Kutangaza Habari Njema Tukiwa na Kitabu God’s Word
1 Katika barua yake kwa mwevanjeli mwenzake, mtume Paulo aliandika hivi: “Kila andiko limevuviwa na Mungu na ni lenye manufaa kwa ajili ya kufundisha, kwa ajili ya kukaripia, kwa ajili ya kufanya mambo yanyooke, kwa ajili ya kutia nidhamu katika uadilifu.”—2 Tim. 3:16, NW.
2 Tukiwa wapiga mbiu wa ki-siku-hizi wa habari njema, tunasadiki taarifa hii kwa moyo wetu wote. Tunakubali Biblia kuwa Neno la Mungu lililovuviwa. Tunakaribisha mwongozo wayo katika kila sehemu ya maisha yetu. (Zab. 119:105; Yn. 17:17) Lakini tunaweza kuwasaidiaje wengine wakubali Biblia kuwa Neno la Mungu na kutumia kanuni zayo katika maisha yao ya kila siku?
JINSI YA KUFANYA HIVYO
3 Tushirikipo katika ugawanyaji wa kwanza wa hadharani wa kitabu hiki kipya The Bible—God’s Word or Man’s? wakati wa mwezi wa Machi, tutakuwa tukisitawisha uhakika katika Biblia na kusaidia watu waone manufaa za kuishi kulingana na shauri layo lililovuviwa. Hilo litakuwa pendeleo lililoje!
4 Tunaweza kusema nini tunapotoa kitabu hiki? Baada ya salamu ya kirafiki, tunaweza kuelekeza fikira kwenye Mithali 14:12 ili kuonyesha kwamba maisha yenye kufanikiwa yanataka mwelekezo wa hekima. Mwelekezo wenye kosa waweza kuleta msiba. Halafu soma Mithali 2:6, 7 ili kuonyesha kwamba Yehova anaandaa hekima ya kweli. Tunaweza kusababu na mwenye nyumba kuhusu uhitaji wa kugeukia Biblia ili tupate hekima ya kimungu. Halafu tungeweza kusema: “Kichapo hiki kinaonyesha kwamba Biblia ni chanzo chenye kutegemeka cha shauri timamu juu ya matatizo wanayokabili watu. Tafadhali angalia yanayosemwa hapa katika fungu 2 kwenye ukurasa 5. [Soma fungu 2, na wakati ukiruhusu, soma fungu 4.] Kichapo hiki kitakusaidia uthamini kwamba Biblia kwa hakika ni Neno la Mungu na kwamba ndani yake mna mwongozo wenye manufaa katika mambo yote ya maisha. Kitabu hiki ni chako kwa mchango wa ____________ peke yake.”
5 Huenda mwenye nyumba akaonekana kuwa mwenye shughuli au akasema hapendezwi, akiwa hataki kujiingiza katika mazungumzo marefu. Ili kutoa utoaji mfupi, waweza kusema: “Bila shaka utakubali kuna matatizo mengi yanayokabili aina-binadamu.” Halafu soma fungu la utangulizi la sura 1. Baada ya mwenye nyumba kutoa maelezo juu ya swali la kumalizia katika fungu hilo, ungeweza kusema: “Biblia inatuambia kwamba karibuni sana sasa Mungu mwenyewe atasuluhisha matatizo yote yenye kutatanisha ya aina-binadamu. Kitabu hiki kinatoa ushuhuda wenye nguvu wa kuonyesha kwamba Biblia ni ya kweli, kwa kuwa hiyo ni Neno la Mungu na wala si la mwanadamu. Ningependa kiwe chako kwa mchango wa peke ____________ yake.”
KUJAZA UHITAJI
6 Kitabu hiki kipya, The Bible—God’s Word or Man’s?, kitawezesha wasomaji wenye mioyo myeupe waelewe na kuthamini kwamba Biblia kwa kweli ni Neno la Mungu. Kufikiria kwa unyofu yale inayosema kwaweza kuwaanzisha kwenda kwenye barabara inayoongoza kwenye uzima. Kwa hiyo, fanya jitihada ya pekee ili kuangusha kitabu hiki kwa watu wengi kama uwezavyo.
7 Sote twapaswa kuwa tumesoma kitabu chote hiki kipya kabla ya kampeni ya Machi kuanza. Tutataka kukipa kitabu God’s Word ugawanyaji mkubwa zaidi iwezekanavyo, tukikitoa katika kila sehemu ya huduma.