“Nasimama Imara! Nasimama Imara! Nasimama Imara!”
1 Maneno hayo ya Mkristo aliyeokoka yale Maangamizi Makubwa yanaonyesha azimio la maelfu ya Mashahidi—wanaoishi na waliokufa—ambao walikuwa wameazimia kushikilia imani zao ujapokuwa ukatili wa Nazi. (Efe. 6:11, 13) Masimulizi yao yenye kusisimua ya ujasiri na ushindi yanatolewa katika video yenye kuchochea sana ya Jehovah’s Witnesses Stand Firm Against Nazi Assault. Wote katika kutaniko wanatiwa moyo kuitazama na kushiriki maoni yao pamoja na wengine.
2 Maswali yafuatayo na yachochee kufikiri kwako: (1) Kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova walichukua msimamo jasiri kinyume cha wafuasi wa Nazi? (2a) Kulitokea maoni gani yenye kupingana kuhusu salamu, na kwa nini? (2b) Jambo hilo liliathirije familia za Mashahidi? (3) Ni Mashahidi wangapi waliopelekwa kwenye kambi za mateso, nao walitambuliwaje huko, na askari wa Gestapo waliwatendeaje? (4) Ndugu zetu walikataa kufanya nini ili wapate uhuru? (5a) Ni jinsi gani na ni lini Mashahidi wa Yehova waliongea kwa ujasiri kuhusu utawala wa Hitler wenye ukatili? (5b) Hitler alitendaje? (6) Umoja wa watu wa Yehova uliokoaje uhai wao na wa wengine, kimwili na kiroho? (7) Ni wimbo upi wa Ufalme ulioandikwa kwenye kambi ya mateso? (8) Ni mifano gani ya wanaume, wanawake, na vijana waaminifu inayokuchochea uendelee kuwa mwaminifu kwa Yehova hata iweje? (Ona pia 1999 Yearbook, ukurasa wa 144-147.) (9) Ukiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, video hii imekufanya uhisije kuhusu kutokuwa sehemu ya ulimwengu?
3 Mfano wa ujasiri wenye kutia moyo wa Mashahidi wa Yehova unaoonyeshwa katika video Stand Firm waweza kusaidia vijana, hata wale ambao si Mashahidi, kukabiliana na masuala ya ubaguzi, msongo wa marika, na dhamiri. Ikiwa wewe ni kijana anayehudhuria shule ya upili au chuo, je, waweza kuwapa walimu wako fursa ya kutumia video hii darasani? Labda waweza kuwapa nakala ya video hiyo kama inapatikana na uwaambie kuwa inaonyesha mambo ya historia yasiyojulikana sana au ni simulizi lenye somo la maadili.
4 Video Stand Firm ni kifaa bora kabisa cha kuonyesha jinsi ufundishaji wa kimungu hutupa nguvu ya kiroho ya kumpendeza Mungu kwa kudumu tukiwa imara kwa ajili ya yaliyo sawa. (1 Kor. 16:13) Itazame pamoja na wote wanaopendezwa na kweli.