Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/97 uku. 7
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Mazishi ya Kikristo Ni Yenye Heshima, Kiasi, na Yanampendeza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Maoni ya Mkristo Kuhusu Desturi za Mazishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Mashahidi wa Yehova Wana Maoni Gani Kuhusu Mazishi?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 3/97 uku. 7

Sanduku La Swali

◼ Kutaniko linapoombwa kusaidia katika kupanga maziko, maswali yafuatayo hutokea:

Ni nani apaswaye kutoa hotuba ya maziko? Huu ni uamuzi wa kufanywa na washiriki wa familia. Huenda wakachagua ndugu aliyebatizwa mwenye msimamo mwema. Baraza la wazee likiombwa liandae msemaji, kwa kawaida watachagua mzee mwenye uwezo atoe hotuba yenye kutegemea muhtasari ya Sosaiti. Ijapokuwa hatutapitisha mpaka kwa kusifu-sifu aliyekufa, ingefaa kukazia sifa zenye kupendeza alizoonyesha.

Je, Jumba la Ufalme litumiwe? Laweza kutumiwa ikiwa ruhusa imetolewa na baraza la wazee. Jumba laweza kutumiwa ikiwa aliyekufa alikuwa na msimamo mzuri naye alikuwa mshiriki wa familia au mtoto mchanga wa mshiriki. Ikiwa mtu huyo alisababisha mwenendo usio wa Kikristo wenye sifa mbaya, au ikiwa kuna mambo mengine ambayo huenda yasipendeze kutaniko, wazee wanaweza kuamua kutoruhusu kutumiwa kwa jumba.—Ona kitabu Huduma Yetu, kurasa 62-63.

Kwa kawaida, Majumba ya Ufalme hayatumiwi kwa ajili ya maziko ya wasioamini. Tofauti pekee na hili iwezayo kufanywa ni ikiwa tu watu wa familia wabakio ni washiriki watendaji walio watangazaji waliobatizwa, aliyekufa alikuwa anajulikana na idadi ya kutosha ya watangazaji wa kutaniko kuwa alikuwa na mtazamo mzuri kuelekea kweli na alikuwa na sifa nzuri ya mwenendo mnyoofu katika jumuiya, na desturi za kilimwengu hazichanganywi na programu hiyo.

Vipi maziko kwa watu wa ulimwengu? Ikiwa aliyekufa alikuwa na sifa nzuri katika jumuiya, ndugu anaweza kutoa hotuba yenye kufariji ya Biblia kwenye nyumba ya maziko au kwenye makaburi. Kutaniko halitakubali kushughulikia maziko ya mtu aliyejulikana kuwa asiye na adili, mwenye mwenendo usiofaa au ambaye mtindo-maisha wake wote ulihitilafiana sana na kanuni za Biblia. Bila shaka ndugu hatashiriki pamoja na kasisi katika kufanya programu yenye mchangamano wa dini nyingi wala katika maziko yoyote yanayofanywa katika kanisa la Babiloni Mkubwa.

Vipi ikiwa aliyekufa alikuwa ametengwa na ushirika? Kwa ujumla kutaniko halitahusishwa. Jumba la Ufalme halitatumiwa. Ikiwa mtu alikuwa ameonyesha uthibitisho wa toba na alionyesha tamaa ya kurudishwa, huenda dhamiri ya ndugu ikamruhusu kutoa hotuba ya Biblia kwenye nyumba ya maziko au kwenye makaburi, ili kuwatolea wasioamini ushahidi na kuwafariji jamaa. Hata hivyo, kabla ya kufanya uamuzi huu, lingekuwa jambo la hekima ndugu kuwasiliana na baraza la wazee na afikirie yale ambayo wanaweza kupendekeza. Katika hali ambazo haingekuwa vizuri ndugu huyo kuhusishwa, huenda ikafaa ndugu ambaye ni mshiriki wa familia ya mtu aliyekufa kutoa hotuba kuwaliwaza jamaa wale.

Mwelekezo zaidi waweza kupatikana katika matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya Oktoba 15, 1990, kurasa 30-31; Januari 1, 1982, ukurasa 23; Novemba 15, 1980, kurasa 5-7; Juni 1, 1978, kurasa 5-8 (la Kiingereza); Novemba 1, 1977, kurasa 495-496; Machi 15, 1970, kurasa 191-192 (la Kiingereza); na Amkeni! la Mei 8, 1991, kurasa 22-23 na la Januari 8, 1979, kurasa 9-13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki