Sanduku la Swali
● Je! ni jambo linalofaa ndugu aendeshe maziko ya mtu wa ulimwengu anayejulikana kuwa mhalifu mwenye sifa mbaya?
Maswali yanazuka mara kwa mara kuhusu kuendesha maziko ya mtu aliyekufa, kama yale ya mtu asiyeamini wa ukoo wa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, ambaye alishirikiana kidogo au hakushirikiana na Mashahidi wa Yehova. Maoni yenye usawaziko kuhusu kuongoza maziko ya mtu kama huyo yanatolewa katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Juni 1, 1977, kurasa 346-7.
Tukiombwa tuendeshe maziko ya mtu katika ulimwengu anayeonwa kuwa mtenda makosa mwenye sifa mbaya tunapaswa kukataa kwa sababu ingekuwa na sifa mbaya kwa Yehova na tengenezo lake.—Mit. 18:3.
Namna gani mtu ambaye hajajiweka wakfu na amejiingiza katika makosa wakati uliopita? Kuna tofauti kati ya mtu ambaye ameendelea kuishi maisha ya kutenda mabaya na mtu fulani ambaye wakati uliopita aliishi maisha yasiyo yenye kupendeza lakini ambaye alikuwa akigeuzwa kiroho na alikuwa akijitahidi kuvaa utu mpya. (Rum. 12:2; Efe. 4:17, 20-24) Huenda mtu huyo akawa bado si Mkristo aliyejiweka wakfu na kubatizwa mwenye kutembea kwa unyofu na ambaye amesafishwa. (1 Kor. 6:9-11; Ufu. 7:9, 10) Lakini huenda akawa alikuwa akichukua hatua za kugeuza maisha yake, na jambo hili linaweza kufikiriwa ombi likitolewa ili kushughulikia maziko yake. Wazee wakihisi kwamba halitaharibu amani na upatano wa kundi wala halitaletea watu wa Mungu suto, hakungekuwa na katazo mzee kutoa hotuba hiyo ikiwa dhamiri yake inamruhusu afanye hivyo.—1 Kor. 10:23, 24, 29, 32, 33.