Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/10 uku. 2
  • Uwe Tayari Kila Wakati Kuanzisha Funzo la Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Tayari Kila Wakati Kuanzisha Funzo la Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Tuna Kifaa Kipya cha Kuanzisha Mafunzo!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Itumie Vizuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Kazia Uangalifu Kazi ya Kufanya Wanafunzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Je! Unatoa Mafunzo ya Biblia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 6/10 uku. 2

Uwe Tayari Kila Wakati Kuanzisha Funzo la Biblia

1. Tunapaswa kufanya nini ili kutimiza agizo la Yesu katika Mathayo 28:19, 20?

1 Yesu alitupa agizo la ‘kufanya wanafunzi na kuwafundisha.’ (Mt. 28:19, 20) Kwa hiyo, tungependa kuwa tayari kila wakati kuanzisha funzo la Biblia, na tusingojee tu ile siku ya mwisho-juma ambayo imeteuliwa kwa kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Madokezo yanayofuata yanaweza kuwa na matokeo.

2. Tunaweza kuwaeleza kina nani kuhusu mpango wa kujifunza Biblia?

2 Waeleze Kuhusu Mpango wa Kujifunza: Kadiri tunavyowaeleza watu wengi zaidi kuhusu mpango wa kujifunza Biblia, ndivyo tunavyokuwa na fursa nyingi zaidi za kupata funzo. (Mhu. 11:6) Je, umejaribu njia ya moja kwa moja ya kuanzisha funzo la Biblia? Kutaniko moja huko Marekani lilifanya jitihada za pekee za kutumia njia hiyo kwa mwezi mmoja. Walifurahi kama nini kuanzisha mafunzo ya Biblia mapya 42! Usidhani kwamba watu wanaopendezwa ambao unawahubiria wanajua kuwa ungependa kujifunza Biblia pamoja nao. Unapowarudia, waeleze kuhusu mpango wa kujifunza. Hata wakikataa kujifunza, hakuna shida. Unaweza kuendelea kuwatia moyo watu hao wenye kupendezwa. Je, umewauliza majirani zako, watu wako wa ukoo, wafanyakazi wenzako, na wanashule wenzako kama wangependa kujifunza Biblia pamoja nawe? Unaweza pia kuwauliza wanafunzi wako wa Biblia kama wana marafiki au watu wa ukoo ambao wangefurahia kujifunza Biblia.

3. Tuna kifaa kipi muhimu cha kutusaidia kuanzisha mafunzo ya Biblia, na tunaweza kukitumia wakati gani?

3 Kifaa cha Kutusaidia: Trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? ni kifaa muhimu cha kutusaidia kuanzisha mafunzo ya Biblia. Unaweza kuwaachia wenye nyumba trakti hiyo, wawe wamekubali vitabu vyetu vya Biblia au la. Unaweza kuitumia unapohubiri maeneo ya biashara, barabarani, unapohubiri kwa barua, na unapowarudia wale waliopendezwa. Pia, unaweza kuiacha katika nyumba zisizo na watu. Beba trakti hiyo unaposafiri kwa magari ya umma, unaponunua vitu, au unapokuwa kazini. Ukurasa wa nyuma wa trakti hiyo unaeleza kuhusu mpango wetu wa kujifunza Biblia na pia unaonyesha kitabu Biblia Inafundisha.

4. Tunawezaje kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia trakti Kujua Ukweli?

4 Baada ya kumpa mtu trakti hiyo, unaweza kumwonyesha maswali kwenye ukurasa wa kwanza na kumuuliza, “Unapendezwa na swali gani kati ya haya?” Kisha pitia pamoja naye jibu lililo kwenye trakti, na usome au uzungumzie ukurasa wa nyuma ambao unaeleza juu ya mpango wa kujifunza Biblia. Unaweza pia kumwonyesha ukurasa unaozungumzia swali hilo kwa undani zaidi katika kitabu Biblia Inafundisha. Mtolee kitabu hicho na ufanye mipango ya kurudi tena ili kuendeleza mazungumzo.

5. Kwa nini tunapaswa kuwa tayari wakati wote kuanzisha funzo la Biblia?

5 Katika eneo letu, bado kuna watu wanaotamani kujua mambo ambayo Biblia inafundisha hasa. Hivyo, tunapokuwa tayari kila wakati kuanzisha funzo la Biblia, tutakuwa na fursa nyingi zaidi za kupata shangwe ya kuwasaidia wengine waingie katika barabara inayoelekea kwenye uzima.—Mt. 7:13, 14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki