Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/00 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Julai 10
  • Juma Linaloanza Julai 17
  • Juma Linaloanza Julai 24
  • Juma Linaloanza Julai 31
  • Juma Linaloanza Agosti 7
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 7/00 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Julai 10

Wimbo 7

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Elekeza uangalifu kwenye sanduku “Tazama Ukurasa wa Nyuma,” na utoe onyesho la utoaji mmoja kati ya utoaji mbalimbali uliodokezwa ambao utafaa katika eneo lenu.

Dak. 15: “Hatuwezi Kukoma Kusema.” Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Kazia sababu ambazo hutufanya tuchukue mgawo wetu wa kuhubiri kwa uzito. Tia ndani mambo yanayohusiana na habari hiyo kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1997, ukurasa wa 23-24.

Dak. 18: “Acheni Mambo Yote Yatukie kwa Ajili ya Kujenga.” Wazee wawili wazungumzia makala hiyo. Soma kila fungu na maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa. Kazia kanuni zinazohusika. Kazia uhitaji wa ufahamu wanaposhughulika na mambo ya biashara au kuweka vitega-uchumi. Chunguza shauri lililo katika Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 1997, ukurasa wa 18-19, 22.

Wimbo 15 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 17

Wimbo 23

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Eleza kifupi jinsi ya kutumia broshua Tazama! kusaidia mtu mwenye kupendezwa athamini uhitaji wa kujua na kutumia jina la kibinafsi la Mungu.—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 425-426.

Dak. 10: “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Maswali na majibu. Tangaza tarehe ya kusanyiko la mzunguko lifuatalo kama yajulikana, na usihi wote wahudhurie siku zote mbili. Tia moyo wote wafanye jitihada ya pekee kualika wanafunzi wa Biblia. Kuhudhuria kusanyiko huenda kukaharakisha tamaa yao ya kushiriki kwa ukawaida na kutaniko. Wakati uleule, Mkusanyiko wetu wa Wilaya wa “Watekelezaji wa Neno la Mungu” umepangiwa mwezi wa Agosti na Septemba. Sisi sote na tuhudhurie programu hiyo yote ya siku tatu.

Dak. 20: Ni Nani Anayepaswa Kuwa Kigezo Chako? Baba anaongoza funzo lake la familia na mmoja au wawili wa watoto wake matineja. Hivi majuzi ameona kwamba mazungumzo yao mara nyingi yanakazia mashujaa wa michezo, wacheza-sinema maarufu, watu mashuhuri wa televisheni, na wanamuziki. Anaeleza hangaiko lake kwa sababu kuvutiwa kwa aina hii ni wonyesho wa roho ya ulimwengu. Wanazungumzia Amkeni!, Mei 22, 1998, ukurasa wa 12-14. Vijana hao wanatambua kwamba kuna hatari ya kuhusudu watu mashuhuri wa kilimwengu, nao wanakubali kwamba umashuhuri wa kilimwengu hauna faida kwa Wakristo. Wanachunguza manufaa za kuwaona wazazi wao, wazee, na vielelezo vingine bora katika kutaniko—na hasa Yesu Kristo—kuwa vigezo vyao.

Wimbo 34 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 24

Wimbo 45

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 15: Kujipendekeza Wenyewe Kuwa Wahudumu wa Mungu. Watumishi wa huduma wawili wanazungumzia onyo la upole la Kimaandiko lililotolewa katika Mnara wa Mlinzi, Desemba 15, 1998, ukurasa wa 19-20. Wanathamini uhitaji wa kufikia kuwa watumishi wa huduma na kuchunguza kile ambacho wao binafsi wanaweza kufanya ili kuonyesha kwamba wanatimiza migawo yao. Wanaona umuhimu wa kuwa vielelezo bora katika huduma ya shambani na wanazungumzia njia wanazoweza kuwa wenye msaada kwa wazee kwa kusaidia wengine kibinafsi. Wanakubali kwamba wanataka kufanya yote wawezayo kusaidia kutaniko lithamini uharaka wa nyakati na kukua na kusitawi kiroho.

Dak. 10: Kuandikia Barua Watu Tusioweza Kuwakuta. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kwa kuwa inaendelea kuwa vigumu kukuta watu nyumbani, wahubiri fulani hupata matokeo kwa kuandika barua. Fikiria miongozo hii. Barua zapaswa kuwa fupi, za Kimaandiko, na zenye staha. Usitume barua zisizo na jina. Andika kwa mwandiko mzuri na wenye kusomeka wazi au upige chapa. Andika anwani ya Jumba la Ufalme na saa za mikutano ya kutaniko pamoja na mwaliko wa kuhudhuria. Usitumie anwani ya Sosaiti. Chunguza madokezo yaliyotolewa kwenye kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 87-88, na Sanduku la Swali la Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1996.

Dak. 15: Tumia Utangulizi Mbalimbali Wenye Matokeo. Teua namna mbili au tatu za utangulizi kutoka katika ukurasa wa 9-15 wa kitabu Kutoa Sababu, na uzungumzie jinsi zinavyoweza kutumiwa kwa matokeo katika eneo lenu. Waulize wasikilizaji, “Ni aina zipi za utangulizi unazotumia unapomfikia mtu barabarani, vivi hivi, au vinginevyo?” Toa onyesho la utangulizi wa aina moja au mbili wakati ukiruhusu.

Wimbo 54 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 31

Wimbo 66

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi za Julai. Waombe wasikilizaji watoe mambo yaliyoonwa ya kibinafsi waliyofurahia mwezi huu walipotoa broshua.

Dak. 12: Mahitaji ya kwenu. Tia ndani vikumbusha vifuatavyo vya kugawanya vichapo bila kuitisha malipo. (1) Vichapo vyote vya Sosaiti vyaweza kupewa wahubiri na watu wote wenye kupendezwa bila kuomba mchango hususa. (2) Kutoa mchango si takwa la kupokea kichapo, bali ni kupendezwa kwa moyo mweupe kukisoma kichapo hicho. (3) Tunapotoa “Michango kwa Ajili ya Kazi ya Sosaiti ya Ulimwenguni Pote—Mathayo 24:14”, twapaswa kukumbuka kwamba hatuchangii tu kulipia gharama ya kutokezwa kwa vichapo, bali, ili kutegemeza kazi yote. Ona barua kwa makutaniko yote ya Oktoba 15, 1999.

Dak. 18: “Je, Wewe Huthamini Subira ya Yehova?” Maswali na majibu. Tia ndani maelezo yanayofaa habari hiyo juu ya ustahimilivu wa Yehova.—Ona Buku la 2 la Insight, ukurasa wa 263-264.

Wimbo 75 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 7

Wimbo 88

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 17: “Je, Wewe Ni Mwenye Haya?” Maswali na majibu. Simulia jambo lililoonwa lenye kutia moyo kutoka kwenye 1997 Yearbook, ukurasa wa 43-44.

Dak. 18: Uwe Mwenye Hekima Wakati Wako Ujao. Hotuba itolewe na mzee. Vijana hutamani kufurahia wakati ujao wenye furaha na wale wanaowapenda. Ijapokuwa hilo ni jambo la asili, lazima watumie shauri la kimungu kama watafanikiwa. (Mit. 19:20) Kuvutiwa na mtu wa jinsia tofauti ni uvutano wenye nguvu ujanani. Hisia zisipodhibitiwa, matokeo yaweza kuleta msiba. Wengi hutilia shaka jinsi ambavyo matineja huwa na uhusiano wa kihisia-moyo na mtu wa jinsia tofauti, ukitokeza uhusiano wa kimahaba ambao huongoza kwenye kupeana miadi. Chunguzeni onyo la upole litolewalo katika kitabu Vijana Huuliza, ukurasa wa 231-235. Kazia mambo makuu yaliyo katika Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1999, ukurasa wa 18-23, yanayoonyesha umuhimu wa vijana kutimiza wajibu wao kamili kwa Mungu. Tia moyo matineja watafakari shauri hili na kuzungumza pamoja na wazazi wao wakiwa na maswali.

Wimbo 101 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki