Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/02 uku. 4
  • “Sikuzote Fuatieni Lililo Jema”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Sikuzote Fuatieni Lililo Jema”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Mkusanyiko wa Wilaya wa 1999 wa “Neno la Mungu la Kiunabii” wa Mashahidi wa Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Uwe Kielelezo Katika Kazi Zilizo Bora
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova la 2008
    Huduma ya Ufalme—2007
  • “Acheni Mambo Yenu Yote Yatendeke kwa Upendo”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 5/02 uku. 4

“Sikuzote Fuatieni Lililo Jema”

1 Njia ya maisha ya Mkristo yamaanisha ‘sikuzote kufuatia lililo jema kuelekea watu wote.’ (1 The. 5:15) Tunapohudhuria makusanyiko yetu ya wilaya, tuna fursa nyingi za kuwatendea wengine mema. Katika pindi hizo, huwa tunatazamwa na watu wote, na maoni ya wale tunaokutana nao hutegemea jinsi tunavyowatendea. Ili kuwa na sifa nzuri tukiwa Mashahidi wa Yehova, twahitaji kuonyesha kwa matendo yetu kwamba ‘tunawaheshimu watu wa namna zote.’ (1 Pet. 2:17) Hiyo yatia ndani “kuangalia, si masilahi ya kibinafsi ya mambo [yetu] wenyewe tu, bali pia masilahi ya kibinafsi yale ya wengine.” (Flp. 2:4) Fikiria jinsi tunavyoweza kufanya hivyo kuhusiana na mipango ya mahali pa kulala.

2 Je, umefanya mipango ya mahali pa kulala? Utalala hotelini, katika bweni au kwenye darasa? Fanya matayarisho mapema ya matandiko, chakula, na kinga za mbu na maji safi ya kunywa. Tii sheria zote zilizowekwa na wasimamizi wa shule au mahali penginepo pa kulala ili kuepuka hatari za moto. Katika madarasa na mabweni mengi, watu hawaruhusiwi kupika.

3 Kufundisha Watoto Jinsi ya Kutenda Mema: Watoto wasiachwe kamwe bila mtu mzima mahali pa kulala kwa kuwa matatizo yanaweza kutokea. (Mit. 29:15) Ikiwa kuna kidimbwi cha kuogelea au mahali penginepo pa tafrija, watoto hawapaswi kuruhusiwa kwenda huko hasa bila wazazi wao. Wote wanapaswa kuwa waangalifu wasiwasumbue wengine.

4 Wazazi, kabla ya kusanyiko ingefaa kama mngetumia wakati fulani kuzungumza na watoto wenu jinsi wanavyopaswa kujiendesha nyakati zote na kila mahali. (Efe. 6:4) Kwa mfano, waambieni kwamba upendo wa Kikristo “haujiendeshi bila adabu, hautafuti masilahi yao wenyewe, haupati kuwa wenye kuchokozeka.” (1 Kor. 13:5) Watu wazima wanaweza kukazia maneno hayo kwa kuwekea wote mfano bora. Watoto, mwaweza kufuatia lililo jema kwa kutii wazazi wenu, kutoharibu vitu, na kujali walio karibu nanyi. (Kol. 3:20) Tunapojitahidi kwa umoja kuwatendea wengine mema, ‘twaremba fundisho la Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote.’—Tito 2:10.

5 Mwenendo wetu mwema una matokeo mazuri, si kwa watazamaji tu, bali pia kwa wale ambao wamekuwa wakituchambua kwa sababu mbalimbali. Chochote tufanyacho kusanyikoni—iwe twatembea barabarani, twala mkahawani, twapumzika kwenye hoteli, katika bweni, darasani, au twashiriki katika mahubiri yasiyo rasmi—twapaswa kuthibitisha kwamba twataka kufuatia lililo jema kwa usemi wetu na matendo yetu ya Kikristo.

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

Tafadhali Kumbuka:

■ Uwe mwenye subira na uheshimu wafanyakazi wa mahali pa kulala.

■ Tii sheria za mahali hapo kwa manufaa ya wageni wote.

■ Epuka chochote ambacho chaweza kuanzisha moto.

■ Angalia jinsi watoto wako wanavyojiendesha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki