Upainia—Utumishi Unaothawabisha Sana
1 Yehova anataka tushangilie na kuona mema kwa kazi yetu yote ngumu. (Mhu. 5:18) Kazi iliyo ya maana zaidi tunayoweza kushiriki ni utendaji wa kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi. Paulo alimhimiza Timotheo: “Fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako.” (2 Tim. 4:5) Yeye alimtia moyo Timotheo, na maneno ya Paulo yanatutia moyo kila mmoja wetu leo tuwe wenye nafsi yote katika huduma yetu. Kwa wengine, huduma ya nafsi yote huenda ikatia ndani kutumika ukiwa painia wa kawaida. Kwa nini usifikirie kwa sala kama hali zako zitakuruhusu kufanya utumishi wa wakati wote?
2 Hatua Chanya Yahitajika: Kuingia katika kazi ya upainia hutaka kuchukua hatua za maana kupatana na sala zetu. Kuza tamaa ya kuhisiwa moyoni ya utumishi wa Yehova, pamoja na upendo kwa watu. Ongeza utendaji wako shambani, ukikuza ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia. Fanyia kazi kusitawisha ratiba nzuri; ona mambo kihalisi. Tafuta madokezo kutoka kwa wazee na mapainia. Shikamana na njia ya maisha iliyofikiriwa vizuri ya kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Nidhamu ya kibinafsi, ujianzishaji, na jitihada zahitajiwa. (1 Kor. 9:23, 25, 27) Hatua hizo chanya zimo miongoni mwa zile zilizochukuliwa na wale zaidi ya 800 waliojiandikisha katika mwaka uliopita.
3 Kuweka miradi hususa na kufanya kazi kwa bidii kuzielekea kutatuwezesha kufanya maendeleo katika mahubiri yetu tunapofanyia maendeleo uwezo wetu. Je! tunaweza kufanyia maendeleo matangulizi yetu kwenye milango au jinsi tunavyoshughulika na mapingamizi? Je! tunatumia kikamili vichapo vyote vinavyopatikana? Je! tunaongoza funzo la Biblia lenye maendeleo? Je! tunaweza kuanza upainia msaidizi sasa tukiwa na wazo la upainia wa kawaida baadaye? Miradi lazima iwe yenye kutumika na iwekwe kulingana na yale tuwezayo kutimiza. Kutimiza miradi hiyo kutaendeleza matokeo yetu na kutuletea uradhi mwingi.—1 Tim. 4:15, 16.
4 Njia ya Maisha Yenye Kuthawabisha: Kufanya upainia ukiwa na kusudi linalofaa na tamaa ya kufanya maendeleo ya kiroho huleta faida nyingi. Tunakuza utegemeo wenye nguvu zaidi kwa Yehova. Ustadi mwingi zaidi wa kutumia Neno la Mungu huja kutokana na kulitumia mara kwa mara katika huduma. Uvutano unaofaa unatolewa kwenye kundi, na wengine huenda wakatiwa moyo kuwa na ushiriki zaidi katika huduma kwa sababu ya mfano wetu wenye bidii. Kupainia kwaweza kutusaidia kuwa na mtazamo wa maisha ulio wa kiroho zaidi na utumike kutulinda kutokana na miradi, tamaa, na mashirika ya kilimwengu.
5 Yesu aliwaambia wafuasi wake: “Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.” (Mt. 9:37, 38) Uhitaji wa wafanyakazi ni mkubwa hata zaidi sasa kuliko ilivyokuwa katika siku za Yesu. Upainia huturuhusu tuwe na fursa ya kuwa na ushiriki kamili katika kazi hii ya haraka, ya kuokoa uhai. Hakuna kitu kinachoweza kulinganishwa na uradhi na utoshelezo ambao huja kwa mtu kutumia maisha yake katika utumishi wa wakati wote kwa Muumba wetu Mkuu.—Mit. 10:22.