Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp19 Na. 2 kur. 4-5
  • Janga la Asili Linapotokea

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Janga la Asili Linapotokea
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUJUA KWELI YA BIBLIA HUTUSAIDIA TUSIKATE TAMAA
  • Je, Umejitayarisha?
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Mtupie Yehova Mahangaiko Yako Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Mfadhaiko Utakoma
    Amkeni!—2001
  • Jinsi ya Kukabiliana na Mahangaiko kwa Mafanikio
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
wp19 Na. 2 kur. 4-5
Wanaume wawili wameketi kwenye mabaki ya jengo lililoporomoka

Janga la Asili Linapotokea

“Tulivunjika moyo kabisa. Maporomoko ya ardhi na mafuriko yaliharibu kila kitu tulichokuwa nacho.”—Andrew, Sierra Leone.

“Baada ya kimbunga, tulirudi kwenye nyumba yetu. Kila kitu kilikuwa kimeharibiwa. Tulipigwa na butwaa. Binti yangu alijitupa chini na kuanza kulia kwa uchungu.”—David, Visiwa vya Virgin.

IKIWA umewahi kukumbwa na janga la asili, basi unaelewa jinsi ambavyo watu huhisi baada ya matukio hayo. Wengi hushtuka sana, huhisi kana kwamba wanachoona si halisi, huchanganyikiwa, huwa na wasiwasi, na kuota ndoto zenye kushtua. Vilevile, baadhi yao huchoka sana na kuvunjika moyo hivi kwamba hawatamani tena kuendelea kuishi.

Ikiwa janga la asili limesababisha upoteze kila kitu, huenda wewe pia ukahisi umeishiwa nguvu za kusonga mbele. Hata unaweza kuanza kuhisi huna sababu ya kuendelea kuishi. Hata hivyo, Biblia inaeleza sababu za kutokata tamaa, na inaweza kukupatia tumaini halisi la maisha mazuri wakati ujao.

KUJUA KWELI YA BIBLIA HUTUSAIDIA TUSIKATE TAMAA

Andiko la Mhubiri 7:8 linasema: “Ni afadhali mwisho wa jambo kuliko mwanzo wake.” Baada tu ya janga kutokea, huenda ukahisi maisha hayana maana yoyote. Lakini unapoanza kujijenga upya hatua kwa hatua, hali inaweza kubadilika na kuwa nzuri.

Kulingana na Biblia, wakati utafika ambapo “sauti ya kulia na ya maombolezo . . . haitasikika tena.” (Isaya 65:19) Hali itakuwa hivyo baada ya dunia kugeuzwa kuwa paradiso, Ufalme wa Mungu utakapokuwa ukitawala. (Zaburi 37:11, 29) Majanga ya asili yatakuwa historia tu. Kumbukumbu zote mbaya na hisia zenye kuumiza zitafutwa kwa sababu Mungu Mweza Yote anaahidi hivi: “Mambo ya zamani hayataingia tena akilini, wala hayataingia tena moyoni.”​—Isaya 65:17.

Hebu wazia jambo hili: Muumba anataka ‘kukupatia wakati ujao na tumaini’—maisha matulivu chini ya utawala bora wa Mungu. (Yeremia 29:11) Je, kujua ukweli huo kunaweza kukusaidia kuona umaana wa kuendelea kuishi? Sally, aliyenukuliwa kwenye makala iliyotangulia, anasema: “Kujikumbusha kuhusu mambo yote mazuri ambayo Ufalme wa Mungu utatufanyia wakati ujao kunaweza kukusaidia usihangaishwe sana na mambo yaliyotokea, na kukupa nguvu za kupambana na hali unazokabili sasa.”

Kwa nini usijifunze zaidi kuhusu mambo ambayo Ufalme wa Mungu utawafanyia wanadamu hivi karibuni? Ukifanya hivyo utakuwa na uhakika kwamba, licha ya hali iliyokupata, una sababu za kuendelea kuishi huku ukisubiri kwa hamu hali nzuri wakati ujao. Kwa sasa, Biblia inatoa mwongozo unaoweza kukusaidia kushughulika na changamoto zinazotokana na janga. Hebu tuchunguze mifano kadhaa.

Maandiko Yanayoweza Kukusaidia

Pumzika vya kutosha.

“Ni afadhali konzi moja ya pumziko kuliko konzi mbili za kazi ngumu na kukimbiza upepo.”​—Mhubiri 4:6.

Watafiti wanasema kwamba, baada ya kupatwa na tukio linaloshtua sana, “kutolala vizuri . . . kunaweza kuzidisha madhara ya kimwili yaliyosababishwa na mshtuko, na kufanya iwe vigumu kwa mtu kudumisha usawaziko wa kihisia.” Hivyo, ni muhimu kupumzika vya kutosha.

Eleza jinsi unavyohisi.

“Mahangaiko yaliyo moyoni mwa mtu huulemea moyo [au, “humfanya ashuke moyo,” maelezo ya chini], lakini neno jema huuchangamsha.”​—Methali 12:25.

Zungumza na mshiriki wa familia au rafiki unayemwamini. Atakusikiliza unapoeleza hisia zako. Na si hilo tu, anaweza kukutia moyo na kukupatia msaada unaohitaji.a

Fikiria hali nzuri za wakati ujao.

“Kulingana na ahadi yake [Mungu] tunangojea mbingu mpya na dunia mpya, na humo uadilifu utakaa.”​—2 Petro 3:13.

a Mtu ambaye amekuwa na mkazo kwa muda mrefu au mahangaiko mengi sana moyoni, huenda akahitaji msaada wa daktari.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki