Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/00 uku. 4
  • “Je, Nihame?”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Je, Nihame?”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Hamia Eneo Lenye Uhitaji Mkubwa Zaidi
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
  • Je, Unaweza ‘Kuvuka Uingie Makedonia’?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • “Toka Katika Bara Lako na Kutoka kwa Watu wa Ukoo Wako”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Njia za Kupanua Huduma Yako
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 9/00 uku. 4

“Je, Nihame?”

1 Katika kuitikia amri ya Yesu ya ‘kwenda kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ watumishi wengi wa Yehova waliojiweka wakfu wamehama ili kutumikia mahali palipo na uhitaji mwingi. (Mt. 28:19) Wanamwiga Paulo, ambaye aliitikia ule mwito: “Vuka uingie Makedonia utusaidie.” (Mdo. 16:9) Jambo hilo laweza kufanywaje kwa njia yenye kutumika?

2 Fanya Mambo Hatua kwa Hatua: Je, kutaniko lenu lina eneo lisilohubiriwa mara nyingi? Ikiwa liko, unaweza kujitahidi kuhubiri sehemu hizo. Kabla ya kuamua kwenda popote, wasiliana na wazee wenu kuona kama wanahisi umejiandaa kikamili kuhamia huko. Pia unaweza kumwuliza mwangalizi wako wa mzunguko kama anajua kutaniko la karibu ambalo unaweza kupanua huduma yako. Kwa upande mwingine, baada ya kuhesabu gharama kwa uangalifu, huenda ukafikiria kusaidia katika sehemu nyingine nchini au katika nchi tofauti. Kama hiyo ni tamaa yako, wewe pamoja na baraza lenu la wazee mwapaswa kuandikia ofisi ya tawi mahali unapopendezwa kutumikia, ukionyesha historia yako ya kitheokrasi. Lingekuwa jambo la hekima kutembea mahali hapo kwanza kabla ya kuamua kama wataka au hautaki kuhamia na kukaa mahali hapo.

3 Uwe Mwangalifu Kuhusu Kuhama: Idadi kubwa ya ndugu zetu wanahamia nchi nyingine kwa sababu wanatafuta hali ya maisha iliyo bora au kupata kitulizo kutokana na kukandamizwa. Wanapofanya hivyo, wengine wameangukia mtego wa watu wasio wanyoofu wanaoahidi kuwasaidia watulie katika nchi mpya kisha wanachukua pesa zao na kuwaacha. Katika visa fulani watu hao hata wanajaribu kuwalazimisha wahamaji kuwa watumwa wa ukosefu wa adili. Wanapokataa, wanaachwa bila ulinzi wowote. Hivyo hali ya wahamaji inakuwa mbaya zaidi kuliko ilivyokuwa katika nchi yao. Hata huenda wakawaomba akina ndugu wawape mahali pa kuishi au kuwasaidia, wakilemea familia nyingine za Kikristo ambazo zinajaribu kupambana na matatizo na magumu yao wenyewe. Washiriki wa familia nyingine wametengana na familia zikadhoofika kiroho kwa sababu ya kuhama huko kusikofaa.—1 Tim. 6:8-11.

4 Ikiwa unataka kuhama kwa sababu ya kupata manufaa za kibinafsi, kumbuka kwamba popote pale unapoishi, kuna matatizo ya kukabiliana nayo. Ni rahisi kushinda matatizo mahali ambapo tayari unajua lugha na utamaduni, kuliko kuanza maisha katika mazingira mapya usiyoyafahamu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki