Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
Ni manufaa zipi zenye kutumika unazopokea sasa kwa kutembea pamoja na Yehova? Unawezaje kukinza kishawishi cha kuruhusu ufuatiaji wa mambo yasiyo ya kitheokrasi yazuie masilahi ya Ufalme yawe ya kwanza maishani mwako? (Mt. 6:33) Je, wewe huona likiwa jambo gumu kutambua lililo jema na lililo baya katika ulimwengu ambao hufanya lililo baya lionekane kuwa jema? (Ebr. 5:14) Mambo hayo yatazungumziwa kwenye kusanyiko la mzunguko lenye kichwa “Nufaika Sasa kwa Kutembea Katika Njia za Mungu,” kuanzia Septemba 1999.—Zab. 128:1.
Jambo jipya Jumamosi ya kusanyiko hili la mzunguko litakuwa Mkutano wa Utumishi wa kigezo. Mwangalizi wako wa mzunguko atajulisha makutaniko kilichopangwa ili wote waje wakiwa wamejitayarisha kufurahia programu hiyo kikamili.
Sehemu yenye kichwa “Mapainia—Fulizeni Kuangalia Jinsi Mnavyotembea” itatuonyesha jinsi tunavyoweza kutumia hekima na kiasi ili tukomboe wakati kwa ajili ya utumishi wa painia. (Efe. 5:15-17) Habari yenye kichwa “Jihadhari na Njia Zinazoonekana Kuwa Sawa Tu” itatufundisha jinsi ya kuhakikisha yale yanayokubalika kwa Mungu katika kila sehemu ya maisha. Hotuba yenye kichwa “Jinsi Unabii Uliotimizwa Unavyotuathiri” itasaidia kujaza akili zetu na mioyo yetu upendo kwa Neno la Mungu. Hotuba ya watu wote yenye kichwa “Njia za Mungu—Jinsi Zinavyonufaisha!” itakazia manufaa zenye kutumika tunazopokea sasa kwa kuendelea kujipatanisha na matakwa yenye uadilifu ya Yehova.
Je, una tamaa ya kuonyesha hadharani kupitia ubatizo wa maji kwamba wataka kutembea katika njia za Mungu ukiwa mmoja wa watumishi wake walio wakfu? Basi zungumza na mwangalizi-msimamizi ili mipango ya lazima ifanywe.
Azimia kutokosa hili kusanyiko la mzunguko la wakati unaofaa. Na uwepo kwa ajili ya programu yote ya siku mbili, kwa kuwa “heri kila mtu amchaye BWANA, aendaye katika njia yake.”—Zab. 128:1.