Kuabudu Yehova kwa Umoja
1 Mtunga zaburi alivuta vizuri hisia zetu kuhusu udugu wa ulimwenguni pote ukiabudu Yehova kwa umoja alipoandika: “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja.” (Zab. 133:1) Kwa kuendelea kukua katika maarifa sahihi ya ukweli na kuchochewa kuutumia katika maisha yetu ya kila siku, sisi sote tunadumisha “akili ile ile na mstari ule ule wa wazo” (1 Kor. 1:10, NW) Umoja miongoni mwetu umezidishwa katika miaka ya karibuni kupitia utumizi wa kitabu Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa pekee wa Kweli, kilichotolewa kwenye “Umoja wa Ufalme” Mikusanyiko ya Wilaya katika 1983. Tunapaswa kuthamini kichapo hiki chenye kutokeza hata zaidi tunapojifunza hicho tena kwenye Funzo la Kitabu la Kundi kuanzia Agosti.
2 Wote watanufaika, tuwe tulikuwa katika kundi wakati kitabu hicho kilidarisiwa mwanzoni au tuwe miongoni mwa maelfu ya wapya ambao wameingia katika ukweli tangu kitabu Wenye Umoja Katika Ibada kiliposomwa mara ya mwisho kwenye Funzo la Kitabu la Kundi. Wapya watanufaika kutokana na maelezo mbalimbali na matumizi yanayotolewa na waabudu wenzi waliokomaa. Matumizi ya mahali penu ya habari hiyo na kukaziwa kwa mambo makuu na viongozi wenye ujuzi bila shaka kutagusa maeneo ya maisha yetu ya kibinafsi na huduma ambayo huhitaji kuelekezewa fikira zaidi. Kwa kuwa hakuna mmoja wetu aliyemo katika hali alizokuwamo wakati tulipojifunza kitabu hicho wakati uliopita, kupitia habari na kutumia shauri katika kitabu Wenye Umoja Katika Ibada kama linavyohusiana na matatizo na mikazo tunayokabili leo, kutatutia nguvu tunapoendelea ‘kuishindania imani.’—Yuda 3.
3 Zaidi ya kuwa na shauri timamu ambalo ni lenye kutia moyo na lenye kumotisha, kitabu cha Wenye Umoja Katika Ibada kinaamsha tamaa yetu kwa ajili ya maarifa ya kiroho. Nguvu zetu za kusababu zinatiwa nguvu kwa njia ambayo habari inatolewa. Maswali yaliyo chini ya ukurasa, pia maswali na maandiko yaliyo katika mafungu fulani fulani, yanahitaji kufikiri sana na kuyatumia kibinafsi kwa upande wetu ikiwa tutafyonza maana kamili ya habari hiyo. Kujifunza kitabu hiki kunatusaidia kukuza uwezo wa kufikiri na kufanyia maendeleo utambuzi wetu wa mambo ya kiroho. Tunasaidiwa kuuona ukweli katika pande nyingi zao na kuchanganua si jinsi tu jambo moja linavyohusiana na jingine bali jinsi linavyotuhusu kibinafsi. (Mit. 1:1-5) Hii inatusaidia “kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi.”—Flp. 1:10, NW.
4 Jambo la maana kabisa katika kunufaika kikamili ni kujitayarisha kwa uangalifu. Ikiwa umejifunza habari hii wakati uliopita na umepiga majibu mstari katika kitabu chako, epuka kufikiri kwamba kujitayarisha kwa uangalifu kila juma hakutahitajiwa. Mara kwa mara sisi sote tunahitaji kuburudishwa akili na mambo haya ya kiroho. Mtume Petro alivuviwa kuwakumbusha ndugu kuhusu kweli za msingi ambazo walikuwa wamejifunza tayari. (2 Pet. 1:12, 13; 3:1) Paulo anatukumbusha sisi kwamba hayo ni kwa usalama wetu wa kiroho. (Flp 3:1) Kwa kuchunguza tena kitabu Wenye Umoja Katika Ibada, tutatiwa nguvu kuendelea kuwa na umoja katika ibada yetu ya Mungu wa pekee wa kweli Yehova katika siku hizi za mwisho zenye hatari.