Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/02 kur. 3-4
  • Tuna Kifaa Kipya cha Kuanzisha Mafunzo!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tuna Kifaa Kipya cha Kuanzisha Mafunzo!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Itumie Vizuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Tumia Trakti Kuanzisha Mazungumzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Uwe Tayari Kila Wakati Kuanzisha Funzo la Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 6/02 kur. 3-4

Tuna Kifaa Kipya cha Kuanzisha Mafunzo!

1 Mwanamke mmoja Mmarekani alikuwa Mkatoliki aliyejitoa sana. Alitetea mafundisho ya kanisa kwa uaminifu. Hata wakati mmoja alifunga safari ya kwenda Vatikani. Lakini, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alipomtembelea, alikubali funzo la Biblia la nyumbani. Kwa nini? Kwa sababu alitaka kujifunza kile ambacho Biblia husema na kanisa lake halikumpa fursa ya kuwa na funzo la Biblia. Jambo hilo latufundisha nini? Kwamba hatujui kamwe ni nani atakayekubali funzo la Biblia bila malipo.—Mhu. 11:6.

2 Je, umewahi kusitasita kuwaambia watu kwamba tuko tayari kujifunza Biblia pamoja na mtu yeyote anayependezwa? Je, kila mtu katika ujirani wako anajua kwamba sisi hutoa huduma hii bila malipo? Twaweza kuhakikishaje kwamba wanajua hivyo? Kwa kutumia kifaa kipya! Kifaa chenyewe ni trakti yenye kupendeza ya kurasa sita yenye kichwa Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? Na tuchanganue vichwa vidogo vya trakti hii hatua kwa hatua.

3 “Kwa Nini Uisome Biblia?” Sababu ambazo zapatikana katika trakti hiyo zapendeza sana. Hueleza kwamba Biblia ina “mafundisho yenye upendo kutoka kwa Mungu,” ikionyesha jinsi ya kumfikia katika sala ili upate msaada na jinsi ya kupokea zawadi ya uhai udumuo milele. (1 The. 2:13) Trakti hiyo yataja “kweli zinazoweza kutuelimisha,” kama vile ni nini kinachotupata tunapokufa na kwa nini kuna matatizo mengi sana duniani. Hueleza juu ya “kanuni za Mungu zinazopatikana katika Biblia” ambazo zikitumiwa, huleta manufaa za kimwili na kuleta furaha, tumaini na sifa nyingine zenye kupendeza. Trakti hiyo yataja sababu nyingine ya kujifunza Biblia—unabii kuhusu wakati ujao ambao waonyesha yatakayotokea hivi karibuni.—Ufu. 21:3, 4.

4 “Msaada wa Kuielewa Biblia”: Trakti hiyo yasema hivi: “Sote tunahitaji kusaidiwa ili kuelewa Neno la Mungu.” Kisha yaeleza njia tunayotumia kujifunza Biblia: “Kwa kawaida inakuwa vizuri kuisoma Biblia hatua kwa hatua, ukianza na mafundisho ya msingi.” Ikieleza wazi kwamba “Biblia ndiyo chanzo cha kweli hizo,” trakti hiyo yaitaja broshua Anataka kuwa kitu kitakachomsaidia mwanafunzi “kuelewa Maandiko yanayozungumzia habari mbalimbali.” Kichwa kinachofuata kina swali lenye kuchochea.

5 “Je, U Tayari Kutumia Wakati Kila Juma Kuielewa Biblia?” Trakti yaeleza kwamba funzo la Biblia laweza kupangwa wakati na mahali panapomfaa mwanafunzi, iwe ni nyumbani kwake mwenyewe, au hata kupitia simu. Ni nani anayeweza kushiriki mazungumzo hayo? Trakti hiyo yajibu hivi: “Familia yako yote na yeyote kati ya marafiki wako ambaye utapenda kualika. Mazungumzo hayo yanaweza kufanywa nawe peke yako ikiwa unataka hivyo.” Lazima mtu ajifunze kwa muda gani? Yasema hivi: “Wengi hutenga muda wa saa moja kila juma ili kujifunza Biblia. Ikiwa unaweza kupata muda mwingi zaidi au hata ikiwa muda unaoweza kupata kila juma ni mfupi, Mashahidi watakuwa tayari kukusaidia.” Hilo ndilo jambo la maana! Tuko tayari kurekebisha hali zetu ili zifaane na hali ya kila mwanafunzi.

6 “Unaalikwa Kujifunza”: Kuna kuponi ambayo mwenye kupokea trakti hii anaweza kujaza na kuomba broshua Anataka au atembelewe na kuelezwa mpango wetu wa funzo la Biblia la nyumbani bila malipo. Jalada la broshua Anataka limeonyeshwa kwa rangi kamili. Je, waweza kuona jinsi trakti hii itakavyotia moyo watu wenye mioyo minyoofu kukubali msaada wetu? Sasa, twaweza kutumiaje kifaa hiki vizuri zaidi?

7 Ni Nani Unayeweza Kumwachia Trakti Hiyo? Trakti hiyo yaweza kuachiwa mtu binafsi au yaweza kuachwa mahali usipokuta mtu nyumbani. Yaweza kugawanywa nyumba kwa nyumba, barabarani, na kwenye eneo la kibiashara. Waachie watu iwe wanakubali vichapo vyetu au la. Iweke ndani ya magazeti au vichapo vingine ambavyo unaachia watu. Iingize ndani ya barua. Watumie wale unaowapigia simu. Zibebe sikuzote ili uwaachie watu unapokwenda dukani, unaposafiri kwa gari la umma, na unapofanya mahubiri yasiyo rasmi. Mpe yeyote anayekutembelea. Wape watu wa ukoo, majirani, wafanyakazi wenzako, wanafunzi wenzako, na wengine unaowajua. Jitahidi kumpa kila mtu unayekutana naye trakti hii! Kisha?

8 Mtu Akikubali Mara Moja: Watu fulani watakubali mara moja kwa kusema kwamba wangependa kujifunza Biblia. Kwa hiyo, wakati wowote unapokuwa katika utumishi wa shambani, hakikisha kwamba sikuzote una nakala mbili za broshua Anataka—moja ya mwanafunzi na nyingine yako. Ikiwa mtu huyo yuko tayari, anzisha funzo papo hapo. Fungua ukurasa wa kwanza, na usome “Jinsi ya Kutumia Broshua Hii.” Kisha muanze somo la 1 na umwonyeshe jinsi ya kujifunza. Ni rahisi, sivyo?

9 Ikiwa Msikilizaji Wako Anahitaji Wakati wa Kufikiria: Jitahidi kumrudia kabla ya muda mrefu kupita. Unapomrudia, hakikisha umebeba broshua Anataka. Mwonyeshe yaliyomo. Mwache achague somo linalompendeza. Fungua hapo, na mwanze kuzungumzia somo alilochagua.

10 Rudia Watu Waliochukua Magazeti: Ikiwa ulimwachia mtu trakti pamoja na magazeti, unaweza kurudi umwambie: “Nilipokutembelea wakati uliopita, nilikuachia gazeti la Mnara wa Mlinzi. Labda uligundua kwamba kichwa kizima cha jarida hilo ni Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova. Leo ningependa kukueleza Ufalme huo ni nini na utamaanisha nini kwako na kwa familia yako.” Kisha fungua broshua Anataka somo la 6. Mkianza na fungu la kwanza, someni na mzungumzie mengi zaidi maadamu mwenye nyumba ana wakati. Kisha fanya mipango ya kurudi siku nyingine mmalizie somo hilo.

11 Usikose Trakti: Mwangalizi wa utumishi na akina ndugu wanaoshughulikia vichapo watahitaji kuwa na trakti nyingi za Kujua Biblia kutanikoni sikuzote. Weka baadhi yazo katika mfuko wako au kibeti, katika gari lako, kazini, shuleni, karibu na mlango wa nyumba yako—mahali popote zitakapoweza kupatikana kwa urahisi. Beba nyingine katika mkoba wako wa mahubiri kwa ajili ya wakati ambapo utakutana na mtu unayeweza kuongea naye juu ya Biblia.

12 Yehova na Abariki Jitihada Zetu: Mradi wenye kupendeza wa kila Mkristo ni kumfundisha mtu mwingine kweli. (Mt. 28:19, 20) Je, unaongoza funzo la Biblia wakati huu? Ikiwa unafanya hivyo, unaweza kupata nafasi ya kuongoza lingine katika ratiba yako ya kila juma? Ikiwa huongozi funzo wakati huu, bila shaka ungependa kufanya hivyo. Mwombe Yehova abariki jitihada zako ili upate mtu unayeweza kujifunza naye. Kisha tenda kulingana na sala hizo.—1 Yoh. 5:14, 15.

13 Tuna kifaa kipya cha kuanzisha mafunzo! Kisome. Waachie watu wengi iwezekanavyo. Fanya yote uwezayo ‘kufanya mema, kuwa tajiri katika kazi zilizo bora, kuwa mkarimu, tayari kushiriki’ yale ambayo umejifunza kuhusu Neno la Mungu.—1 Tim. 6:18.

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

FURSA ZA KUGAWANYA TRAKTI

◼ Katika mazungumzo ya kila siku

◼ Mtu anapokubali kichapo chetu

◼ Tunapokosa mtu nyumbani

◼ Tunapofanya ziara za kurudia

◼ Tunapokutana na mtu barabarani

◼ Tunapohubiri katika eneo la kibiashara

◼ Tunapofanya mahubiri yasiyo rasmi

◼ Tunapoandika barua

◼ Tunaposafiri kwa magari ya umma

◼ Mtu anapotutembelea

◼ Tunapoongea na watu wa ukoo, majirani, wafanyakazi wenzetu, wanafunzi wenzetu, na watu wengine tunaowajua

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki