Habari Za Kitheokrasi
Utendaji wenye kutokeza wa funzo la Biblia uliripotiwa Novemba kutoka nchi zifuatazo ambako kazi yetu imepata utambulisho rasmi hivi karibuni:
Albania: Jumla ya wahubiri 99 waliongoza mafunzo ya Biblia 210.
Bulgaria: Wahubiri wao 296 waliripoti mafunzo ya Biblia 657.
Majimbo ya Baltiki: Nchi hizi ziliripoti jumla iliyounganishwa ya wahubiri 2,199 na mafunzo ya Biblia 4,632.
Hesabu ya ripoti zenye kutia moyo pia zaja kutoka Afrika:
Chad: Kukiwa na wahubiri 345 katika Oktoba, hudhurio kwenye programu zao sita za siku ya kusanyiko la pekee lilikuwa 654.
Jamhuri ya Afrika ya Kati: Kilele kipya cha wahubiri 1,600 kilifikiwa katika Oktoba, na waliripoti mafunzo ya Biblia nyumbani 2,966.
Rwanda: Katika Novemba wahubiri 1,762 walioripoti waliongoza mafunzo ya Biblia nyumbani 6,270.
Ripoti hizo zilizounganishwa zatoa uthibitisho wa kustaajabisha kwamba Yehova anatimiza ahadi yake sasa ya kuzidisha kazi ya kukusanya katika siku yetu—Isa. 60:22.