Sanduku La Swali
◼ Ni jambo gani linalopaswa kufanywa msemaji wa hotuba ya watu wote akosapo kufika kwa wakati kwenye mkutano?
Pindi kwa pindi, hali zisizoepukika zitazuia ndugu kufika kwa wakati ili kutoa hotuba yake aliyoratibiwa. Ikiwa kuna sababu ya kuamini kwamba atafika karibuni, wazee huenda wakaamua kuendelea na Funzo la Mnara wa Mlinzi; Mkutano wa Watu Wote unaweza kufuata baadaye. Vipi ikijulikana kwamba msemaji hatafika? Labda mmojawapo wasemaji wa kwenu anaweza kutoa hotuba yoyote ambayo tayari ametayarisha.
Mara nyingi kupanga mapema kwa uangalifu huzuia tatizo hili. Mpangaji wa hotuba ya watu wote apaswa kuwasiliana na kila msemaji angalau juma nzima mapema ili kumkumbusha juu ya mgawo wake. Kikumbusha chapaswa kutia ndani wakati wa mkutano, mahali lilipo Juma la Ufalme na namba ya simu, na mielekezo yenye kueleweka ya jinsi ya kupata jumba. Msemaji apaswa kuandika vizuri mambo haya. Apaswa kuchukulia mgawo huo kwa uzito, akifanya marekebisho yoyote yahitajiwayo kwa mambo yake ya kibinafsi ili aweze kutimiza kikamili daraka lake. Jambo lisiloepukika litokeapo ambalo litamzuia kufanya hivyo, apaswa kumjulisha mpangaji wa hotuba ya watu wote mara moja ili msemaji wa badala apangiwe. Kila jitihada yapaswa kufanywa ili kuepuka mahairisho ya dakika za mwisho. Msemaji akichelewa na awe atafika dakika chache baadaye, anaweza kufanya mipango ya kupiga simu mahali inapowezekana, kwenye Jumba la Ufalme ili ndugu wajue jambo la kufanya.
Uthamini wa migawo ya hotuba ya watu wote, mpango mzuri wa mapema na vikumbusha, na uangalizi mzuri waweza kuhakikisha kwamba kutaniko litaweza kufurahia hotuba ya watu wote yenye kunufaisha kila juma.