Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Tumewahi kusikia msemo huu ‘Yesu alikufa kwa ajili yetu.’ [Nukuu Yohana 3:16.] Je, umewahi kujiuliza jinsi kifo cha mtu mmoja kinavyoweza kutuokoa sote? [Ngoja jibu.] Biblia hutoa jibu rahisi. Makala hii yenye kichwa, ‘Yesu Huokoa—Jinsi Gani?,’ inaeleza jambo hilo waziwazi.”
Amkeni! Nov. 22
“Je, unafikiri wanadamu wanajitahidi vya kutosha kuhifadhi mazingira? [Ngoja jibu.] Watu wengi hujiuliza kama viumbe na mazingira yatadumu milele. Jambo zuri ni kwamba Mungu anapendezwa sana na suala hilo. [Soma Nehemia 9:6.] Gazeti la Amkeni! huzungumzia mahangaiko kuhusu mazingira na mambo ambayo yatatukia wakati ujao kwa viumbe vilivyomo duniani.”
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Katika kipindi hiki cha mwaka, watu wengi wanajishughulisha sana kutoa zawadi na kuwatendea wengine kwa fadhili. Hilo linatukumbusha ile Kanuni Bora. [Soma Mathayo 7:12.] Je, wafikiri inawezekana kufuata kanuni hiyo sikuzote? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linatoa habari nyingi za kufikiria kuhusu kichwa hiki ‘Ile Kanuni Bora—Je, Bado Inafaa?’”
Amkeni! Des. 8
“Biblia inaahidi kwamba siku moja hakuna atakayesema, ‘mimi mgonjwa.’ [Soma Isaya 33:24.] Kwa kupatana na ahadi hiyo, toleo hili la Amkeni! linazungumzia ugonjwa unaokumba mamilioni ya watu, vijana kwa wazee. Lina kichwa hiki ‘Tumaini kwa Wale Wanaougua Yabisi-Kavu.’ Nina hakika kwamba makala hizi zitakuarifu mambo mengi.”