Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/96 uku. 1
  • Kutoacha Kutangaza Habari Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoacha Kutangaza Habari Njema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Kuendeleza Huduma Yetu Bila Kuacha
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Watasikiaje?
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Nyumba kwa Nyumba Bila Kuacha
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Hubiri Bila Kuacha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 8/96 uku. 1

Kutoacha Kutangaza Habari Njema

1 Wakristo wa mapema waliichukulia kwa uzito sana huduma yao. Luka aliripoti: “Kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.” (Mdo. 5:42) Hakuna kitu chochote ambacho kingewazuia, hata mnyanyaso. (Mdo. 8:4) Waliwaambia wengine juu ya kweli kila siku.

2 Vipi na sisi? Jiulize: ‘Je, mimi huhisi uharaka wa nyakati? Je, nimeazimia kuendelea kutangaza habari njema bila kuacha?’

3 Vielelezo vya Siku ya Kisasa vya Kuhubiri Bila Kuacha: Dada mmoja, mwenye ugonjwa wa polio, alikuwa katika chombo cha kusaidia kupumua. Hakuweza kwenda kwenye Jumba la Ufalme au kuhudhuria kusanyiko. Lakini alikuwa na shughuli nyingi sana ya kuhubiri habari njema. Wakati wa ugonjwa wake wa miaka 37, aliweza kusaidia watu 17 wajifunze kweli! Alifanyaje hivyo? Ijapokuwa alishindwa kwenda mlango hadi mlango, alipata njia ya kutoa ushahidi wa vivi hivi kila siku kwa wale waliokutana naye.

4 Ndugu zetu katika Bosnia wamelazimika kukabiliana na vita na uhitaji. Hata hivyo, wao huendelea kwa ukawaida kuhubiria wengine. Katika Sarajevo watangazaji wamekuwa wakifanya wastani wa saa 20 kila mwezi wakiongea na wengine kuhusu habari njema, na kwa wastani wanaongoza mafunzo ya Biblia mawili kila mmoja. Ijapokuwa hali zao ngumu sana, wao wanahubiri na kufundisha bila kuacha.

5 Wachanga pia huonyesha bidii kwa huduma. Familia ya Mashahidi katika Rwanda waliwekwa kwenye chumba ambapo wanajeshi walikuwa wamejitayarisha kuwaua. Hiyo familia iliomba ruhusa ya kusali kwanza. Wakaruhusiwa, na binti mchanga, Deborah, alisali kwa sauti kubwa: “Yehova, juma hili baba na mimi tuliangusha magazeti matano. Tutarudije kwa watu hawa kufundisha kweli na kuwasaidia wapate uhai?” Kwa sababu ya imani yake yenye nguvu na upendo wake kwa huduma, familia nzima ilihifadhiwa.

6 Leo, kuna uhitaji wa kuangalia fursa za kutolea wengine ushahidi na kutafuta wale “walio na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele.” (Mdo. 13:48, NW) Kupatana na hali za kwenu, wazee wa kutaniko wanaweza kufanya mipango ya vikundi vya kutoa ushahidi nyakati zifaazo, iwe ni asubuhi, alasiri, au jioni. Makala zilizo katika Huduma ya Ufalme Yetu na sehemu ya Mikutano ya Utumishi, makusanyiko ya mzunguko, na mikusanyiko ya wilaya hutoa madokezo ya wakati ufaao na kitia moyo cha kushiriki katika aina mbalimbali za ushahidi wa Ufalme. Kwa kuongezea haya, waangalizi wa mzunguko na wa wilaya huzoeza watangazaji kutoa ushahidi wa barabarani, wao huonyesha jinsi ya kuhubiri eneo la biashara, na kuonyesha njia nyinginezo za kutoa ushahidi mahali popote ambapo watu wanapatikana. Yote hayo hukazia kutoacha kutangaza habari njema!

7 Mitume wa Yesu walitangaza hivi kwa ujasiri: “Sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.” Walivumiliaje vijapokuwa vipingamizi vyote hivyo? Walimwomba Yehova awasaidie, naye akafanya hivyo, na “wote wakajaa roho Mtakatifu [“roho takatifu,” NW], wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.” (Mdo. 4:20, 29, 31) Si kila mtu awezaye kubarikiwa na mambo yaliyoonwa yenye kutokeza katika huduma, lakini ikiwa kwa kweli twatamani kutangaza habari njema bila kuacha na ikiwa twajitahidi kufanya hivyo hata kila siku, Yehova atatusaidia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki