Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/00 uku. 1
  • “Acheni Mambo Yote Yatukie kwa Ajili ya Kujenga”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Acheni Mambo Yote Yatukie kwa Ajili ya Kujenga”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Acha Ufahamu Ukulinde Salama
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Kudumisha Umoja wa Kikristo Katika Mahusiano ya Kibiashara
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Biashara Yako Itakugharimu Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Uwe Mwenye Kujenga
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 7/00 uku. 1

“Acheni Mambo Yote Yatukie kwa Ajili ya Kujenga”

1 Tunaposhughulika na ndugu zetu, twapaswa kufanya yaliyo mema na yatakayowajenga. Hiyo yamaanisha kuhangaikia na kulinda masilahi yao ya kiroho. Ikiwa tunahusika katika kazi ya kimwili inayohusu kutokeza bidhaa fulani au utumishi wa aina fulani, twahitaji kuwa waangalifu tusifanye lolote la kukwaza ndugu zetu.—2 Kor. 6:3; Flp. 1:9, 10.

2 Wengine wamejiingiza katika biashara fulani za kujasiria, wakiwaona Wakristo wenzao kuwa wateja. Mashirika fulani ya mauzo hutia moyo washiriki wake wamwone kila mtu kuwa mteja wao—kutia ndani wale walio katika dini yao. Ndugu wengine wamepanga vikusanyiko vikubwa vya Mashahidi kwa kusudi la kuwatia moyo wajihusishe na biashara fulani. Wengine huendeleza biashara yao ya kujasiria kwa kuwatumia waamini wenzao makala, broshua, habari katika Internet, au tepe ambazo hawakuomba. Je, ingefaa Mkristo kutumia uhusiano wake wa kitheokrasi kujinufaisha kupitia ndugu zake wa kiroho? La!—1 Kor. 10:23, 24, 31-33.

3 Akina Ndugu Wapaswa Kujihadhari: Hiyo haimaanishi kwamba Mkristo hawezi kufanya biashara na ndugu. Hilo ni jambo la kibinafsi. Hata hivyo, wengine huanzisha mipango ya biashara ambayo huchochea pupa, nao hufanya waamini wenzao wawe wenzi wao au watega-uchumi. Nyingi za biashara hizo za kujasiria hufilisika, zikiwagharimu wenye kuhusika fedha nyingi sana. Ijapokuwa huenda ikawa wale waliojiunga na biashara hiyo walichochewa na tamaa ya kupata pesa haraka, msimamizi hapaswi kuhisi kwamba hatalaumiwa biashara hiyo ikifilisika. Anapaswa kuchunguza mapema kwa uangalifu jinsi hali ya kiroho na ya kimwili ya akina ndugu itakavyoathiriwa biashara hiyo ya kujasiria isipofaulu. Hasa wale wenye madaraka ya kitheokrasi wanapaswa kuwa waangalifu kuhusu shughuli zao za kimwili kwa sababu huenda ikawa wengine huwastahi na kuwatumaini sana. Lingekuwa jambo lisilofaa kutumia vibaya kutumainiwa huko. Mapendeleo ya utumishi mtakatifu huenda yakapotezwa ndugu apotezapo staha kutoka kwa wengine.

4 Mradi wetu wapaswa kuwa ‘kuacha mambo yote yatukie kwa ajili ya kujenga.’ (1 Kor. 14:26) Twapaswa kuepuka kufanya chochote ambacho hutokeza au huchochea shughuli za kibiashara ndani ya kutaniko. Mambo hayo hayahusiani na sababu zetu za Kimaandiko za kukusanyika pamoja.—Ebr. 10:24, 25.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki