Sanduku La Swali
◼ Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko yanapaswa kuongozwa wakati gani?
Kwa kawaida yafaa zaidi kuwa na vikundi kadhaa vya funzo la kitabu vikikutana katika mahali mbalimbali kotekote katika eneo la kutaniko badala ya kufanya wote waje kwenye Jumba la Ufalme. Mafunzo hayo yapaswa kuongozwa wakati ufaao zaidi kwa wengi wa wale wanaogawiwa kuhudhuria mahali hapo. Kwa kawaida, hiyo ni jioni moja katika juma wakati hakuna mikutano mingine au utendaji mwingine wa utumishi uliopangwa. Hata hivyo, huenda ikanufaisha kupanga kuwe na funzo la kitabu wakati wa mchana ili kuwezesha wazee-wazee wanaosita kutoka nje wakati wa giza na wafanyakazi wa usiku wahudhurie. Katika hali chache, huenda ikafaa kuwa na funzo la wakati wa mchana katika mwisho-juma.
Wazee wanaweza kuuliza maswali yanayofaa ili kuamua nyakati za mikutano “inavyofaa wingi wa wahubiri” na pia wale wanaopendezwa. (om-SW uku. 62) Wakati unaochaguliwa wapaswa uwe siku na saa ambayo haitakatiza isivyofaa wala kuwekea mpaka mipango ya utumishi wa shambani iliyowekwa.