Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/01 uku. 3
  • ‘Shughulika kwa Juhudi Nyingi’ na Huduma Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Shughulika kwa Juhudi Nyingi’ na Huduma Yako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Kujishughulisha Sana na Habari Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Aprili—Wakati wa ‘Kufanya Kazi kwa Bidii na Kujikakamua Wenyewe’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Je, Twaweza Kufanya Aprili 2000 Kuwa Mwezi Wetu Bora Zaidi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 4/01 uku. 3

‘Shughulika kwa Juhudi Nyingi’ na Huduma Yako

1 Tunaposoma kwamba mtume Paulo alifanya kazi ya kutengeneza mahema huko Korintho, huenda tukakata kauli kwamba kazi hiyo ilipunguza fursa yake ya kuhubiri. Hata hivyo, Matendo 18:5 husimulia hivi: “Paulo alianza kushughulika kwa juhudi nyingi na lile neno, akiwatolea Wayahudi ushahidi ili kuthibitisha kwamba Yesu ndiye Kristo.” Kwa nini Paulo alishughulika kwa juhudi nyingi na kazi ya kuhubiri? Hata ingawa wengi katika Korintho tayari walikuwa waamini, Bwana alithibitisha kwamba bado kulikuwa na wanafunzi wengi zaidi wa kutafutwa katika jiji hilo. (Mdo. 18:8-11) Je, sisi tuna sababu hiyohiyo ya kushughulika kwa juhudi nyingi na huduma yetu? Ndiyo. Kuna watu wengi zaidi ambao wanaweza kupatikana ili wafunzwe kweli.

2 Tumia Wakati Mwingi Katika Utumishi Mwezi wa Aprili: Labda una mradi wa kujishughulisha sana kuhubiri habari njema kila mwezi. Lakini kuna miezi kadhaa ambayo hutaka ‘tushughulike kwa juhudi nyingi’ na utendaji huu. Miezi hiyo yatia ndani mwezi wa Aprili, kilele cha majira ya Ukumbusho. Je, hali zako zimekuruhusu kufanya upainia-msaidizi au kuongeza jitihada zako katika huduma mwezi huu? Wahubiri wengi ambao wanafanya hivyo wamebarikiwa sana. (2 Kor. 9:6) Ikiwa unafanya yote uwezayo, kumbuka kwamba Yehova anapendezwa na utumishi wako wa nafsi yote. (Luka 21:2-4) Hata hali zako ziwe gani, fanya uwe mradi wako “kushughulika kwa juhudi nyingi” na huduma yako mwezi wa Aprili. Na usisahau kutoa ripoti yako ya utumishi wa shambani mwishoni mwa mwezi ili jitihada zako zihesabiwe pamoja na zile za watu wengine wa Yehova.

3 Tembelea Wapya Waliohudhuria Ukumbusho: Mwaka jana, katika nchi tano zinazosimamiwa na ofisi yetu ya tawi, hudhurio la Ukumbusho lilikuwa 98,077. Twangoja kuona jumla ya hudhurio la mwaka huu. Hata hivyo, ripoti zaonyesha kwamba kuna uwezekano mkubwa ajabu wa “mavuno” makubwa. (Mt. 9:37, 38) Kwa hiyo, mara iwezekanapo, pangia kuwarudia watu wanaopendezwa waliohudhuria Ukumbusho ili uwasaidie kiroho. Kuahirisha ziara hizo kwaweza kumruhusu ‘yule mwovu kunyakua neno la ufalme lililopandwa mioyoni mwao.’ (Mt. 13:19) Kuwarudia mara moja kutaonyesha kwamba wewe kwa kweli ‘unashughulika kwa juhudi nyingi’ na huduma yako.

4 Endelea Kusaidia Wasiotenda: Katika Februari jitihada ya pekee ya kusaidia wasiotenda ilianzishwa. Ikiwa kungali na wale ambao hawajapata ziara za uchungaji, wazee wanapaswa kupanga kuwatembelea kabla ya Aprili kwisha. Wazee watajitahidi kuchunguza sababu ya tatizo la mtu huyo na jinsi watakavyomsaidia ifaavyo amtumikie Yehova kwa bidii tena. Msaada huo wenye upendo waonyesha kwamba wazee wanachukua daraka lao kwa uzito wakiwa wachungaji wa “kundi la Mungu.” (1 Pet. 5:2; Mdo. 20:28) Toleo la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 1993, ukurasa wa 22-23, latoa madokezo bora zaidi yanayoweza kutumiwa na wazee wanaposhughulikia yoyote kati ya yale matatizo matano ya kawaida ambayo huenda yanaathiri wasiotenda. Ikiwezekana, wengine huenda wakachochewa kwenda katika huduma ya shambani mwezi wa Aprili.

5 Saidia Wengi Wawe Wahubiri Wasiobatizwa: Je, watoto wako wamestahili kuwa wahubiri wa habari njema? Vipi wengine ambao unajifunza nao Biblia? Ikiwa wamependekezwa na wazee, je, Aprili haungekuwa mwezi unaofaa kwao kuanza kuhubiri? Ikiwa mtu anafanya maendeleo na amejifunza broshua Anataka, na kitabu Ujuzi, funzo la Biblia laweza kuendelezwa katika kitabu cha pili—kitabu Neno la Mungu, Amani ya Kweli, au Umoja Katika Ibada. Mradi wako ni kusaidia mwanafunzi afikie ufahamu zaidi wa kweli, astahili kuwa mhubiri asiyebatizwa, na kuwa Shahidi wa Yehova aliyejiweka wakfu na kubatizwa.—Efe. 3:17-19; 1 Tim. 1:12; 1 Pet. 3:21.

6 Unapoendelea kupendezwa kikweli na wanafunzi wako wa Biblia huenda hilo likawasaidia kufanya kweli iwe yao hatimaye. Shahidi mmoja alikutana na wenzi wazee ambao walikubali kwa moyo wote kujifunza Biblia. Lakini wenzi hao waliahirisha funzo kwa majuma matatu mfululizo. Hatimaye funzo lilianzishwa. Kisha, wenzi hao wakaahirisha funzo baada ya kila juma moja. Ingawa hivyo, mwishowe, mke alifanya maendeleo kufikia ubatizo. Ndugu huyo akumbuka hivi, “baada ya kubatizwa, macho yake yalijawa na machozi ya furaha, na jambo hilo lilitufanya tutokwe na machozi ya furaha, mimi na mke wangu.” Naam, “kushughulika kwa juhudi nyingi” na habari njema hutuletea shangwe kubwa!

7 Unabii wa Biblia na matukio ya ulimwengu huonyesha kwamba twaishi katika nyakati za mwisho. Sasa ndio wakati ambao watu wa Mungu wanahitaji “kushughulika kwa juhudi nyingi” na kujulisha wengine habari njema. Mtume Paulo anatupa uhakikisho wa kwamba kazi hiyo kwa kweli “si bure kuhusiana na Bwana.”—1 Kor. 15:58.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki