Kuwasaidia Wengine Wathamini Thamani ya Vichapo Vyetu
1 “Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu.” (Ebr. 4:12) Kwa kuwa vichapo vyetu vya Biblia husaidia watu wanufaike kutokana na nguvu ya Neno la Mungu, twavitumia kuchochea kupendezwa katika Biblia tunapotoa ushahidi wa vivi-hivi au tunapoenda nyumba kwa nyumba.
2 Toleo la fasihi la Januari ni kitabu chochote cha kurasa 192 kilichochapwa kwenye karatasi inayobadili rangi na kuwa manjano au inayochakaa au chochote kilichotangazwa kabla ya 1980. Ikiwa vitabu hivyo vinapatikana katika kutaniko lenu, tayarisha utoaji wako wa ujumbe wa Ufalme ili utaje jambo hususa katika kitabu unachotumia. Jambo hili laweza kufanywaje?
3 Jinsi ya Kutayarisha: Kwanza, chagua elezo moja katika kitabu unachotumia ambalo yaelekea litawavutia watu wenye moyo mweupe katika eneo lenu. Kisha, fikiria tukio la karibuni au jambo la kupendeza kwa ujumla ambalo huenda ukaweza kuzungumzia kifupi na mwenye nyumba kabla ya kuvuta uangalifu wake kwenye elezo lililochapishwa ambalo umechagua. Labda kuna andiko lililowekwa bila manukuu lililonukuliwa au ambalo unaweza kusoma, liwe katika Biblia au moja kwa moja kutoka kwa kitabu, la kuunga mkono maelezo yako. Kitoe kitabu hicho kwa mchango wa kawaida. Kisha jaribu kumwacha na swali au wazo ambalo waweza kutumia kuwa msingi wa ziara ya kurudia.
4 Makutaniko mengi yana nakala chache za Kupata Faida Zote za Ujana Wako na Kumsikiliza Mwalimu Mkuu. Ikiwa vitabu hivi vyapatikana, kwa nini usijitayarishe kwa mazungumzo pamoja na vijana unaokuta katika eneo lenu? Watie moyo wasome mojapo vichapo hivyo vizuri. Ikiwa unatoa Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele, unaweza kutumia njia iliyoonyeshwa juu na ujitayarishe kuzungumzia yoyote ya mafundisho ya Biblia yaliyo kwenye msaada huu bora sana wa Biblia.
5 Toa Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu: Huenda ukaweza kuanzisha mazungumzo kwa kutoa uangalifu kwa habari ambayo yaonyesha kujihusisha kwa dini katika mambo ya kilimwengu au inayoonyesha uvutano wa dini katika maisha za watu.
Halafu tokeza swali, kama hili:
◼ “Wewe unafikiri Mungu anaonaje mifumo ya kidini yenye uvutano juu ya mambo ya ulimwengu leo? [Ruhusu jibu.] Je! utashangaa kujua kwamba mafundisho ya msingi ya dini hizi zote yanafanana na kwamba hayo ni tofauti kabisa na mafundisho ya Biblia?” Mwenye nyumba akitaka kusikiliza, mwonyeshe yaliyomo, na umweleze kifupi kwamba mtu awe ni wa kidini au sivyo, maisha yake yanaathiriwa na mavutano yenye nguvu ya kidini. Mwonyeshe kwamba anaweza kunufaika kwa kujifunza ni kwa nini utafutaji wa Mungu wa ainabinadamu umeongoza kwenye njia nyingi na zilizo mbali na jinsi ya kuitambua dini ya kweli.
6 Nyakati nyingine huenda ikafaa zaidi kutoa magazeti au trakti. Tuna kila sababu ya kuwa na idili na bidii juu ya kutia moyo wengine wasome vichapo hivi ili kwamba waweze kujiandaa kuona uwezo wa Neno la Mungu katika maisha yao kwa kuitikia mwelekezo walo.