Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 15
“Mahali popote ambapo watu wanaishi, wanatamani kuwa na usalama, hasa usalama unaopatikana kwa kuwa na kazi nzuri. Lakini umewahi kuwazia kama kuna chanzo cha usalama wa kudumu, utakaokuwezesha uwe salama milele? [Soma Zaburi 16:8, 9.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linachunguza mahali tunapoweza kupata usalama wa kweli.”
Amkeni! Apr. 22
“Watu wengi leo wanaacha dini zao ili kumwabudu Mungu jinsi wapendavyo. Unaonaje mwelekeo huo? [Ngoja ajibu.] Biblia huonyesha kwamba jinsi tunavyomwabudu Mungu ni muhimu. [Soma Yohana 4:24.] Toleo hili la Amkeni! laonyesha njia bora zaidi ya kutosheleza mahitaji yako ya kiroho.”
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Unajua mtu yeyote ambaye ni mgonjwa sana au ni mlemavu? Bila shaka unakubali kwamba watu kama hao wanahitaji kutiwa moyo. Lakini twaweza kusema nini ili kuwatia moyo? Biblia inatoa tumaini. [Soma Isaya 35: 5, 6.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi laeleza kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba unabii huu utatimia.”
Amkeni! Mei 8
“Mwaka uliopita, ulikuwa mwaka uliokosa amani kuliko wakati mwingine wowote. Je, unafikiri kwamba serikali za binadamu zaweza kuleta amani ulimwenguni pote? [Baada ya jibu, soma Isaya 2:4.] Toleo hili la Amkeni! laonyesha ni kwa nini twaweza kuwa na uhakika kwamba hivi karibuni kutakuwa na amani ulimwenguni pote.”