Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/90 kur. 1-2
  • Sababu Wapaswa Kutaka Kuongoza Funzo la Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu Wapaswa Kutaka Kuongoza Funzo la Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SALI KWA AJILI YA MAFUNZO
  • MAKALA ZA USONI
  • Je! Unatoa Mafunzo ya Biblia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Sehemu ya 1: Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Je, Unaweza Kushiriki Katika Kazi ya Kufanya Wanafunzi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Kutoa Habari Njema Kutoa Mafunzo ya Biblia Nyumbani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 8/90 kur. 1-2

Sababu Wapaswa Kutaka Kuongoza Funzo la Biblia

1 Mojawapo mambo yenye kuthawabisha sana kwa Mkristo ni kutumiwa na Yehova kusaidia mtu mwingine awe mwanafunzi wa Kristo. (Mt. 28:19, 20; 1 Kor. 3:6, 9) Kwa wale tunaosaidia katika njia hiyo, yaweza kumaanisha uhai wa milele.

2 Uhusiano wa karibu sana husitawi kati ya mwalimu na yule anayefunzwa. Ukuzi wa kiroho wa mwanafunzi hakika ni chimbuko la shangwe kubwa. (1 The. 2:11, 19, 20) Kwa hiyo, wapasa kuwa mradi wa kila Mkristo kuongoza angalau funzo la Biblia moja la nyumbani pamoja na mtu wa nje ya nyumba yake mwenyewe. Bila shaka, ni daraka la kila kichwa wa familia kuongoza funzo la Biblia lenye maana, la kawaida pamoja na familia yake mwenyewe. Katika nyumba zile ambazo baba si mwamini, mama Mkristo atahitaji kufanya mipango inayohitajiwa kwa ajili ya kujifunza Biblia pamoja na watoto.

SALI KWA AJILI YA MAFUNZO

3 Kwa kuwa tumesonga sana katika huu wakati wa mwisho, wote wapaswa kutia jitihada za kuongoza mafunzo ya Biblia yenye mafanikio. Sala za kawaida kwa Yehova kuhusu hilo hudhihirisha tamaa yetu ya moyo mweupe ya kuongoza funzo la Biblia. Huonyesha kwamba sisi huliona suala la uhai na kifo linalohusika. (Eze. 33:7-9, 14-16) Twaweza kuwa na uhakika wa baraka ya Yehova juu ya jitihada zetu za kudhamiria.—1 Yn. 5:14, 15.

4 Ili kuwa wenye mafanikio katika kufanya wanafunzi, ni lazima tutayarishe vizuri. Pia husaidia sana kuchunguza wengine walio wastadi wa kuongoza mafunzo ya Biblia. Katika miezi ijayo, tutawajulisha madokezo kutoka kwa waangalizi wasafirio na wengine ambao wamefaulu katika kufanya wanafunzi. Mfululizo wa makala utakakazia mawazo fulani yenye kutumika juu ya jinsi ya kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia yenye mazao.

MAKALA ZA USONI

5 Ni yapi baadhi ya mawazo hayo yatakayofikiriwa katika makala za usoni za Huduma ya Ufalme Yetu? Tutazungumza jinsi wahubiri na mapainia mbalimbali wameanzisha mafunzo ya Biblia na ni mbinu gani za kufundisha ambazo wametumia kufikia mioyo ya wanafunzi. Pia tutashiriki madokezo juu ya kujenga uthamini kwa ajili ya tengenezo la Yehova na kusitawisha tamaa ya kushiriki katika utumishi wa shambani. Pia kutakuwako madokezo juu ya jinsi ya kufanya funzo la familia yako mwenyewe liwe lenye maana zaidi ili watoto wako wasitawishe uhusiano wa karibu na Yehova.

6 Wakati wa miaka minne ya utumishi iliyopita, watu 959,834 wamebatizwa ulimwenguni kote, na 4,258 kati yao imekuwa katika makundi ya Afrika Mashariki. Walio wengi wa watu hao walifikia hatua ya kubatizwa kwa msaada wa mtu fulani mwenye kuongoza funzo la Biblia pamoja nao. Uhudhuriaji kwenye Ukumbusho na kwenye mikusanyiko ya wilaya yetu hudokeza kuna wengi zaidi wanaoweza kusaidiwa wafanye maendeleo kufikia ubatizo. Kwa kuendelea na jitihada zetu za kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia na watu hao, huenda tukaweza kuwasaidia wengi zaidi wawe wanafunzi na hatimaye washangilie uhai wa milele.—1 Tim. 6:12, 19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki