Mkusanyiko wa Wilaya wa 1999 wa “Neno la Mungu la Kiunabii” wa Mashahidi wa Yehova
1 Waisraeli walipokuwa nyikani, Yehova alimwagiza Musa afanyize tarumbeta mbili za fedha. Kama tarumbeta moja ingepulizwa, wajumbe wa makabila walikuwa wakusanyike mlangoni pa hema la kukutania. Mapulizo ya tarumbeta zote mbili yangetolea ishara kusanyiko lote la Israeli lije pamoja. (Hes. 10:1-4) Leo, je, hatusisimuki tunaposikia matangazo ambayo, kama mapulizo ya tarumbeta, hutukusanya kwenye mikusanyiko yetu ya wilaya ya kila mwaka? Kwenye mikusanyiko yetu sisi hupokea mafundisho na mwongozo wa Yehova kupitia Neno lake na wawakilishi wake waliowekwa. Hiyo hutusaidia twendelee kuwa imara katika utumishi wa Mungu. Je, hatushangilii tuonapo maelfu—labda hata makumi ya maelfu—ya waabudu wenzetu waaminifu wakikusanyika pamoja katika upendo na amani? Kwa hakika sisi hushangilia!—Zab. 122:1, 7, 8.
2 Kuanzia Novemba 1998 hadi Januari 1999, jumla ya Mikusanyiko ya Wilaya na ya Kimataifa 16 ilifanywa katika miji 15 kotekote Afrika Mashariki. Akina ndugu na dada wanaoishi Nairobi walikaribisha maelfu ya wajumbe kutoka nchi mbalimbali duniani, waliokuwa wakihudhuria mkusanyiko wa kimataifa uliofanyiwa Kenya. Lugha mbalimbali zilizozungumzwa hazikuthibitika kuwa kizuizi chochote cha mawasiliano kwa upendo mchangamfu kwenye mikusanyiko. Akina ndugu waliotoa nafasi katika makao yao ili kuwakaribisha wajumbe wa kigeni walipata ushirika wenye kufurahisha zaidi. Wamishonari waliohudhuria mikusanyiko katika nchi zao walirudi kwa wakati ufaao na walikuwepo kwenye mkusanyiko wa kimataifa, Nairobi. Kuwapo kwao kulithibitika kuwa kwenye kutia moyo wote kiroho. Tunapokusanyika pamoja kwa ajili ya mkusanyiko wetu wa wilaya wa 1999, tutakuwa na fursa za ziada za kufurahia udugu wetu wenye thamani na kumshukuru Yehova kwa muungano ambao ametupatia.
3 Kufanya Mipango Yako ya Mahali pa Kulala: Fikiria mapema kwa uzito mahali utakapolala. Ukitaka kukaa hotelini kwenye mji wa mkusanyiko nawe wataka msaada kutoka Idara ya Mahali pa Kulala, tafadhali andikia Idara ya Mahali pa Kulala ya mkusanyiko, ukionyesha ni kiasi gani ambacho uko tayari kulipia mtu mmoja kwa siku. Ukifanya mipango ya kukaa hotelini kupitia Idara ya Mahali pa Kulala, tafadhali heshimu mpango huo.
4 Kutunza Walio na Mahitaji ya Pekee: Tafadhali uwe chonjo kuangalia mahitaji ya wazee-wazee, wagonjwa, wale walio katika utumishi wa wakati wote, au wengine walio katika kutaniko lenu ambao huenda wakahitaji msaada wa kuhudhuria mkusanyiko. Watu wa jamaa, wazee, na wengine kutanikoni ambao wanajua hali za pekee za wale wenye mahitaji ya pekee wanaweza kusaidia kwa upendo kufanya mipango ya lazima.—Linganisha 1 Timotheo 5:4.
5 Fomu ya Sosaiti ya Ombi la Mahali pa Kulala kwa Wenye Mahitaji ya Pekee yaorodhesha sifa zinazohitajiwa ili kuwasilisha fomu hii. Uandalizi huo ni kwa ajili ya wahubiri walio na msimamo mzuri tu, kutia ndani wale walio na watoto wenye adabu nzuri, ambao wamekubaliwa na Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Maombi haya yapasa kupelekwa kwenye Idara ya Mahali pa Kulala upesi iwezekanavyo, kwa kutumia anwani ya mkusanyiko iliyoonyeshwa upande wa nyuma wa fomu hiyo.
6 Kuonyesha Uthamini: Familia moja ya Mashahidi iliandikia meneja wa hoteli walimokaa hivi: “Hoteli yako ilikuwa hoteli nzuri zaidi ambayo familia yetu imepata kukaa. Vyumba vilisafishwa sana na kuwekwa vitu vyote ambavyo tungehitaji. Tulifurahia mwisho-juma huo mzuri sana kwa sababu ya ushirikiano wa kila mmoja katika hoteli yako. Twakushukuru kwa kushirikiana na mipango ya Mikusanyiko ya Watchtower kwa kutuandalia bei ambazo tungemudu kulipia.” Je, wewe pia washukuru kwa mipango mingi iliyofanywa kwa niaba yako? Sosaiti inafurahi kusaidia kutafuta mahali pa kulala penye gharama nafuu wakati wa mkusanyiko, ikituruhusu kukazia uangalifu manufaa za kiroho za mkusanyiko na programu hiyo.
7 Inatia moyo kusikia sifa inayotolewa kwa jina la Yehova kwa sababu ya mwenendo mzuri wa ndugu na dada zetu kwenye mikusanyiko. Mfanyakazi mmoja wa hoteli alisema: “Wajumbe wenu ni watu wazuri kabisa tulio nao hapa.” Mwingine alieleza hivi: “Sisi hupenda kuwawekea nafasi watu wenu. Ni wapole na huwa tayari na habari tunayohitaji. Na ni kikundi kilicho rahisi zaidi kushughulika nacho.” Meneja wa mkahawa mmoja alisema: “Tunafurahia kuwa na kikundi cha watu mjini, ambacho tunaweza kuonea fahari.” Mkahawa huo ulipunguzia bei kwa kiasi cha asilimia 10 wajumbe waliovalia beji ya mkusanyiko! Naye meneja mmoja wa hoteli alisema hivi: “Imekuwa furaha kuwa na watu wenu katika hoteli yetu.” Maelezo hayo ni ushuhuda mzuri kutoka kwa watu wa nje. Sifa nzuri ambayo tumejipatia humtukuza Yehova na kumfanya atuonee fahari.—1 The. 4:12; 1 Pet. 2:12.
8 Twakutia moyo ufanye mipango sasa ili uhudhurie siku zote tatu za Mkusanyiko wa Wilaya wa 1999 wa “Neno la Mungu la Kiunabii.” Tafadhali ona kwamba mikusanyiko ya wilaya itafanywa Agosti/Septemba 1999. Twatazamia kwa hamu pamoja nanyi kusikia “vigelegele vya shukrani” vya wale wanaomwabudu Mungu wakiwa umati uliounganika. (Zab. 42:4, BHN) Yehova na abariki mipango yote inayofanywa ili twendelee kutajirishwa kiroho!
[Sanduku katika ukurasa wa 3]
Saa za Programu
Ijumaa na Jumamosi
3:30 asubuhi – 11:00 jioni
Jumapili
3:30 asubuhi – 10:00 jioni