Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/98 uku. 1
  • Je, Una “Mwiba Katika Mwili”?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Una “Mwiba Katika Mwili”?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Kukabiliana na “Mwiba Katika Mwili”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Udhaifu wa Kibinadamu Hutukuza Nguvu za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • “Mwiba Katika Mwili” wa Paulo
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 5/98 uku. 1

Je, Una “Mwiba Katika Mwili”?

1 Twatamani sana kutimiza utume wetu wa kuhubiri habari njema kwa uwezo wetu ulio bora zaidi. Hata hivyo, wengi kati ya ndugu na dada zetu wapendwa, huona kuwa vigumu kushiriki kikamili kwa sababu ya magonjwa makubwa ya kimwili au kutojiweza huingilia, kukifanya iwe vigumu kufanya mengi zaidi kadiri ambavyo wangependa. Kwao, huenda likawa jambo gumu kukabiliana na hisia za kuvunjika moyo, hasa wanapoona wengine wakiwa watendaji sana katika huduma.—1 Kor. 9:16.

2 Kielelezo cha Kuiga: Ilimbidi mtume Paulo ashindane na “mwiba katika mwili.” Mara tatu alimsihi Yehova aondoe kizuizi hicho chenye kutaabisha, ambacho alikifafanua kuwa “malaika wa Shetani” aliyefuliza kumpiga kofi. Hata hivyo, licha ya hilo, Paulo alivumilia na kusonga mbele katika huduma yake. Hakujihurumia wala kulalamika daima. Alifanya yote awezayo. Kilichomwezesha kufanikiwa kukabiliana na hali hiyo kilikuwa uhakikishio huu kutoka kwa Mungu: “Fadhili yangu isiyostahiliwa yakutosha wewe; kwa maana nguvu yangu inafanywa kamilifu katika udhaifu.” Udhaifu wa Paulo uliimarishwa alipojifunza kukubali hali yake na kumtegemea Yehova na roho takatifu ili avumilie.—2 Kor. 12:7-10.

3 Jinsi Unavyoweza Kuvumilia: Je, udhaifu wa kibinadamu huwekea mipaka utumishi wako kwa Mungu? Ikiwa ndivyo, iga mtazamo wa Paulo. Hata kama ugonjwa wako au kutojiweza kwako hakuna ponyo la kudumu katika mfumo huu wa mambo, waweza kumtumaini Yehova kabisa, ambaye huelewa mahitaji yako naye ataandaa “nguvu ipitayo iliyo ya kawaida.” (2 Kor. 4:7) Tumia kwa kujifaidi msaada uliopo kutanikoni, si kujitenga mwenyewe. (Mit. 18:1) Ukiona ni vigumu kushiriki katika mahubiri ya mlango hadi mlango, tafuta njia zitumikazo za kutoa ushahidi wa vivi hivi au kwa njia ya simu.

4 Ijapokuwa mwiba katika mwili huenda ukakuzuia kufanya yale unayoweza katika huduma, huhitaji kuhisi kwamba huwezi kushiriki. Kama vile Paulo, wewe pia waweza “kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili isiyostahiliwa ya Mungu,” ukifanya yale ambayo nguvu na hali zako zaruhusu. (Mdo. 20:24) Unapojitahidi kutimiza huduma yako, jua ya kwamba Yehova apendezwa sana.—Ebr. 6:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki