Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/89 uku. 3
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Mazishi ya Kikristo Ni Yenye Heshima, Kiasi, na Yanampendeza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Maoni ya Mkristo Kuhusu Desturi za Mazishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 11/89 uku. 3

Sanduku la Swali

● Je! ni jambo linalofaa ndugu aendeshe maziko ya mtu wa ulimwengu anayejulikana kuwa mhalifu mwenye sifa mbaya?

Maswali yanazuka mara kwa mara kuhusu kuendesha maziko ya mtu aliyekufa, kama yale ya mtu asiyeamini wa ukoo wa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, ambaye alishirikiana kidogo au hakushirikiana na Mashahidi wa Yehova. Maoni yenye usawaziko kuhusu kuongoza maziko ya mtu kama huyo yanatolewa katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Juni 1, 1977, kurasa 346-7.

Tukiombwa tuendeshe maziko ya mtu katika ulimwengu anayeonwa kuwa mtenda makosa mwenye sifa mbaya tunapaswa kukataa kwa sababu ingekuwa na sifa mbaya kwa Yehova na tengenezo lake.—Mit. 18:3.

Namna gani mtu ambaye hajajiweka wakfu na amejiingiza katika makosa wakati uliopita? Kuna tofauti kati ya mtu ambaye ameendelea kuishi maisha ya kutenda mabaya na mtu fulani ambaye wakati uliopita aliishi maisha yasiyo yenye kupendeza lakini ambaye alikuwa akigeuzwa kiroho na alikuwa akijitahidi kuvaa utu mpya. (Rum. 12:2; Efe. 4:17, 20-24) Huenda mtu huyo akawa bado si Mkristo aliyejiweka wakfu na kubatizwa mwenye kutembea kwa unyofu na ambaye amesafishwa. (1 Kor. 6:9-11; Ufu. 7:9, 10) Lakini huenda akawa alikuwa akichukua hatua za kugeuza maisha yake, na jambo hili linaweza kufikiriwa ombi likitolewa ili kushughulikia maziko yake. Wazee wakihisi kwamba halitaharibu amani na upatano wa kundi wala halitaletea watu wa Mungu suto, hakungekuwa na katazo mzee kutoa hotuba hiyo ikiwa dhamiri yake inamruhusu afanye hivyo.—1 Kor. 10:23, 24, 29, 32, 33.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki