Michango kwa Kazi ya Ulimwenguni Pote ya Sosaiti Yaunga Mkono Upanuzi
Kama ilivyotabiriwa kwenye Isaya 54:2, 3, ibada safi ya Yehova yaendelea kupanuka ulimwenguni pote. Hii yatia ndani nchi mbalimbali katika bara la Afrika na visiwa vilivyo karibu. Wakati wa miaka kumi iliyopita, vizuizi vya utendaji wa Kikristo vimeondolewa mahali kama vile Angola, Ethiopia, Guinea ya Ikweta, Kamerun, Madagaska, Malawi, Msumbiji, na Togo. Katika nchi hizi na nyinginezo ambapo shamba ni jeupe kwa mavuno, wamishonari wa Gileadi, wahitimu wa Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, washiriki wa familia ya Betheli, na wengine wamepata migawo.—Mt. 9:37, 38.
Ni wazi kwamba ongezeko la waabudu wa kweli katika tengenezo la Yehova lahitaji ujenzi wa mamia ya Majumba ya Ufalme mapya. Pia kupangia Majumba ya Kusanyiko na majengo mapya au yaliyopanuliwa ya tawi kumekuwa kwa lazima. Kugharimia kifedha miradi hii pamoja na kuendeleza kazi ya Ufalme katika Afrika na sehemu nyingine za ulimwengu pia kumetumia michango mingi sana ya kazi ya ulimwenguni pote ya Sosaiti.
Picha na michoro iliyo kwenye kurasa mbili za nyongeza hii zakujulisha kile ambacho Sosaiti imekuwa ikijitahidi kutimiza katika shamba la Afrika. Linaloonyeshwa ni baadhi ya ujenzi ambao sasa unaendelea na miradi ambayo itaanza hivi karibuni.
Kwa kuangalia chati ya utumishi wa shambani katika Kitabu-Mwaka cha 1996, (cha Kiingereza) unaweza kuelewa vizuri kile ambacho watangazaji katika nchi hizi wanafanya katika huduma. Maongezeko yenye kutokeza yamekuwa yakiendelea katika nchi nyingi, na uwezekano wa ukuzi unaonyeshwa katika mahudhurio ya Ukumbusho yasiyo na kifani. Tunapokumbuka yanayotimizwa yakiwa sehemu ya kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi ya tufe lote katika bara letu, tunakaziwa pendeleo tulilo nalo la kutegemeza kwa njia ya kimwili makusudi ya ibada ya kweli.—Luka 16:9; 1 Tim. 6:18.
[Picha katika ukurasa wa 3]
Jumba la Ufalme katika KwaZulu-Natal, Afrika Kusini, lililojengwa kwa siku 9
[Picha katika ukurasa wa 3]
Jumba la Ufalme lenye gharama ndogo katika Nigeria
[Picha katika ukurasa wa 3]
Jumba la Kusanyiko katika Msumbiji lenye viti vya kukalia watu 1,500, linalopaswa kukamilishwa mwishoni mwa 1996
[Picha katika ukurasa wa 3]
Majengo ya tawi la Msumbiji, yanayopaswa kuwa tayari kutumiwa mwishoni mwa 1996
[Picha katika ukurasa wa 3]
Tawi la Sierra Leone, limeratibiwa kukamilika kiangazi hiki
[Picha katika ukurasa wa 4]
Jumba la Kusanyiko la Mauritius lililo na paa lakini bila kuta, pamoja na majengo ya tawi, yanayopaswa kukamilishwa katika masika ya 1997
[Picha katika ukurasa wa 4]
Tawi la Zimbabwe lingali linaendelea kujengwa
[Picha katika ukurasa wa 4]
Jumba la Kusanyiko lililo wazi na tawi jipya linaendelea kujengwa katika Senegal
[Picha katika ukurasa wa 4]
Tawi jipya la Kenya, katika jiji kuu, Nairobi
[Picha katika ukurasa wa 4]
Tawi la Madagaska linalopaswa kukamilishwa hivi karibuni
[Picha katika ukurasa wa 4]
Majengo yanayokusudiwa Malawi