Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/00 uku. 3
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Sehemu ya 7—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Uwe Imara Katika Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Kusali Mbele ya Wengine Kwa Moyo Mnyenyekevu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Inueni Mikono Yenye Uaminifu-Mshikamanifu Katika Sala
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 6/00 uku. 3

Sanduku La Swali

◼ Ni nani apaswaye kutoa sala kwenye mikutano ya kutaniko?

Sala ya kutaniko ni sehemu muhimu ya ibada yetu. Kuwakilisha wengine mbele ya Yehova ni pendeleo lenye thamani na daraka kubwa sana. Kwa sababu ya umuhimu wake, wazee wanahitaji kutumia uamuzi mzuri wanapoamua ni akina ndugu gani wanaostahili kutoa sala kwenye mikutano. Ndugu waliobatizwa wanaowakilisha kutaniko wanapaswa kuwa wahudumu Wakristo wakomavu ambao wanajulikana kuwa vielelezo bora na kutaniko linawastahi. Sala zao zenye kumhofu Mungu na zenye staha zapaswa kuonyesha uhusiano wao mzuri pamoja na Yehova Mungu. Makala “Kusali Mbele ya Wengine kwa Moyo Mnyenyekevu” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Mei 15, 1986, yaonyesha kanuni muhimu ambazo ni zenye msaada hasa kwa wale ambao husali hadharani kwa niaba ya kutaniko.

Wazee hawatamchagua ndugu ambaye anajulikana kuwa na mwenendo wenye kutilika shaka au mwenye kupuuza mambo atoe sala. Ndugu ambaye huelekea kuwa mwenye chukichuki au mwenye kutumia sala ya hadharani kuwa wakati wa kueleza hitilafiano za kibinafsi hangechaguliwa. (1 Tim. 2:8) Hata ingawa ndugu kijana anaweza kuwa amebatizwa, wazee wataamua kama amekomaa kiroho vya kutosha kuweza kusali kwa niaba ya kutaniko.—Mdo. 16:1, 2.

Mara kwa mara kwenye mikutano ya utumishi wa shambani, huenda ikalazimu dada aliyebatizwa atoe sala ikiwa hakuna ndugu mwenye kustahili wa kuwakilisha kikundi hicho. Atahitaji kujifunga kitambaa kinachofaa cha kichwa. Ikiwa yaonekana kwamba ndugu anayestahili hatakuwapo katika mikutano fulani ya utumishi, wazee wanapaswa kumpa mgawo dada anayestahili aongoze.

Ni jambo la kawaida mwenyekiti wa Mkutano wa Watu Wote kutoa sala ya kufungua. Hata hivyo, kwenye mikutano mingine ya kutaniko, ikiwa kuna ndugu wengi wanaostahili, mtu mwingine badala ya ndugu anayefungua mkutano au aliyegawiwa sehemu ya mwisho anaweza kuitwa atoe sala ya kufungua au sala ya kumalizia. Kwa vyovyote vile, ndugu atakayeitwa kutoa sala kwenye mkutano wa kutaniko apaswa kujulishwa mapema ili aweze kufikiria atakalosema. Kisha anaweza kutoa sala yenye kueleweka, ya kutoka moyoni inayofaa mkutano huo hasa.

Sala hizo hazihitaji kuwa ndefu. Ndugu atoapo sala ya hadharani, mara nyingi ataeleweka vizuri akisimama, akijieleza mwenyewe kwa sauti ya kutosha, na akiongea wazi. Hilo litaruhusu wale wote waliokusanyika wasikie sala hiyo na mwishowe waseme kwa moyo wote “Amina!”—1 Nya. 16:36; 1 Kor. 14:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki