Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/15 uku. 1
  • Kazia Uangalifu Kazi ya Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazia Uangalifu Kazi ya Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Uwe Tayari Kila Wakati Kuanzisha Funzo la Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Je, Unaweza Kushiriki Katika Kazi ya Kufanya Wanafunzi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • ‘Nendeni Mkafanye Wanafunzi’—Je! Wewe Unafanya Hivyo?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Fundisha Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 7/15 uku. 1

Kazia Uangalifu Kazi ya Kufanya Wanafunzi

1. Tunahitaji kufanya nini ili watu waokolewe?

1 Ripoti ya mwaka wa 2014 inaonyesha bidii na azimio la watu wa Mungu la kuhubiri habari njema ya Ufalme. (Mt. 24:14) Kupitia kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba, kampeni za pekee za kusambaza trakti na mialiko, na mahubiri ya hadharani, watu wengi wanapata ujumbe wa Biblia kuliko wakati mwingine wowote. Hata hivyo, ili watu waokolewe, ni lazima tuwasaidie wawe wanafunzi wa Yesu kwa kujifunza Biblia pamoja nao.—1 Tim. 2:4.

2. Ni maswali gani yanayoweza kutuchochea kuwa tayari kuanzisha funzo la Biblia?

2 Sikuzote Uwe Tayari Kuanzisha Funzo la Biblia: Je, wewe hujitahidi kuchukua anwani au namba za simu za wale wanaopendezwa na kuwatembelea au kuwapigia simu bila kukawia ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia? Ni lini mara ya mwisho ulipojaribu kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza? Ni lini mara ya mwisho ulipojaribu kuanzisha funzo la Biblia na wale unaowaachia magazeti kwa ukawaida? Je, umewahi kutumia video Kwa Nini Ujifunze Biblia? na Ni Nini Hutendeka Kwenye Funzo la Biblia? unapowahubiria wafanyakazi wenzako, wanafunzi wenzako, jirani zako, watu wako wa ukoo, na watu wengine unaowafahamu? Unapohubiri kwa kutumia vigari vyenye machapisho, je, wewe hujitahidi kuwaeleza wale wanaochukua machapisho yetu kuhusu mpango wa kujifunza Biblia bila malipo?

3. Tunahitaji kufanya nini ili kufundisha kweli kwa njia yenye matokeo?

3 Msaada Kutoka kwa Yehova na Yesu: Yesu alianza na neno “nendeni,” alipotoa amri ya ‘kufanya wanafunzi’ na hivyo akaonyesha kwamba tunahitaji kuwa wenye bidii na kuchukua hatua ya kwanza. Hata hivyo, hakutuacha peke yetu bali aliahidi kuwa pamoja nasi. (Mt. 28:19, 20) Kwa kuongezea, Yehova ametupatia roho yake takatifu, na pia vifaa na mazoezi tunayohitaji ili tuweze kuwafundisha watu kweli. (Zek. 4:6; 2 Kor. 4:7) Tunaweza kusali ili tuwe “na nia” na uwezo wa kushiriki katika kazi hiyo muhimu.—Flp. 2:13.

4. Kwa nini tunapaswa kukazia uangalifu kazi ya kufanya wanafunzi?

4 Tunapata furaha tele tunapohubiri habari njema. Hata hivyo, shangwe yetu inaongezeka zaidi tunapomfundisha mtu kweli na kumsaidia ajiunge nasi katika “barabara inayoongoza kwenye uzima.” (Mt. 7:14; 1 The. 2:19, 20) Jambo la maana hata zaidi ni kwamba tunapokazia uangalifu kazi ya kufanya wanafunzi, tunampendeza Yehova ambaye “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.”—2 Pet. 3:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki