzi kila juma ili waweze kutoa maelezo.) Je, jitihada hizo zilistahili? Leo, kuna Mashahidi wanaosema Kiarabu waliopangwa kitengenezo katika mizunguko mitano katika Ufaransa yote. Mwanafunzi mwingine, Miko Puro, alieleza jinsi Kifaransa alichokuwa amejifunza shuleni kilivyomsaidia kuwahubiria wakimbizi Waafrika waliokuwa Finland, nacho kitamsaidia sana katika mgawo wake wa mishonari katika Benin. Bonny Bowes alikumbuka jitihada yake ya kuzungumza Kifaransa vizuri ili aweze kutumikia kwa mafanikio katika Quebec, Kanada. Na Bjarki Rasmussen, kutoka Denmark, alieleza mambo waliyoona yeye na mkeye wakati wa miaka ya utumishi katika Visiwa vya Faeroe. Ndiyo, wamishonari hawa wapya ni watumishi wa wakati wote wenye uzoefu.

Wahitimu hao walipewa mgawo wa kwenda nchi 19—katika Afrika, Amerika ya Kati na ya Kusini, Ulaya Mashariki, na sehemu za Mashariki. Wahitimu wa madarasa ya awali tayari wametumika katika zaidi ya nchi 200. Wengi wa wahitimu hao bado wana shughuli nyingi katika migawo yao. Hawa wamishonari wapya wanajiunga nao sasa katika kupanua zaidi ushahidi wa Ufalme mpaka miisho ya dunia.—Matendo 1:8.

[Picha katika ukurasa w25]

Mandhari za darasa kwenye Kitovu cha Kielimu cha Watchtower

[Picha katika ukurasa wa26]

Darasa Lenye Kuhitimu la 99 la Watchtower Bible School of Gilead

Katika orodha iliyoko chini, safu zimeratibiwa kutoka mbele kuelekea nyuma, na majina yameorodheshwa kuanzia kushoto kuelekea kulia kwa kila safu.

(1) Heffey, S.; Riley, E.; Mortensen, D.; Honable, A.; Bolton, J.; Poole, J.; Siimes, G.; Sousa, L. (2) Pashnitski, B.; Shepherd, D.; Pashnitski, W.; Järvinen, J.; Paulsen, K.; Rasmussen, E.; Schewe, C.; Olsson, L. (3) Paulsen, E.; Samsel, T.; Bowes, B.; Harris, E.; Kazan, I.; Liebl, N.; Sousa, P.; Puro, J. (4) Lager, K.; Lager, V.; Golden, K.; Bolton, S.; Johnson, M.; Johnson, S.; Liebl, A.; Rasmussen, B. (5) Harris, D.; Samsel, W.; Schewe, O.; Heffey, R.; Kazan, L.; Riley, T.; Järvinen, O.; Puro, M. (6) Mortensen, D.; Golden, R.; Honable, L.; Shepherd, M.; Bowes, R.; Siimes, T.; Poole, E.; Olsson, J.

[Picha katika ukurasa wa27]

Wakiwa bado katika migawo yao: (kushoto) Charles Leathco pamoja na mkeye, Fern, katika Brazili, wahitimu wa darasa la kwanza na la sita la Gileadi; (chini) Martha Hess, katika Japani, wahitimu wa darasa la saba la Gileadi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki