Je, Utahudhuria?
Kuhudhuria nini? Vipindi vya Ijumaa vya Mkusanyiko wa Wilaya wa 1999 wa “Neno la Mungu la Kiunabii.” Mwaka jana katika eneo la ofisi ya tawi ya Kenya, kilele cha hudhurio Ijumaa kilikuwa 8,318 chini ya kilele cha hudhurio la Jumapili. Hiyo yamaanisha kwamba zaidi ya asilimia 15 ya jumla ya idadi ya watu waliohudhuria Jumapili walikosa thuluthi moja hivi ya programu ya mkusanyiko. Katika maeneo fulani, zaidi ya asilimia 20 walikosa thuluthi moja hivi ya programu hiyo. Je, utapanga mambo yako ili uwepo siku zote tatu za mkusanyiko wa 1999? Twatumaini hivyo.