Habari Za Kitheokrasi
Congo: Tuna furaha kuripoti kwamba kazi ya Mashahidi wa Yehova ilitambuliwa kisheria katika Jamhuri ya Watu ya Congo wakati wa Novemba 1991.
Afrika Mashariki: Wakati wa ziara ya mwangalizi wa eneo la dunia ya hivi karibuni, 5,661 walihudhuria hotuba ya pekee Nairobi na 4,360 katika Addis Ababa.
Kenya: Alhamisi, Machi 26, 1992, serikali ya Kenya ilirudisha usajili wa shirika la Association of Jehovah’s Witnesses in East Africa. Hatua hiyo inaondolea mbali swali lolote au shaka kuhusiana na msimamo wa kisheria wa Shirika hilo.
Peru: Jumla ya wahubiri 39,104 katika Desemba inaonyesha ongezeko la asilimia 12 kupita mwezi uo huo mwaka mmoja uliopita. Jambo la kutokeza ni uhakika wa kwamba mapainia 8,842 hufanyiza asilimia 23 ya jumla ya wahubiri.